"Kipe Kitu" ni jina la wimbo uliotungwa na kuimbwa na kundi zima la muziki wa hip hop kutoka nchini Tanzania, G.W.M. Wimbo umetayarishwa na Bonny Luv ndani ya Mawingu Studio. Wimbo huu ulitoka mwaka 1996, wa pili kutolewa baada ya Cheza Mbali na Kasheshe. Moja kati ya nyimbo za miaka ya 1990 zilizobamba kupita maelezo. Hata kwa GWM walionekana tishio hasa kwa vijana kutoka Temeke. Wimbo unatoka katika albamu ya Mikosi.

"Kipe Kitu"
"Kipe Kitu" kava
Wimbo wa G.W.M

kutoka katika albamu ya Mikosi

Umetolewa 1996
Umerekodiwa 1996
Aina ya wimbo Hip hop
Urefu 3:00
Studio Mawingu Studios
Mtunzi G.W.M
Mtayarishaji Bonny Luv
Mikosi orodha ya nyimbo
  1. A1 Yamenikuta
  2. A2 - Bwana Kidevu
  3. A3 - Mguu Nje
  4. A4 - Kipe Kitu
  5. A5 - Mguu Nje Instru.
  6. B1 - Mikosi
  7. B2 - Mwenye Nyumba
  8. B3 - Machizi Wangu
  9. B4 - Autro
  10. B5 - Machizi Wangu Instru.


Viungo vya Nje hariri