Mikosi, ni jina la albamu ya kwanza kutoka kwa kundi zima la muziki wa hip hop la Temeke Dar es Salaam, Tanzania maarufu kama G.W.M. Albamu imetoka mwaka wa 2000 - ukiwa mwaka wa matoleo mengi ya albamu za hip hop ya Tanzania kutoka. Hamasa ya kutoa albamu na kufanya uzinduzi zama hizi ndiyo hasa zilitamba. G.W.M ni moja kati ya makundi yanayoheshimika katika miaka ya 1990.

Mikosi
Mikosi Cover
Studio album ya G.W.M
Imetolewa 2000
Aina Hip hop
Lebo GMC
Mtayarishaji Rajabu Marijani
Bonny Luv

Walikuwa kufahamika haraka nchini Tanzania kwa ujuvi wao wa utunzi wa mashairi ulioendana na wakati ule. Walianza kutamba mwaka 1995 baada ya kutoa wimbo wa "Cheza mbali na kasheshe". Albamu hii ilitakiwa itoke tangu miaka ya 1990, lakini mipango ya kusaini mkataba wake ilienda kombo na kuja kutoka mwaka wa 2000, mbele kidogo baada ya kuvuma kwa sana. KR baaaye akajiunga na kundi la muda mfupi la Wachuja Nafaka. Nyimbo za katika albamu zilitayarishwa na Bonny Luv na Rajabu Marijani.

Orodha ya nyimbo hariri

 
Zama zile ilikuwa lazima utie saini katika kila kanda itakayotoka ili kuonesha uhalali wa usambazwaji huo. Hii ni moja kati ya mihuri ya GWM iliyoonesha kuidhinishwa kwa kazi hii. Ingawa kulikuwa na malalamiko mengi sana juu ya uhujumu wa mauzo ya kanda kwa wakati huo.

Hii ni orodha ya nyimbo zinazopatika katika albamu hii na maelezo yake ya msingi.

Upande Jina la wimbo Maelezo
A1 Yamenikuta Wakiwa na II Proud
A2 Bwana Kidevu Wakiwa na G. Solo na Mc Steav
A3 Mguu Nje Wakiwa na Dolla Soul
A4 Kipe Kitu Ilivuta hisia kwa watu wengi wakati ule
A5 Mguu Nje Instru. Midundo mitupu
B1 Mikosi Wakiwa na Dre'z
B2 Mwenye Nyumba Wakiwa na Dre'z
B3 Machizi Wangu Wakiwa na Sloughter
B4 Autro
B5 Machizi Wangu Instru. Midundo mitupu

Kikosi kazi hariri

Viungo vya Nje hariri

  • Mikosi katika wavuti ya Discogs