Ndugu, Pwanyonyi, twamfurahia kila mmoja anayeingia na kuungana nasi. Kwa sasa hivi, utaniona sana mimi (Muddyb) na Mr Accountable ambao tunaonekana mara kwa mara! Pia, nitoe shukrani zangu kwako kwa kutayarisha Orodha ya Marais Wa Marekani. Lakini pia kusikitika kwa kukueleza kwamba makala hiyo tayari ipo kwenye Wikipedia hii! Makala ina kwenda kwa jina la Orodha ya Marais wa Marekani. Tofauti yake ni wewe ulipoweka "Wa" herufi kubwa badala ya ndogo. Si kitu. Uoni kama afadhali una-kili baadhi ya maelezo na uyaweke ndani ya ukurasa wa awali? Halafu ile makala nyingine tuifute! Tafakari...--Muddyb MwanaharakatiLonga 12:55, 9 Novemba 2009 (UTC)Reply

Sawa ndugu, hamna wasiwasi. Nashukuru. Pwanyonyi (majadiliano) 06:03, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Ahsante kwa jibu lako! Je, ungependa kuchukua yale maelezo na kuyaweka kwenye ule ukurasa wa awali? Halafu? Haya, basi endelea! Wako,Muddybau,--Muddyb MwanaharakatiLonga 06:26, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Nitayaweka, lakini mwanzo nitauhariri ukurasa wake Obama ili kujumlisha kiungo kwenye ukurasa wa wa awali wa marais, na kishaye, pole pole, niyajumlishe maelezo ya ukurasa niliouongeza kwenye ule wa awali. Pwanyonyi (majadiliano) 06:31, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Haya, basi taratibu ndugu! Ukimaliza hatua "a" na "b", tumaini langu itavutia! Mengineyo: ungependa kuanzia ukurasa wako wa mtumiaji? Yaani, pale kuwe kunaonekana yale maarifa ya lugha na kadhalika! Ni hayo tu, basi!--Muddyb MwanaharakatiLonga 07:25, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Sasa tunaanza kutishana, kaka! Duh! Kiingereza nne? Ninadhani wewe ni mtu wa Kenya, siyo? Haya, tuendelee!!!--Muddyb MwanaharakatiLonga 07:35, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Kweli, mimi Mkenya... :) Pwanyonyi (majadiliano) 07:40, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply
Ndugu, tafadhali tazama majadiliano haya.--Muddyb MwanaharakatiLonga 07:52, 10 Novemba 2009 (UTC)Reply