Mbuga ya Wanyama ya Mahang

Mbuga ya Wanyama ya Mahango (pia inajulikana kama Hifadhi ya Wanyama ya Mahango [1] ) ni eneo lililohifadhiwa nchini Namibia ndani ya Mbuga ya taifa ya Bwabwata . [2] Iko katika mpaka wa mashariki wa nchi hiyo na Botswana katika tambarare za mafuriko ya bonde la Mto Okavango, karibu na Maporomoko ya Popa kwenye mto huo.

Ukanda wa Caprivi .

Ukanda wa Caprivi hufunika sehemu ya magharibi ya mbuga hiyo. [3] Ilianzishwa mwaka 1986 na ina eneo la hektari 24,462.

Ina zaidi ya aina 300 za ndege, imeteuliwa kuwa Eneo Muhimu la Ndege na shirika la BirdLife International . Takribani theluthi mbili ya spishi za ndege wanaopatikana Namibia wanapatikana hapa kwani inajumuisha aina zote mbili za ardhi oevu na za kitropiki za nchi kavu. [4]

Marejeo hariri

  1. "Mahango Game Reserve". Namibian.org. Iliwekwa mnamo May 9, 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. "Protected Areas Network Map". Ministry of Education and Tourism. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2014-12-04. Iliwekwa mnamo 2013-05-08. 
  3. "Mahango National Park". Info Namibia.com. Iliwekwa mnamo 6 May 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  4. "Mahango Game Reserve and Kavango River". BirdLife International Organization. Iliwekwa mnamo 6 May 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)