Mimi ni Mkenya.

Napenda maswala ya mtandao, teknolojia, tarakilishi na pia magari. Huwa naandika na kuhariri maswala haya. Nina shahada ya somo la Takwimu (BSc Statistics) kutoka chuo kikuu cha Nairobi. Vile vile nina diploma ya somo la teknolojia na mawasiliano (Information and Communication Techonology, ICT Diploma).

Nimefurahi kwa mradi huu wa Wikipedia ya Kiswahili ambapo naweza kuchanga na pia kutafsiri kutoka kwa wikipedia ya Kizungu. Nakipenda Kiswahili ijapokuwa watu wengi huona kana kwamba Kiswahili cha Kenya kimeyumbishwa na viswahili vya mitaa (sheng)