Mume ni binadamu wa jinsia ya kiume ambaye ameoana na mwanamke.

Ndoa ya Kiyahudi ilivyochorwa na Jozef Israëls, 1903.

Katika adhimisho la ndoa, mwanamume anaitwa pia bwana arusi.

Mwanamume wa namna hiyo anaendelea kuitwa mume hadi ndoa ivunjike kwa kifo cha mkewe (hapo ataanza kuitwa "mjane") au kwa talaka (hapo ataanza kuitwa "mtaliki").

Utengano haumuondolei hadhi ya kuwa mume wala haki zinazoendana nayo kadiri ya sheria na desturi za jamii husika.