Sheria

mfumo wa sheria na miongozo, ambayo kwa ujumla inaungwa mkono na mamlaka ya serikali

Makala hii ina dalili ya kutungwa kwa kutegemea programu ya kompyuta kama "google translation" au "wikimedia special:content translation" bila masahihisho ya kutosha. Watumiaji wanaombwa kuchunguza lugha, viungo na muundo wake tena. Wakiridhika na hali yake wanaweza kuondoa kigezo hiki kinachoonekana kwenye dirisha la kuhariri juu ya matini ya makala kwa alama za {{tafsiri kompyuta}} .

Sheria (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza law [4]) ni mfumo wa kanuni, ambazo kwa kawaida hutekelezwa kupitia seti ya taasisi maalumu.[5] Inaunda siasa, uchumi na jamii kwa njia mbalimbali na huratibu mahusiano baina ya watu.

Mwanamke wa Haki ni ishara ya idara ya sheria.[1][2] Haki inaonyeshwa kama mungu jike ambaye anabeba ishara tatu za utawala wa kisheria: upanga unaoashiria nguvu ya mahakama; mizani zinazoashiria upimaji wa madai yanayoshindana; na kitambaa kinachofunika macho kuashiria kutofanya upendeleo.[3]

Sheria ya mkataba huongoza kila kitu, kuanzia kununua tiketi ya basi hadi biashara katika masoko.

Sheria ya mali inafafanua haki na wajibu unaohusiana na uhamisho wa jina la mali ya binafsi na mali ya kweli.

Sheria ya hifadhi inatumika kwa mali yanayotumika kwa uwekezaji na usalama wa kifedha, huku sheria ya kukiuka wajibu inaruhusu madai ya fidia ikiwa haki au mali za mtu zinafanyiwa madhara.

Ikiwa madhara ni kinyume cha sheria, sheria ya jinai inatoa mbinu zinazoweza kutumiwa na taifa ili kumshtaki mhusika.

Sheria ya kikatiba inatoa utaratibu wa utungaji wa sheria, ulinzi wa haki za kibinadamu na uchaguzi wa wawakilishi wa kisiasa.

Sheria ya utawala inatumika kuangalia upya maamuzi ya vyombo vya serikali, huku sheria ya kimataifa inatawala shughuli baina ya nchi huru zinazohusu mambo kama vile biashara, vikwazo vya kimazingira na hatua za kijeshi.

Akiandika mnamo 350 K.K., mwanafalsafa wa Ugiriki ya Kale Aristotle alisema, "Utawala wa sheria ni bora kuliko utawala wa mtu yeyote binafsi."[6]

Mifumo ya sheria inaelezea haki na majukumu kwa njia mbalimbali. Tofauti ya jumla inaweza kufanywa kati ya maeneo yanayotawaliwa na mfumo wa sheria ya kiraia, ambayo huandika sheria zao, na yale yanayofuata sheria za kawaida, ambapo sheria haijaundwa kwa utaratibu maalumu. Katika baadhi ya nchi, sheria ya dini bado hutumika kama sheria maalum. Sheria ni chanzo kikuu cha uchunguzi wa kitaalam, wa historia ya sheria, falsafa ya sheria, uchambuzi wa kiuchumi wa sheria au somo la kijamii kuhusu sheria.

Sheria pia huibua masuala muhimu na magumu kuhusu usawa, uadilifu na haki. "Katika usawa wake wa ajabu", alisema mwandishi Anatole France mnamo mwaka 1894, "sheria inakataza matajiri na mafukura kulala chini ya madaraja, kuombaomba barabarani na kuiba mikate."[7] Katika demokrasia ya kawaida, taasisi za msingi za kutafsiri na kuunda sheria ni matawi matatu makuu ya utawala, ambayo ni mahakama isiyo na upendeleo, bunge na serikali yenye kuwajibika.

Ili kutekeleza na kutumia nguvu za kufanya sheria ifuatwe na kutoa huduma kwa umma, urasimu wa serikali, jeshi na polisi ni muhimu. Vyombo hivyo vyote vya dola viliundwa na kutawaliwa na sheria, taaluma ya kisheria iliyo huru na jamii yenye bidii zinajulisha na kusaidia maendeleo.

Masomo ya sheria hariri

Mifumo yote ya kisheria inahusu na masuala ya msingi, lakini kila taifa inaainisha na kubainisha masomo yake ya kisheria kwa njia mbalimbali. Tofauti ya kawaida ni kuwa "sheria ya umma" (maneno yanayohusika kwa karibu na taifa, na kuhusisha sheria ya kikatiba, kitawala na ya jinai), na "sheria ya kibinafsi" (inayohusisha mkataba, sheria ya kukiuka wajibu na mali).[8] Katikamifumo ya sheria ya kirai , mkataba na kukiuka wajibu zinapatikana chini ya sheria ya majukumu huku sheria ya hifadhi inapatikana chini ya serkali za halali au mikataba ya kimataifa. Sheria ya Kimataifa, kikatiba, kitawala, jinai, mkataba, kukiuka wajibu na mali na hifadhi zinatambulika kama "masomo msingi ya jadi",[9] ingawa kuna masomo zaidi ambayo yanaweza kuwa na umuhimu mkubwa zaidi wa kiutendaji.

Sheria ya Kimataifa hariri

 
Ikitoa katiba ya sheria ya kimataifa ya umaa, mfumo wa Umoja wa Mataifa ulikubaliwa wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Sheria ya kimataifa inaweza kuashiria mambo matatu: sheria ya umma ya kimataifa, sheria ya kibinafsi ya kimataifa au mgongano wa sheria na sheria ya mashirika makubwa ya kimataifa.

  • Mgongano wa sheria (au "sheria ya kibinafsi ya kimataifa" katika nchi za sheria ya kiraia) unahusisha maeneo ya kimamlaka ya kisheria ya mgogoro wa kisheria baina ya watu wa kibinafsi unafaa kusikizwa na sheria za maeneo gani ya kimamlaka ya kisheria ndiyo inayofaa kutumika. Leo, biashra zinazidi kuwa na uwezo wa kusongeza minyororo ya ugavi ya mtaji na ajira kuvuka mipaka, na pia kufanya biashara na kampuni za nchi za ng'ambo, hivyo kulifanya swali kuhusu nchi ipi ndiyo inayomamlaka ya kisheria kuwa muhimu zaidi. Idadi kubwa zaidi ya biashara zinachagua usuluhishi wa kibiashara chini ya Mkataba wa New York wa mnamo mwaka1958.[13]
  • Sheria ya Umoja wa Ulaya ndiyo ya kwanza, kufikia sasa, ambayo ni mfano wa sheria kuu ya kimataifa. Kutokana na mwenendo wa kuongezeka kwa ushirikiano wa kiuchumi Duniani, mikataba mingi ya kikanda — hasa ya Umoja wa Nchi za Amerika Kusini — zimeanza kuufuata mfano kama huu. Katika Umoja wa Ulaya, nchi huru zimekusanya mamlaka yao katika mfumo wa mahakama na taasisi za kisiasa. Taasisi hizi zinapewa uwezo wa kutekeleza kanuni za kisheria dhidi ya au kwa nchi wanachama na raia katika namna ambayo haiwezekani kupitia sheria ya umma ya kimataifa.[14] Kama Mahakama ya Ulaya ya Haki yalivyosema katika miaka ya 1960, sheria ya Umoja wa Umoja wa Ulaya hujumiusha "muundo mpya wa sheria ya kimataifa" kwa ajili ya faida inayotegemeana ya kijamii na kiuchumi wa nchi zote wanachama.[15]

Sheria ya kikatiba na ya kiutawala hariri

 
Azimio la Haki za Kibinadamu na za Raia, ambalo kanuni zake bado zini thamani ya kikatiba

Sheria ya kikatiba na kiutawala zinasimamia mambo ya nchi. Sheria ya kikatiba inahusisha uhusiano baina ya serikali, bunge na mahakama na haki za kibinadamu au uhuru wa kiraia wa watu binafsi dhidi ya nchi. Maeneo mengi ya kisheria, kama vile Marekani na Ufaransa, zina katiba moja iliyoandikwa kwa makini, iliyo na Muswada wa Haki. Katiba chache kama vile Uingereza, hazina hati kama hiyo."Katiba" kwa ufupi ni zile sheria ambazo zinajumuisha mwili wa kisiasa, kutoka kanuni, sheria za uamuzi na mkataba. Kesi kwa jina Entick dhidi ya Carrington[16] ilionyesha wazi kanuni ya kikatiba inayotokana na sheria ya kawaifa. Nyumba ya Bwana Entick ilifanyiwa upekekuzi na Afisa mmoja wa polisi aliyeitwa Carrington. Wakati Bwana Entick alipolalamika mbele ya mahakama, Afisa Carrington alidokeza kwamba kibali kutoka waziri wa Serikali, Ali wa Halifax, kilikuwa na mamlaka halali. Hata hivyo, hakukuwa na sheria iliyoandikwa au mamlaka ya kimahakama ambayo yalitoa uwezo huo.Hakimu mkuu, Bwana Camden, alisema,

Mwisho mkubwa, ambao ulifanya watu kuingia katika jamii, ilikuwa kupata mali. Haki hiyo imetunzwa na ni takatifu na haiwezi kuondolewa wakati wowote, ambapo haijaondolewa au kufupishwa na sheria fulani ya umma kwa manufaa ya wote...Hakuna sababau inayoweza kupatikana au kutolewa, kimya cha vitabu ni mamlaka dhidi ya mshtakiwa, na aliyeathiriwa lazima atendewe haki.[17]

Kanuni ya kimsingi ya kikatiba, ilitokana na John Locke, inadokeza ya kwamba mtu binafsi anaweza kufanya isipokuwa kile ambacho kimekataliwa kisheria.[18][19] Sheria ya utawala ndiyo mbinu msingi ya kufanya mashirika ya umma yawajibike. Watu wanaweza kutumia mapitio ya kimahakama kwa matendo au uamuzi uliofanywa na za halmashauri za mitaa, huduma za umma au wizara za serikali, kuhakikisha kuwa zinazingatia sheria. Mahakama ya kwanza ya maalum ya kiutawala yalikuwa mahakama ya Conseil d'État yaliyoundwa mnamo mwaka wa 1799, wakati Napoleon Bonaparte alipochukua mamlaka nchini Ufaransa.[20]

Sheria ya jinai hariri

Makala kuu: Sheria ya jinai

Sheria ya jinai, inayojulikana pia kama sheria ya kuadhibu, inahusisha makosa na adhabu.[21] Kwa hivyo inapima ufafanuzi wa adhabu ya makosa yaliyopatikana kuwa na madhara yanaonekana kuwa na uwezo wa kusababisha uharibifu lakini, kwa undani, haifanyi uamuzi wa kimaadili kumhusu mkosaji wala kuwekea jamii vikwazo ambavyo vinakataza watu kimwili wasifanye makoa mwanzoni.[22] Investigating, apprehending, charging, and trying suspected offenders is regulated by the law of criminal procedure.[23] Kesi ya kidhana ya uhalifu inatokana na ushahidi, kuzidi shaka ya kuridhisha, kuwa mtu ana hatia ya mambo mawili. Kwanza, mshtakiwa lazima awe amefanya kitendo ambacho kinatazamwa na jamii kuwa hatia, au actus reus (kitendo cha hatia).[24] Pili, lazima mshtakiwa awe na dhamira ya kufanya uharibifu ya kufanya kitendoo fulani cha jinai, au mens rea (akili ya hatia). Hata hivyo, kwa kile kinachojulikana kama hatia za "dhima kali", actus reus haitoshi.[25] Mifumo ya jinai ya utamaduni wa sheria ya raia zinatofautisha kati ya nia katika dhana pana (dolus directus na dolus eventualis), na uzembe. Uzembe hauna jukumu la jinai isipokuwa ambapo hatia fulani una adhabu yake maalum.[26][27]

 
Picha inayoonyesha kesi ya uhalifu, kwa sababu ya uchawi katika eneo la Salem

Mifano ya uhalifu ni mauaji, kushambulia, udanganyifu na wizi. Katika mifano maalum utetezi unaweza kutumika kwa vitendo maalum, kama zile kuuwa ili utetezi wa kibinafasi, au katika nyakati maalum kujitetea kuwa wazimu. Mfano mwingine ni katika kesi ya karne ya 19 ya Jamhuri dhidi ya Dudley na Stephens, iliyopima utetezi wa "kimahitaji". Meli ya Mignonette, iliyokuwa ikisafiri kutoka mji wa Southampton kuelekea mji wa Sydney, ilizama. Wafanyikazi watatu wa meli hiyo na Richard Parker, kijana aliyekuwa na umri wa miaka 17, walibaki katika meli iliyoundwa na vijiti. Walikuwa na njaa na kijana yule alikuwa karibu kufa. Kwa sababu ya kuwa na njaa iliyokithiri, wafanyikazi hao walimuuwa kijana yule na kumla. Wafanyikazi hao waliokolewa, lakini wakafikishwa mahakamani huku wakiwa na hatia ya mauaji. Walijitetea kwa kusema kwamba ilihitajika kwa lazima kwa wao kumuuwa kijana yule ili kuyaokoa maisha yao. Bwana Coleridge, akieleza kukataa kukubwa, aliamua, "kuhifadhi maisha ya kibinafsi ni, kwa kuzungumza kijumla, wajibu, lakini inaweza kuwa jukumu kuu kuyatoa maisha hayo kama kafara." Wanaume hao walihukumiwa nyonga, lakini maoni ya umma uliunga mkono haki ya wafanyikazi wale wa meli kuyaokoa maisha yao. Mwishowe, Ufalme ulipunguza hukumu zao hadi miezi sita gerezani.[28]

Makosa ya jinai yanatambulika si tu kama makosa dhidi ya waathirika binafsi, lakini jamii pia.[22] Taifa, kawaida likisaidiwa na polisi, huongoza mashitaka, basi hiyo ndiyo sababu mbona katika nchi zenye sheria ya kawaida kesi hutajwa kama "Watu dhidi ya..." au "Jamhuri (kwa "Rex" au Regina) dhidi ya..." Pia, jopo la waamuzi ambao hutokana na raia wa kawaida hutumika kuamua hatia ya washitakiwa kutokna na pointi zinazoweza kubainika ukweli: jopo la waamuzi haliwezi kubadilisha kanuni za kisheria. Baadhi ya nchi zilizostawi bado hutumia adhabu ya kifo kwa matendo ya jinai lakini adhabu ya kawaida ya uhalifu itakuwa ni kufungwa gereza, faini usimamizi wa taifa (kama vile probesheni), au huduma ya kijamii. Sheria ya kisasa ya jinai imeathiriwa vilivyo na sayansi ya jamii, hasa kuhusu kuhukumu, utafiti wa kisheria, kuunda sheria, na kuwasaidia wahalifu kurekesha mwenedo wao.[29] Katika ngazi ya kimataifa, nchi 108 wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, ambayo ilianzishwa kuwahukumu watu kwa hatia dhidi ya ubinadamu.[30]

Sheria ya mkataba hariri

Makala kuu: Mkataba
 
Tangazo maarufu la kampuni ya Carbolic Smoke Ball lidai kuwa lingeweza kutibu homa. Mahakama yaliamua kuwa tangazo hilo lilikuwa mkataba wa mtu yeyote

Sheria ya mkataba inahusu ahadi zinazowezwa kutendwa, na inaweza kuandikwa kwa ufupi katika maneno ya Kilatinipacta sunt servanda (ahadi lazima zitimizwe).[31] Katika maeneo ya kimamlaka ya sheria ya kawaida, vipengele vitatu muhimu kuhusu utengenezaji wa mkataba vinahitajika: kutoa na kukubali, kutilia maanani na nia ya kutengeneza uhusiano wa kisheria.Katika kesi ya Carlill shisi ya Kampuni ya Carbolic Smoke Ball kampuni ya matibabu ilitangaza kuwa dawa yake mpya ya ajabu, smokeball, ingewatibu watu kutokana na mafua, na ikiwa haingefaulu kuwatibu, wanunuzi wangepata £ 100. Watu wengi waliwasilisha kesi mahakamani ili wapate £100 zao wakati dawa hiyo iliposhindwa kuwatibu. Ikiogopa kufilisika, Kampuni ya Carbolic ilijitetea kwa kusema kuwa tangazo lile lilikuwa mzaha tu, na kwa hivyo halikuwa toleo lenye nguvu za kisheria. Lilikuwa karibisho, mchezo tu. Lakini mahakama ya rufaa yaliamua kuwa kwa mtu mwenye kufikiria kwa kawaida kampuni ya Carbolic ilikuwa imefanya toleo. Watu walikuwa wametoa kusudi la kununua bidhaa ile kwa kupitia "shida bayana" ya kutumia bidhaa yenye hitilafu. "Soma tangazo vile utakavyo, na ulibadilishe tangazo hilo vile utakavyo", alisema Hakimu Lindley, "haa kuna ahadi maalum ilitajwa katika lugha isyokuwa na utata wowote".[32]

"Kutilia maanani" knaonyesha ukweli kwamba vyama vyote katika mkataba vimebadilisha kitu fulani chenye maana. Baadhi ya mifumo ya sheria ya kawaida, ikiwemo Australi, zinasonga mbali kutoka dhana ya kutilia maanani kama mojawapo ya mahitaji ya mkataba. Dhana ya "estoppel" au culpa in contrahendo, inaweza kutumika kuunda wajibu wakati mazungumzo kabla ya kuingia mkataba[33] Katika maeneo ya kisheria ya kiraia, kutilia maanani si lazima kwa mkataba kuwa na nguvu ya kisheria.[34] Nchini Ufaransa, mkataba wa kawaida unasemekana kutokea ambapo "kukutana kwa akili" au kwa "kuwa na nia zinazowiana". Ujerumani ina mtazamio maalum kuhusu mikataba, ambayo inayusisha sheria ya mali. Kanuni ya dhana ya kiakili (Abstraktionsprinzip wanayoitumia, inamaanisha kuwa wajibu wa kibinafsi wa mkataba unaundwa kando na jina la mwenye mali yanayokabidhiwa. Wakati ambapo mikataba inavunjwa kwa sababu fulani (kwa mfano mnunuzi wa gari amelewa kiasi kwamba hana uwezo wa kisheria wa kufanya mkataba)[35] Wajibu wa kimkataba wa kulipa unaweza kuvunjwa tofauti na jina la mwenye gari. Sheria ya kutajirika kusio kwa haki, badala ya sheria tya mkataba, basi inatumika kurudisha jina kwa mmiliki halali.[36]

Sheria ya ukiukaji wa wajibu hariri

Makala kuu: Ukiukaji wa wajibu

Sheria ya ukiukaji wa wajibu, ambayo wakati mwingine huitwa kosa la jinai, ni makosa ya raia. Kuwa na kosa la ukiukaji wa wajibu, mtu lazima awe amekiuka wajibu aliukwa anafaa kumtendea mty mwingine, au kukiuka haki fulani ya awali ya kisheria. mfano unaweza kuwa kumgonga mtu kimakosa na mpira wa mchezo wa kriketi.[37] Chini ya sheria ya uzembe, ambayo ndiyo aina ya ukiukaji wa wajibu maarufu zaidi, mtu aliyepatwa na madhara anaweza kuomba fidia kwa ya majeraha yake kutoka kwa mtu mwenye uwajibikaji. Kanuni za uzembe zinaonyeshwa na kesi ya Donoghue dhidi ya Stevenson.[38] Rafiki mmoja wa Bi. Donoghue aliagiza chupa isiyopenyeka nuru la pombe ya tangawizi (iliyokusudiwa kutumika na Bi. Donoghue) katika mkahawa katika eneo la Paisley. Baada ya kunya kunya nusu ya bia ile , Bi, Donoghue alimimina iliyosalia katika bilauri. Mabaki yaliyooza ya konokono yalielea juu ya pombe. Alidai kuwa alipigwa na bumbuwazi, na kupata ugonjwa wa kuchomeka ndani ya matumbo, na ilimbidi kumpeleka mtengenezaji pombe kwa kuruhusu kinywaji kuchafuka ovyo. Nyumba ya Mabwana iliamua kwamba mtengezaji pombe aliwajibika kwa ugonjwa wa Bi. Donoghue. Bwana Atkin alikuwa na mtazamo maalum wa kimaadili, na akasema,

Dhima ya upuuzaji ... bila shaka ina msingi wake katika mawazo ya kijumla ya umma kuhusu makosa ya kimaadili amabyo mkosaji lazima alipe ... Kanuni ya kuwa unafaa kumpenda adui yako, kisheria inakuwa, haufai kumjeruhi jirani yako; na swali la wakili, nani ndiye jirani yangu? linapokea jibu lenye vikwazo. Lazima uwe na uwangalifu wa kuepuka na vitendo au visa ambapo hautendi lolote inapofaa, ambavyo unaweza kutazamia kuwa vikamjeruhi jirani yako.[39]

Huu ulikuwa msingi wa kanuni nne za upuuzaji; (1) Bwana Stevenson alimdai Bi. Donoghue wajibu wa kujali wa kuuza vinywaji salama (2) yeye alivunja wajibu wake wa kujali (3) madhara hayangefanyika isipokuwa kwa kuvunja kwake kwa wajibu wa kujali na (4) tendo lake lilikuwa sababau ya karibu, au haikuwa tokeo la mbali, la madhara yaliyompata mtu fulani.[38] Mfano mwingine wa ukikaji wa wajibu unaweza kuwa wa jirani ambaye anapiga kelele nyingi sana na na mashine katika nyumbani kwake.[40] Chini ya dai la kero kelele hiyo inaweza kukomeshwa. Ukiukaji wa wajibu pia inaweza kuhusisha vitendo vya kimakusudi, kama vile ushambulizi, vita au kuvuka na kuingia katka maeneo yaliyopigwa marufuku. Sheria ya ukiukaji wa wajibu inayofahamika vyema ni ile ya kumharibia mtu jina, ambayo inafanyika, kwa mfano, wakati gazeti linapochapisha madai yasiyokuwa na msingi ambayo yanaharibu sifa ya mwanasiasa fulani.[41] Ukiukaji wa wajibu ambao ni mbaya zaidi ni zile wa kiuchumi, ambao huwa msingi wa sheria ya ajira katika baadhi ya nchi kwa kufanya vyama vya kibiashara kuwa na dhima kwa sababu ya migomo,[42] Wakati ambapo amri ya kisheria haipatiani kinga.[43]

Sheria ya mali hariri

Makala kuu: Sheria ya mali
 
Picha ya Bubujiko la Bahari ya Kusini, mojawapo ya majanga ya kiuchumi yalilotokana na uvumi. Janga hilo la kiuchumi lilisababisha kuundwa kwa kanuni kali kuhusu uuzaji wa hisa.[44]

Sheria ya mali inatawala vitu vya thamani ambavyo watu huvitambua kama 'vyao'. Mali ya kweli wakati mwingine huitwa 'mali isiyohamishika' inahusu umiliki wa ardhi na vitu vilivyojikita katika ardhi hiyo.[45] Mali ya kibinafsi, inaashiria mambo mengineyo; vyombo vinavyowezwa kusongeshwa, kama vile tarakilishi, magari, mapambo na mikate au turathi haki, kama vile akiba na hisa. Haki ya in rem ni haki ya kipande maalum cha mali, ikitofautishwa na haki in personam ambayo inaruhusu fidia kwa hasara, lakini si kwa kurudishiwa kitu fulani. Sheria ya ardhi inajumuisha msingi wa aina nyingi za sheria za mali, na ndiyo ngumu zaidi. Inahusisha mogeji, mikataba ya kukodisha, leseni, maagano, ruhusa na mifumo ya kisheria kwa usajili wa ardhi. Kanuni kuhusu matumizi ya ardhi ya kibinafsi chini ya haki miliki, sheria ya kampuni, hifadhi na sheria ya biashara. Mfano wa kesi msingi ya ya sheria nyingii za mali ni Armory v Delamirie.[46] Kijana wa kufagia chimni alipata pambo lenye mawe ya thamani. Alichukua pambo lile kwa muundaji wa vifaa vya dhahabu ili thamani yake ikadiriwe. Mwanafunzi wa muundaji wa vifaa vya dhahabu aliangalia pambo lile, akaiba mawe yale ya thamani, ma kumuambia kijana yule kuwa thamani yake ilkuwa nusu peni tatu na kuwa angeinunua. Kijana yule alimwambia kuwa angepenga arudishiwe pambo lile, kwa hivyo mwanafunzi wa muundaji vifaa alimrudishia pambo, lakini bila mawe yale ya thamani. Kijana yule alimpeleka mtengenezaji wa vifaa vya dhahabu kotini kwa jaribio la mwanafunzi wake kumdanganya. Bwana Hakimu Mkuu Pratt aliamua kuwa ingawa kijana hangesemekana kuwa mumiliki wa pambo lile, angefaa kutazamwa kama mpataji aliyefaa ("mpataji muwekaji") hadi mumiliki wa kiasili anapopatikana. Kwa kweli mwanafunzi na kijana yule wote walikuwa na haki ya umiliki wa pambo lile (dhana ya kiufundi, inayomaanisha kuwa kitu fulani kingeweza kumilikiwa na mtu fulani), lakini nia ya kijana yule ya kumiliki ilitazamiwa kuwa bora zaidi, kwa sababu ingeweza kudhihirishwa kuwa ya kwanza katika wakati. Umiliki unaweza kuwa sehemu tisa kwa kumi ya sheria, lakini si yote.

Kesi hii hutumika kudhihirisha mtazamo wa mali katika maeneo ya kisheria ya kawaida, kuwa mtu anayeweza kuonyesha dai bora zaidi la kipande cha mali, dhidi ya chama kingine, ndiye mumiliki.[47] Kwa kulinganisha, mbinu ya kiklasiki ya sheria ya raia kuhusu mali, iliendelezwa na Friedrich Carl von Savigny, ni kuwa ni haki nzuri dhidi ya Ulimwengu. Wajibu, kama mkataba na ukiukaji wa wajibu hutazamwa kama haki nzuri dhidi ya watu binafsi.[48] Dhana ya mali inaibua maswala mengi zaidi ya kifalsafa na kisiasa. Locke alidokeza kwamba "maisha, uhuru na nyumba" zetu ni mali yetu kwa sababu tunamiliki mali yetu na tunachangayana ajira yetu na mazingira yetu.[49]

Usawa na amana hariri

 
Mahakama ya Chancery, London, mwanzoni mwa karne ya 19

Usawa na amana ni mwili wa sheria ulioibuka nchini Uingereza kando na "shera ya kawaida". Sheria ya kawaida ilisimamiwa na mahakimu. Bwana Chansela kwa upnade mwingine, kama muwekaji dhamiri wa mfalme, angeweza kupuuza sheria iliyotengenezwa na hakimu ikiwa alifikiria kuwa ilikuwa sawa kufanya hivyo.[50] Hili lilimaanisha kuwa usawa ulianza kufanya kazi zaidi kupitia kanuni bali si sheria ambazo hazikubadilika. Kwa mfano, ambapo mifumo ya sheria ya kawaida au sheria ya raia haiwaruhusu watu kugawa umiliki wa kutoka kwa udhibiti wa kipande kimoja cha mali, usawa unaruhusu hili kupitia mpango unaoitwa 'amana'. Kudhibitiwa kwa mali na 'wenye amana' ambapo kwa upande mwingine umiliki 'wenye manufaa' (au 'yenye usawa') wa mali ya amana inashikiliwa na watu wanojulikana kama 'wadhamini'. Wadhamini wana wajibu kwa walengwa wao wa kuyachuna vyema mali waliyokabidhiwa.[51] Katika kesi ya awali ya Keech dhidi ya Sandford[52] mtoto alirithi haki ya kokodisha katika soko katika eneo la Ramford, mjini London. Bw, Sandford alikabidhiwa mali hayo hadi wakati ambapo mtoto angekomaa. Lakini kabla ya hapo, kipindi cha kukodisha kilikwisha. Kabaila alikuwa (inaonekana) amemwambia Bw. Sandford kuwa hakutaka mtoto yule awe na kukodisha kupya. Lakini bado kabaila alikuwa amefurahi (inaonekana) kumpa Bw. Sandford fursa ya kukodisha. Bw Sandford aliichukua. Wakati ambapo mtoto (sasa Bw. Keech) alikuwa mkubwa, alimpeleka Bw. Sandford mahakamani kwa faida aliyokuwa akipata kwa kupata kukodisha kwa soko. Bw. Sandford alifaa kuaminika, lakini alijiweka katika nafasi ya mgongano wa maslahi. Bwana Kansela, Bwana Mfalme, alikubali na kumuamuru Bw. Sandford kutoa faida ile na kumlipa Bw. Keech. Aliandika,

Ninaona vizuri sana kuwa, ikiwa mdhamini, akikataa kufanya kukodesha upya, anaweza kuwa na kukodesha kwake mwenyewe mali chache ya kiamana yangesajiliwa upya ... Hili linaweza kuonekana kuwa gumu sana, kuwa mdhamini ndiye mtu wa kipekee kwa binadamu wote ambaye hatakuwa na kukodisha; lakini ni bora kanuni ifuatiliwe na isipuuzwe wakati wowote.

Bila shaka, Bwana Mfalme LC alikuwa na wasiwasi kwamba wadhamini huenda wakatumia fursa ya kutumia mali ya amana wenyewe badala ya kuyachunga. Wadadisi wa kibiashara wanaotumia hifadhi walikuwa wamesababisha kuaguka kwa soko la hisa katika siku hizo. Wajibu mkali kwa wadhamini ulijumuishwa katika sheria ya serikali na kutumika kwa wakurugenzi wa makampuni na maafisa watendaji wakuu. Mfano mwingine wa jukumu la mdhamini unaweza kuwa kuwekeza mali vizuri au kuiuza.[53] Hii hasa ndiyo kesi kwa fedha za pensheni , aina muhimu kwa zote ya amana, ambapo wawekezaji ndio wadhamini wa akiba za watu hadi wastaafu. Lakini amana pia zinaweza kuundwa kwa madhumuni ya hisani, mifano maarufu ikiwa Makavazi ya Uingereza au Shirika la Rockefeller.

Utaalamu zaidi hariri

Sheria huenea mbali kuliko masomo ya msingi hadi karibu kila eneo la maisha. Ngazi tatu zimetajwa hapa ili kurahisiha majadiliano, ingawa masomo mbalimbali hufanana na kutegemeana.

Sheria na jamii
 
Chama cha wafanyikazi kilichoundwa na kikundi cha UNISON walipogoma
Sheria na biashara
Sheria na vikwazo
 
Sakafu ya biashara ya Soko la Hisa la New York baada ya kuanguka kwa Wall Street mnamo mwaka wa 1929, kabla ya sheria kali zaidi za vikwazo vya kibenki vilipoanza kutumika

Mifumo ya sheria hariri

Kwa ujumla, mifumo ya kisheria inaweza kugawanywa kati ya mifumo ya kisheria ya kiraia na mifumo ya kisheria ya kawaida.[57] Maneno "sheria ya kiraia" yanayoashiria mfumo wa kisheria hayapaswi kuchanganyishwa na "sheria ya kiraia" kama kundi la masomo ya kisheria ambayo ni tofauti na sheria ya umma au ya jinai. Aina ya tatu ya mfumo wa kisheria—inayokubalika bado na baadhi ya nchi ambazo zina utengano wa kanisa na taifa—ni sheria sheria ya kidini, ambayo ina msingi wake katika maandiko ya kidini. Aina ya mfumo amabo nchi inatumia kutawala mara nyingi kudhamiriwa na historia yake, uhusiano wake na nchi zingine au kushikilia kwake kwa viwango vya kimataifa. Vyanzo ambavyo maneneo fulani ya kisheria hutumia kama kama zenye uwezo wa kuwa nguvu za kisheria ndizo sifa fafanuzi za mfumo wowote wa kisheria. Hata hivyo, uainishaji ni jambo la umbo kuliko maana, kwani sheria sawa mara nyingi hutawala.

Sheria ya kiraia hariri

Makala kuu: Sheria ya kiraia
 
Ukurasa wa kwanza wa toleo la mwaka wa 1804 la Sheria za Kinapoleoni

Sheria ya kiraia ni mfumo wa kisheria unaotumika katika nchi nyingi Duniani. Katika sheria ya kiraia vyanzo vinavyotambulika kama kuwa na mamlaka, ni, haswa, uundaji wa sheria—haswa sheria zilizoandikwa katika katiba au amri zinazopitishwa na serikali—na tamaduni.[58] Sheria za kuandikwa zinapatikana hata katika miaka mingi ya awali , huku mfano mmoja ukiwa Codex Hammurabi ya Kibabeli. Mifumo ya sheria za kiraia ya kisasa inatokana na mazoezi ya kisheria ya Dola la Kirumi ambalo maadiko yake yalipatikana katika Ulaya ya Zama za Kati. Sheria ya Kirumu katika siku za Jamhuri ya Kiruma na Dola la Kirumi lilitegemea sana utaratibu, na ilikosa daraja la kitaaluma.[59] Badala uake mtu wa kawaida aliyeitwa, iudex, alichagukiwa kufanya uamuzi. Kesi za awali hazikuripotiwa, kwa hivyo sheria yoyote yenye msingi katika kesi iliyoibuka ilifichwa na hata kutotambulika.[60] Kila kesi ilikuwa ilimuliwe upya kutokana na sheria za nchi, ambayo ni sawa na kupungua kwa umuhimu (kinadharia) wa uamuzi wa mahakimu kwa kesi za siku za usoni kwa mufumo ya kisheria siku za leo. Katika kipindi cha karne ya 6 NK katika Dola la Mashariki la Roma, Kaisari Justinian I aliandika na kuzikusanya pamoja sheria ambazo zilikuwa zinapatikana hapo awali katika Roma, ambapo kile kilichobakia kilikuwa sehemu moja juu ya ishirini ya kiwango cha maandiko ya kisheria kutoka awali.[61] Hili ikawa inafahamika kama Corpus Juris Civilis. Kwa mujibu wa mwanahistoria mmoja wa kisheria, "Justinian alitazama kwa uangalifu hadi miaka ya dhahabu ya nyuma ya sheria ya Kirumi na alilenga kuirejesha hadi upeo wake wa karne tatu za awali."[62] Wakati uo huo, Ulaya ya Magharibi ilitumbukia polepole katika Zama za Giza, na haikuwa hadi karne ya 11ambapo wasomi katika Chuo Kikuu cha Bologna walipoyagundua upya maandiko yaliyokuwa yamepotea na kuyatumia kuzitafsiri sheria zao.[63] Maandiko ya sheria za kiraia yenye msingi unaofanana kwa karibu na sheria ya Kirumu, sambamba na ushawishi mchache kutoka sheria za kidini kama vile sheria ya Kikanoni na sheria ya Kiislamu,[64][65] iliendelea kuenea kote baranii Ulaya hadi Kutaalmika; kisha, katika karne ya 19, Ufaransa, na Sheria iliyoandikwa ya Kiraia, na Ujerumani, Bürgerliches Gesetzbuch, zilifanya sheria zao zilizokuwa zimeandikwa kuwa za kisasa. Sheria hizi mbili zilizoandikwa zilisukuma vilivyo si tu mifumo ya kisheria ya nchi katika Bara Ulaya (kama vile Ugiriki), lakini pia tamaduni za kisheria za Ujapani na Kikorea.[66][67] Leo, cnhi ambazo zina mifumo ya kisheria ya kiraia ni kama vile Urusi na Uchina na maeneo mengi ya Marekani ya Kati na Marekani ya Kilatini.[68] Marekani inafuata sheria ya kawaida inayofafanuliwa hapa chini.

Sheria ya kawaida na usawa hariri

Makala kuu: Sheria ya kawaida
 
Mfalme Yohana wa Uingereza anatia sahini Magna Carta

Sheria ya kawaida na usawa ni mifumo ya kisheria ambapo uamuzi wa mahakama yanakubalika wazi kuwa vyanzo vya sheria."Mafundisho ya utangulizi", au stare decisis (Kilatini kwa "kusimama kwa uamuzi") unamaanisha kuwa sumauzi unaofanywa na mahakama yenye mamlaka kubwa yanafunga mahakama yenye mamlaka ya chini. Mifumo ya kisheria ya kawaida hutumia amri mara chache sana, zinazopitishwa na bunge, lakini huenda zikafanya jaribio ambalo si la kitaratibu kuandika sheria zao kuliko katika "mfumo wa sheria wa kiraia". Sheria ya kawaida ina asili yake nchini Uingereza na imerithiwa na karibu nchi zote ambazo hapo awali zilihusika na Dola la Uingereza (isipokuwa Malta, Scotland, na jimbo la Marekani la Louisiana, na jimbo la Kanada la Quebec). Katika Uingereza wakati wa zama za kati, ushindi wa Norman ulisababisha kuungana kwa desturi mbalimbali za kikabila na hivyo basi kuunda sheria ya "kawaida" ya nchi yote. Labda ikisukumwa na mazoea ya kisheria ya Kiislamu wakati wa Krusedi,[65] sheria ya kawaida iliendelea ambapo Mfalme wa Kiingereza alikuwa amefanywa kuwa dhaifu na gharama kubwa ya vita vywa kudhibiti sehemu kubwa za Ufaransa. Mfalme Yohana alikuwa amelazimishwa na mabaroni wake kutia saini hati iliyoweka vikwazo kwa mamlaka yake ya kupisha sheria. "Mkataba huu mkuu" au Magna Carta wa mwaka 1215 pia ulihitaji jopo la mahakimu wa Mfalme kufanya mikutano yao ya kimahakama na uamuzi wao katika "mahali maalum" badala ya kutoa haki ya kibepari katika maeneo yaliyokuwa magumu kutabiri kote.[69] Kundi la mahakimu walsomi na waliokolea walipata jukumu muhimu katika kuunda sheria chini ya mfumo huu, na ikilinganishwa na wenzao Barani Ulaya mahakama ya Uingereza ilikuwa na urasimu mwingi zaidi. Kwa mfano, mnamo mwaka wa 1297, wakati ambapo mahakama kuu ya Ufaransa yalikuwa na mahakimu hamsini na wawili, Mahakama ya Uingereza ya Maombi ya Kawaida yalikuwa na watano.[70] Mahakama haya yenye nguvu na yaliyoshikamana yalisababisha mfumo wa kikiritimba.[71] Kufuatana na hilo, kadiri wakati ulivyopita, idadi iliyoongezeka ya raia waliomba Mfalme kupuuza sheria ya kawaida, na kwa niaba ya Mfalme Bwana Chansela alitoa uamuzi kufanya kile ambacho ni sawa kwa kila kesi. Kuanzia wakati wa Thomas More, wakili wa kwanza kuteuliwa kama Bwana Chansela, mwili wa kimfumo wa usawa uliongezeka kando ya sheria ya kawaida yenye ukiritimba, na ilianzisha Mahakama yake ya Chancery. Mwanzoni, usawa ulikosolewa kuwa ulikosa kukosa utaratibu, na kuwa ulibadilika kulingana na urefu wa mguu wa Chansela.[72] Lakini baada ya muda iliunda kanuni, hasa chini ya Bwana Eldon.[73] Katika karne ya 19 mifumo hiyo miwili iliunganishwa pamoja. Katika kuendeleza sheria ya kawaida na usawa, waandishi wa kitaaluma wamekuwa na jukumu muhimu. William Blackstone, kuanzia kipindi cha 1760, alikuwa mwanachuoni wa kwanza kuelezea na kufunza usawa.[74] Lakini kwa kuelezea tu, wasomi walitafuta melezo na miunso msingi walibadilisha polepole jinisi sheria ilivyofanya kazi.[75]

Sheria ya kidini hariri

Makala kuu: Sheria ya kidini

Sheria ya kidini inatokana na maagizo ya dini. Baadhi ya mifano ni Halakha ya Kiyahudi na Sharia ya Uislamu — ambazo zote mbili zinamaanisha "njia ya kufuata" — huku sheria za Kanisa za Ukristo nazo hutumika katika madhehebu machache, kama vile Kanisa Katoliki, Kanisa la Kiorthodoksi na la Anglikana.

Mara nyingi dini inadai kutobadilika kwa sheria, kwa sababu neno la Mungu haliwezi kufanyiwa marekebisho wala kupingwa na mahakimu au serikali.

Hata hivyo mfumo fasaha wa sheria kwa jumla unahitaji upanuzi upande wa binadamu. Kwa mfano, Torati au Vitabu Vitano vya Musa katika Agano la Kale. Vitabu hivyo vina kanuni na sheria za msingi za Uyahudi, ambayo baadhi ya jamii ya Kiisraeli huchagua kutumia. Halakha ni kanuni ya sheria za Kiyahudi inayofanya muhtasari wa baadhi ya ufafanuzi wa kitabu cha Talmud. Hata hivyo, Sheria za Israeli zinaruhusu mlalamikaji kuchagua mbinu za kidini ikiwa tu anataka. Mfano mwingine ni Korani ambayo ina sheria, na inakuwa kama chanzo cha sheria zaidi kupitia ufafanuzi,[76] Qiyas (kulinganisha), Ijma (kufikia muafaka) na yaliyokwishatokea. Hili hasa hupatikana katika mkusanyo wa sheria na falsafa ya kisheria inayojulikana kama Sharia na Fiqh.

 
Kesi katika Dola la Ottoman, mwaka 1879, wakati sheria ya kidini ilitumika chini ya Mecelle.

Hadi karne ya 18, Sharia ilitekelezwa kote katika Ulimwengu wa Kiislamu katika mfumo ambao haukuwa umeandikwa kwa ufasaha, huku sheria ya Mecelle ya Dola la Ottoman katika karne ya 19 ilikuwa ya kwanza kuandika vipengele vya Sharia. Tangu miaka ya kati ya 1940, majaribio yamefanywa, katika nchi nyingi, kufanya sheria hizo zifanane zaidi na hali na dhana za kisasa.[77][78]

Katika nyakati za sasa, mifumo ya kisheria katika mataifa mengi ya Kiislamu hutegemea sheria za kiraia na sheria ya kawaida na pia sheria na tamaduni za Kiislamu. Katiba za baadhi ya nchi za Kiislamu, kama vile Misri na Afghanistan, zinatambua Uislamu kama sheria ya taifa, hivyo kuyafanya mabunge katika nchi hizo yasiwe na budi kufuata Sharia.[79] Saudia inatambua Korani kama katiba, na inatawaliwa kwa msingi wa sheria ya Kiislamu.[80] Iran pia imeshuhudia kurudi kwa sheria ya Kiislamu katika mfumo wake wa kisheria baada ya mwaka 1979.[81] Katika miongo michache iliyopita, mojawapo ya tofauti kuu ya harakati ya mwamko wa Kiislamu imekuwa wito wa kuirejesha Sharia, wito ambao umeibua kiasi kikubwa cha maandishi na kuathiri siasa duniani.[82]

Nadharia ya sheria hariri

Historia ya Sheria hariri

Makala kuu: Historia ya sheria
 
Mfalme Hammurabi anaonyeshwa mkusanyiko wa sheria na mungu wa jua wa Kimesopotamia Shamash, ambaye pia anatambulika kama mungu wa haki

Historia ya sheria inashikamana kwa karibu na maendeleo ya ustaarabu. Sheria ya Misri ya Kale, iliyorudi nyuma mbali hadi mnamo 3000 KK, ilikuwa na mkusanyiko wa sheria ambao huenda ulikuwa umegawanjwa katika vitabu kumi na viwili. Ilizingatia dhana ya Ma'at, iliyokuwa na sifa ya mapokeo, hotuba za kushawishi, usawa wa kijamii na uaminifu.[83][84]

Kufikia karne ya 22 KK, mtawala wa zamani wa Kisumeri, Ur-Nammu alikuwa ameandaa mkusanyiko wa sheria, ambao ulihusisha kauli za kimjadala ("ikiwa ... basi ...").

Kufikia mwaka wa 1760 KK, Mfalme Hammurabi aliboresha zaidi Sheria ya Babeli, kwa kuikusanya na kujandika katika jiwe kubwa. Hammurabi aliweka nakala kadhaa za jiwe lile kote katika milki ya Babeli kama stelae, ili watu wote waitazame; hii ilikuja kufahamika kama Mkusanyiko wa Sheria za Hammurabi. Nakala iliyobaki ambayo haijaharibika sana wa stelae hizi iligunduliwa katika karne ya 19 na Waingereza wasomi wa mambo ya milki ya Assyria, na tangu wakati huo imenakiliwa upya na kutafsiriwa katika lugha mbalimbali, zikiwemo Kiingereza, Kijerumani na Kifaransa.[85]

Agano la Kale lilianza mnamo 1280 KK, na linachukua umbo la amri za kimaadili kama mapendekezo ya jamii nzuri.

Mji-dola wa Ugiriki ya Kale, Atheni ya Kale kuanzia karne ya 8 KK ilikuwa jamii ya kwanza kuwa na msingi wake katika kuhusisha raia kwa upana; isipokuwa wanawake na daraja la watumwa. Hata hivyo, Atheni haikuwa na sayansi ya kisheria, na hapakuwa na neno la "sheria" isipokuwa kama dhana ya kiakili tu.[86] Bado sheria ya Ugiriki wa Kale ilikuwa na uvumbuzi mkubwa wa kikatiba katika kuendeleza demokrasia.[87]

Sheria ya Kirumi ilisukumwa sana na falsafa ya Kigiriki, lakini maelezo yake ya kina yaliendelezwa na wanasheria wa kitaaluma, na yalikuwa magumu sana.[88][89] Katika kipindi cha karne zilizopita kati ya kupanda na kushuka kwa Dola la Roma, sheria imebadilishwa ili kukabiliana na hali za kijamii zilizokuwa zikibadilika, na ilikusanywa na kuandkiwa vilivyo wakati wa utawala wa kaisari Justinian I.[90] Ingawa ilipungua kwa umuhimu mwanzoni mwa Karne za Kati, Sheria ya Kirumi iligunduliwa upya wakati wa karne ya 11 ambapo wasomi walianza kutafiti mkusanyiko wa sheria za Kirumi na kuyatumia mawazo yao.

Katika Uingereza ya Zama za Kati, mahakimu wa Mfalme waliunda mwili wa utangulizi, ambao baadaye ulijulikana kama sheria ya kawaida. Sheria ya biashara ya Ulaya mzima iliundwa ili kuwapa wafanyabiashara uwezo wa kufanya biashara kwa kutumia viwango sawa vya mazoezi; badala ya kutumia sheria za kimtaa zenye pande nyingi. Hiyo Lex Mercatoria, mtangulizi wa sheria ya kisasa ya biashara, ilihimiza uhuru wa mkataba na kuwekwa mbali kwa mali.[91]

Kadiri utaifa ulipozidi katika karne za 18 na 19, ndipo Lex Mercatoria ilipozidi kujumuishwa katika sheria za kimanispaa za nchi mbalimbali chini ya mkusanyiko mpya wa sheria za kiraia. Mkusanyiko wa Sheria za Napoleoni na sheria za Kijerumani ulikuwa na ushawishi mkubwa zaidi. Ikitofautishwa na sheria ya kawaida ya Uingereza, ambayo ina idadi kubwa ya sheria za kesi, mikusanyiko ya sheria katika vitabu vidogo ni rahisi kuuza nje ili mahakimu waweze kuitumia. Hata hivyo, hivi leo kuna ishara kuwa sheria ya kiraia na sheria ya kawaida zinazidi kukaribiana.[92] Sheria ya Umoja wa Ulaya imekusanywa katika mikataba, lakini huendelezwa kupitia utangulizi unaofanywa na Mahakama ya Ulaya ya Haki.

 
Katiba ya nchi ya Uhindi ndiyo katiba ndefu zaidi iliyoandikwa kwa nchi, ikiwa na Ibara 444, Ibara 12 ndogo, na marekebisho mengi na maneno 117,369

Sheria ya Kiislamu na falsafa ya sheria zilianza katika kipindi cha Zama za Kati.[93] Mbinu ya kisheria ya utangulizi na kufikiria kupitia mlinganisho (Qiyas) iliyotumika katika sheria ya mapema ya Kiislamu ilifanana na na ile ya baadaye ya mfumo wa Sheria ya Kawaida ya Uingereza.[94] Hii ilitumika hasa katika shule ya Maliki ya sheria ya Kiislamu iliyopatikana sana katika eneo la Afrika Kasakazini, Uhispania wa Kiislamu na baadaye Sicily ya Kiemereti. Kati ya karne za 8 na 11, sheria ya Maliki iliendeleza taasisi nyingi zilizokuwa sambamba na taasisi za baadaye za sheria ya kawaida.[95]

Sheria ya kale ya Uhindi na Uchina zinawakilisha mapokeo tofauti ya sheria, na kihistoria yamekuwa na shule huru za kinadharia na mazoezi.

Arthashastra, ambayo pengine iliandikwa mnamo 100 BK (ingawa ina maandiko ya awali kidogo), na Manusmriti (100–300) yalikuwa mikataba ya uanzilishaji nchini Uhindi, na ilikuwa na maandiko yanayofikiriwa kuwa wongofu wenye mamlaka wa kisheria.[96] Falsafa kuu ya Manu ilikuwa kuvumiliana na Mfumo wa Vyama Vingi, na ilitajwa kote katika eneo la Asia ya Kusini Mashariki.[97]

Mapokeo haya ya Kihindu, pamoja na sheria ya Kiislamu, yalibadilishwa na na sheria ya kawaida wakati ambapo Uhindi ilifanywa kuwa sehemu ya Dola la Uingereza.[98] Malaysia, Brunei, Singapore na Hong Kong pia ilianza kutumia sheria ya kawaida, Mapokeo ya sheria ya Asia ya Kusini yanaangazia mkusanyiko maalum wa ushawishi wa kidunia na kidIni.[99]

Ujapani ilikuwa nchi ya kwanza kuufanya mfumo wake wa sheria uwe wa kisasa sambamba na ule wa nchi za magharibi, kwa kuagiza sehemu za mkusanyiko wa sheria za Ufaransa, lakini hasa mkusanyiko wa sheria za Kijerumani.[100] Hili lilionyesha kwa kiwango fulani hadhi ya Ujerumani kama nguvu yenye uwezo mkubwa zaidi katika kipindi cha mwisho cha karne ya 19.

Pia, sheria ya mapokeo ya Uchina ilifungua njia kwa kubadilishwa na nchi za magharibi kuelekea miaka ya mwisho ya nasaba ya Ch'ing kupitia njia ya mkusanyiko wa sheria tatu za kibinaFsi zilizokuwa na msingi katika muundo wa Ujapani wa sheria ya Ujerumani.[101] Leo sheria ya Taiwan inabaki na mshikamano wa karibu zaidi na mkusanyiko wa sheria kutoka kipindi hicho, kwa sababu ya mgawanyiko kati ya wanataifa wa Chiang Kai-shek, ambao walitoroka kutoka sehemu hiyo, na wakomunisti wa Mao Zedong waliopata ushindi wa kudhibiti bara mnamo mwaka wa 1949. Muundombinu wa sasa wa Jamhuri ya Watu wa Uchina ilishawishika pakubwa na Sheria ya Kisoshalisti ya Umoja wa Kisovyeti, inayopea sheria ya utawala umuhimu mwingi kuliko haki za sheria ya kibinafsi.[102] Kwa sababu ya kuongezeka kwa kasi kwa viwanda, leo Uchina inapitia machakato wa wa marekebisho, angalau katika nyanja ya haki za kiuchumi, ikiwa si haki za kijamii na kisiasa. Sheria mpya ya mkataba ya mwaka wa 1999 ilikuwa ishara ya kusonga mbali na kuwa na utawala mwingi.[103] Isitoshe, baada ya mazungumzo yaliyodumu miaka kumi na mitano, mnamo mwaka 2001 Uchina ilijiunga na Shirika la Biashara Duniani.[104]

Falsafa ya sheria hariri

Makala kuu: Falsafa ya sheria

Falsafa ya sheria kwa kawaida inaitwa jurisprudensi. Jurisprudensi unaozidi kuongezka wenyewe ni falsafa ya kisiasa, na unauliza "sheria inafaa kuwa nini?", huku jurisprudensia ya uchambuzi inauliza "sheria ni nini?". Jibu la kiutumikaji la John Austin linajibu kuwa sheria ni "amri, zinazoandamana na matishio ya vkwazo, kutoka kwa mtawala, ambaye watu wote wamezoea kumtii".[105] Mawakili wa sheria ya kimaumbile kwa upande mwingine, kama vile Jean-Jacques Rousseau, wanadokeza kwamba sheria inaangazia sheria isiyobadilika ya tabia ya kimaumbile. Dhana ya "sheria ya kimaumbile" iliibuka katika falsafa ya Kigiriki ya zamani kwa wakati mmoja na kwa pamoja na dhana ya haki, na iliingia mkondo wa utamaduni wa Magharibi kupitia maandiko ya Thomas Aquinas na maoni ya mwanafalsafa wa Kiislamu na mwanasheria Averroes.[106][107]

Hugo Grotius, mwanzilishi wa mfumo uliotegemea dhana za kiakili pekee ya sheria ya kimaumbile, alidokeza kuwa sheria inatokana na msukumo wa kijamii—jinsi Aristotle alivyokuwa amesema—na kufikiria.[108] Immanuel Kant aliamini kuwa amri ya kimaadili inahitaji sheria "zichaguliwe kana kwamba zinafaa kushikilia kama sheria za ilimwenguni kote za kimaumbile".[109] Jeremy Bentham na mwanafunzi wake Austin, wakimfuata David Hume, waliamini kuwa hili liliongeza utata wa "kilicho" na kile ambacho "kinafaa kuwepo". Bentham na Austin walisisitiza kuwe na sheria ya uchanya; na kuwa sheria ya kweli ni tofauti kabisa na "maadili".[110] Kant pia alikosolewa na Friedrich Nietzsche, ambaye alikataa kanuni ya usawa, huku akiamini kuwa sheria hutokana na nia kwa nguvu, na haiwezi fanywa kuwa ya "kimaadili" au "utovu wa nidhamu".[111][112][113]

Mnamo mwaka wa 1934, mwanafalsafa wa Kiaustria, Hans Kelsen, alizidi na mapokeo ya uchanya katika kitabu chake Nadharia Safi ya Sheria.[114] Kelsen aliamini kuwa ingawa sheria ni tofauti na maadili, inapewa "ukawaida"; kumaanisha kuwa tunfaa kuitii. Ingawa sheria ni taarfa chanya za "ni" (k.m. faini ya kuendesha kwa kurudi nyuma katika barabara kuu ni 500); hii sheria inatuelezea kile "tunachofaa" kutenda. Kwa hivyo kila mfumo wa sheria unaweza kudadisiwa kuwa na kanuni ya msingi (Grundnorm) ianyotupea amri ya kutii. Mpinzani mkuu wa Kelsen, Carl Schmitt, alikataa uchanya na dhana ya utawala wa sheria kwa sababu hakukubali umuhimu wa kanuni za kidhana za Uchanya badala ya mitazamo na uamuzi bayana wa kisiasa.[115] Kwa hiyo, Schmitt alipendekeza falsafa ya sheria ya maalum (hali ya dharura), ambayo ilikanusha kuwa kanuni za kisheria zingezunguka uzoefu wote wa kisiasa.[116]

 
Nadharia za Bentham za utumikiaji zilibaki kimya katika sheria hadi karne ya 20

Baadaye katika karne ya 20, H. L. A. Hart alimshambulia Austin kwa kurahisisha kwake kwa suala hilo na Kelsen kwa kutunga kwake kwa mambo ya kihadithi katika kitabu cha Dhana ya Sheria.[117] Hart alidokeza kuwa sheria ni mfumo wa kanuni, zilizogawanywa kuwa (kanuni za maadili) ambazo ndizo za kimsingi na sheria za upili (zinazowalenga maafisa kusimamia kanuni msingi). Kanuni za upili zimegawanywa zaidi kuwa sheria za uamuzi (kutatua migogoro ya kisheria), kanuni za mabadiliko (zinazoruhusu sheria kuwa tofauti) na sheria ya utambuzi(inayoruhusu sheria kutambulika kama halali). Wawili kati ya wanafunzi wa Hart waliendeleza mjadala: Ktaika kitabu chake Dola la Sheria, Ronald Dworkin alimshabulia Hart na wachanya kwa kukataa kwao la kufanya sheria iwe suala la kimaadili. Dworkin anadokeza kuwa sheria ni dhana ya "kitafsiri",[118] inayowataka mahakimu kupata suluhisho bora zaidi kwa mgogoro wa kisheria, kwa mujibu wa mila zao. Joseph Raz, kwa upande mwingine, anawataka alitetea mtazamo wa kichanya na kukosoa mtazamo wa Hart wa "nadharia laini ya kijamii" katika kitabu chake Mamlaka ya Sheria.[119] Raz anadokeza kuwa sheria ni mamlaka, yanayotambulika kupitia vyanzo vya kijamii na bila kurejelea hoja za kimaadili. Katika maoni yake, uainishaji wowote wa kanuni zozote zaidi ya majukumu yao kama vifaa vya kimamlaka katika upatanisha ni bora yaachiwe elimu ya jamii, badala ya falsafa ya sheria.[120]

Uchambuzi wa kiuchumi wa sheria hariri

Makala kuu: Sheria na uchumi

Katika karne ya 18 Adam Smith aliwasilisha msingi wa kifalsafa wa kuelezea uhusiano kati ya sheria na uchumi.[121] Taaluma hiyo ilitokana na mchango wa ukosoaji dhidi ya vyama vya wafanyikazi na sheria dhidi ya amana nchini Marekani. Watetezi wa taaluma hii waliokuwa na ushawishi mkubwa zaidi, kama vile Richard Posner na Oliver Williamson na kinachojulikana kama Shule ya Chicago ya wanauchumi na mawakili ikiwemo Milton Friedman na Gary Becker, kwa jumla ni watetezi wa uouguzaji wa udhibiti na ubinafsishaji, na ni maadui wa udhibiti wa serikali au kile wanachokiona kuwa vikwazo dhidi ya unedeshaji wa masoko huru.[122]

 
Richard Posner, mmoja wa watetezi wa Chuo cha Chicago, huandika blogu pamoja na Gary Becker mwanauchumi ambaye ni mshindi wa Tuzo la Benki ya Uswidi.[123]

Mchambuzi maarufu zaidi wa kiuchumi wa sheria ni mshindi wa Tuzo la Nobel la mnamo 1991 Ronald Coase, ambaye makala yake makuu ya kwanza, Hali ya Kampuni (1937), kulidokeza sababu za kuwepo kwa makampuni mbalimbali (makampuni, ubia, n.k.) ndiyo kuwepo kwa gharama za biashara.[124] Binadamu ambao hufikiria kawaida hufanya biashara kupitia mikataba ya bilaterala katika masoko wazi hadi wakati ambapo gharama ya biashara kunamaanisha kuwa kutumia makampuni ya kihalmasahhuri ili kuzalisha bidha ni ya ufanisi mwingi zaidi.Makala yake makuu ya pili, Shida ya Gharama ya Kijamii (1960), yalidokeza kuwa tunaishi katika Dunia bila gharama za kibiashara, watu ambao huongea kuhusu gharama pamoja wanatengeneza mgao sawa wa rasilimali, buila kujali jinsi mahakama yanavyoweza kuamua katika migogoro kuhusu mali.[125] Coase alitumia mfano wa kesi ya kero iliyoitwa Sturges dhidi ya Bridgman, ambapo mtengenezaji peremende ambaye alipiga kelele nyingi na daktari mtulivu walikuwa majirani na walienda mahakamani ili wajue nani kati yao ndiye angefa kuhama.[40] Coase alisema kuwa bila kujali ikiwa hakimu aliamua kuwa mtengenezaji peremende angefaa kuwacha kutumia mashine zake, au ikiwa ingembidi daktari kuvumilia kelele ile, wote wawili wangefikia mapatano ya pamoja kuhusu nani ndiye angefaa kuhama ambayo yanafikia matokeo sawa na mgawanyo wa rasilimali. Ni kuwepo tu kwa bei za biashara kunaoweza kuzuia hili.[126] Kwa hivyo sheria infaa kutazamia kile ambacho huenda kikafanyika, na kuongozwa na ufumbuzi wenye ufanisi. Wenye kuunda mipango serikalini wanaamini wazo kwamba sheria na vikwazo si muhimu au zenye ufanisi katika kuwasaidia watu.[127] Coase na wengine kama yeye walitaka mabadiliko ya mbinu, ili kuweka mzigo wa ushahidi katika serikali iliyokuwa ikiingilia soko, kwa kuchambua gharama za hatua.[128]

Elimujamii ya sheria hariri

Somo la kijamii la sheria ni taaluma pana ya masomo inayotazama mwingiliano kati ya sheria na jamii na inahusiana kwa karibu na falsafa ya sheria, uchambuzi wa kiuchumi wa sheria na masomo maalum zaidi kama somo la jinai.[129] Taasisi za ujenzi wa jamii na mifumo ya kisheria ni maeneo muhimu ya uchunguzi wa taaluma hii. Mwanzoni, wananadharia wa kisheria walishuku taaluma hii. Kelesen alimshambuliwa mmoja wa waanzilishi wake, Eugen Ehrlich, ambaye alitaka kuweka wazi tofauti kati ya sheria ya uchanya, ambayo mawakili wanajifunza na kutumia, na aina zingine za 'sheria' au kanuni za kijamii zinazodhibiti maisha ya kila siku, na kwa jumla kuzuiwa migogoro isiwafikie mawakili mahakamani.[130][131]

 
Max Weber mnamo mwaka wa 1917, Weber alianza kazi yake kama wakili, na antazamwa kama mmoja wa waanzilishi wa somo la jamii na somo la jamii la kisheria

Katika kipindi cha mwaka 1900 Max Weber alifafanua mbinu yake ya "kisayansi" ya sheria, huku akitambua "umbo la kimantiki ya sheria" kama aina ya utawala, ambao si chanzo cha watu lakini kwa dhana za kiakili.[132] Umantiki wa kisheria yalikuwa maneno yake aliyoyatumia kuelezea mwili wa sheria zinazoeleweka na zinazoweza kuhesabika na zilikuwa hatua ya kwanza ya maendeleo ya kisasa ya kisiasa na taifa la ukiritimba la kisasa na kuibuka sambamba na ubepari.[129] Msomi mwingine wa somo la jamii, Émile Durkheim, aliandika katika Mgawanyo wa Ujira na Jamii kuwa kadiri jamii inavyozidi kuwa kubwa, ndivyo mwili wa sheria ya kiraia unaohusika hasa na fidia unapozidi kukuwa kwa gharama ya sheria za jinai na vikwazo vya kisheria.[133] Wasomi wengine wa somo la jamii ni Hugo Sinzheimer, Theodor Geiger, Georges Gurvitch na Leon Petrażycki Barani Ulaya, na William Graham Sumner nchini Marekani[134][135]

Taasisi za kisheria hariri

Sheria si mwili wa kanuni zisizobadilika bali ni "machakato badilifu wa kanuni zinazobadilishwa kila wakati, kuundwa, na kupewa umbo ili kuambatana na hali fulani."[136] Mabadiliko yanafanywa kila wakati na taasisi mbalimbali katika jamii. Taasisi kuu za sheria katika Demokrasia huru ni Mahakama huru, mifumo ya haki, bunge, serikali yenye uwajibikaji, na ukiritimba wenye uwezo na usiokuwa na ufisadi , kiksoi cha polisi, kudhibitiwa kwa jeshi na raia na taaluma ya kisheria yenye nguvu inayohakikisha watu wanapta haki na jamii ya kiraia mbalimbali—neno linalotumika kuashiria taasisi za kijamii, jamii na ushirikiano unaunda msingi wa kisiasa wa sheria.[137][138]

John Locke, katika Maandiko Mawili kuhusu Serikali, na Baron de Montesquieu katika Roho ya Sheria, walitetea mgawanyo wa madaraka kati ya miili ya kisiasa ya bunge na serikali.[139] Kanuni yao ilikuwa kuwa hakuna mtu anayefaa kuwa na uwezo wa kuchukua mamlaka yote ya taifa, ikitofautishwa na nadharia ya uimla ya Thomas Hobbes' Leviathan.[140] Max Weber na wengine walibadilisha mawazo kuhusu taifa. Jeshi la kisasa, upolisi na mamalaka ya ukiritimba juu ya masiha ya raia wa kawaida husababisha matatizo maalum ya uwajibikaji ambayo waandishi wa awali kama vile Locke au Montesquieu hawangeweza kutabiri. Mashirika ya kisasa ya kimataifa huzingatia umuhimu wa utawala wa sheria na utawala mzuri, huku waandishi wengine hutafiti uhsusiano kati ya utawala wa sheria na utawala wa ufanisi katika nchi za kisasa.[141][142]

Mahakama hariri

Makala kuu: Mahakama

Mahakama ni idadi ya mahakimu wanaosikiza migogoro ili kuamua matokeo. Nchi nyingi zina mfumo wa mahakama ya rufaa, yanayojibu kwa mamlaka makuu ya kisheria. Nchini Marekani haya ni Mahakama Kuu ya Marekani;[143] nchini Australia, Mahakama Kuu ya Australia; nchini Uingereza , ni Mahakama Kuu ya Uingereza[144] (tangu tarehe1 Oktoba 2009; hapo awali yalikuwa, Nyumba ya Mabwana);[145] nchini Ujerumani ni Bundesverfassungsgericht; nchini Ufaransa ni Cour de Cassation.[146][147] Kwa nchi nyingi za Ulaya Mahakama ya Ulaya ya Haki nchini Luxembourg inaweza kuukataa umauzi wa kitaifa, wakati ambapo sheria ya Umoja wa Ulaya inafaa. Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu inayopatikana Strasbourg inawaruhusu raia wa nchi wanachama za Baraza la Ulaya kuleta kesi zao zinzohusiana na haki za kibinadamu mbele yake.[148]

Baadhi ya nchi huruhusu mamlaka yao makuu ya mahakama kukataa sheria wanayopata kuwa kinyume na katiba. Katika kesi ya Roe dhidi ya Wade, Mahakama Kuu ya Marekani ilipindua sheria ya jimbo la Texas iliyopiga marufuku kutoa msaada kwa wanawake wenye nia ya Kuavya mimba.[149] Marekebisho ya Kumi na Nne ya katiba ya Marekani yalikuwa yametafsiriwa kuwapa ya faragha, na kwa hivyo haki ya mwanamke kuchagua kuavya mimba.

Mahakama kinadharia yamefundwa na katiba, kama tu miili ya bunge. Katika nchi nyingi, mahakimu wana uwezo tu wa kutafsiri katiba na sheria zingine zote. Lakini katika nchi zasheria ya kawaida, ambapo mambo si ya kikatiba, mahakama pia yanweza kuunda sheria chini ya mafundisho ya utangulizi. Uingereza, Finland na New Zealand hutumia dhana ya uhuru wa bunge, ambapo mahakama ambayo hayajachaguliwa hayawezi kupindua sheria iliyopitishwa na bunge la kidemokrasia.[150] Katika nchi za kikomiunisti, kama vile Uchina, mahakama mara nyingi hutazamwa kama sehemu ya serikali, au kuwa chini ya bunge; taasisi za kiserikali na watendaji mbalimbali basi wana ushawishi tofauti kwa mahakama.[151] Katika nchi za Kiislamu, mahakama mara nyingi huchunguza ikiwa sheria za nchi zinafuata Sharia: Mahakama Kuu ya Kikatiba ya Misri inaweza kuoinga sheria kama hizo,[152] Na nchini Iran Baraza la Ulinzi linahakikisha uwiano wa sheria zinazopitishwa na "vigezo vya Uislamu".[152][153]

Bunge hariri

Makala kuu: Bunge
 
Chumba cha mjadala cha Bunge la Ulaya

Mifano maarufu ya bunge ni Majumba ya Bunge mjini London, Kongresi mjini Washingtin D.C., Bundestag mjini Berlin na Duma nchini Moscow, Parlamento Italiano mjini Roma na Assemblée nationale mjini Paris. Kwa kanuni ya serikali wakilishi watu hupigia kura wanasiasa ili watimize matakwa yao. Ingawa nchi kama Israeli, Ugiriki, Uswidi na Uchina zina nyumba moja ya bunge, nchi nyingi zina nyumba mbili za bunge, kumaanisha kuwa zina nyumba mbili za kibunge zinazochaguliwa tofauti. Katika 'nyumba ya chini' wanasiasa wanachaguliwa kuwakilisha maeneo wakilishi bungeni. 'Nymba ya juu' kawaida huchaguliwa kuwakilisha majimbo katika mfumo wa majimbo (kama vile nchii Australia, Ujerumani au Marekani) au upigaji kura tofauti katika katika mfumo wa umoja (kama vile nchini Ufaransa). Nchini Uingereza nyumba ya juu inachaguliwa na na serikali kama nyumba ya marudio. Ukosoaji mmoja wa mifumo yenye nyumba mbili yenye nyumba mbili zilizochaguliwa ni kuwa nyumba ya juu na ya chini huenda zikafanana. Utetezi wa tangu jadi wa mifumo ya nyumba mbili nni kuwa chumba cha juu huwa kama nyumba ya marekebisho. Hili linaweza kupunguza uonevu na dhuluma katika hatua ya kiserikali, 101</ref>

Ili kupitisha sheria, idadi kubwa ya Wabunge lazima wapige kura ili muswada (sheria inayopendekezwa) upitishwe katika kila nyumba. Kawaida kutakuwa na kusoma kwingi na marekebesho mengi yaliyopendekezwa na makundi tofaiti ya kisiasa. Ikiwa nchi ina katiba inayofuatiliwa vyema, idadi maalum ya mabadiliko katika katiba yanahitajika, hivyo kufanya iwe gumu kubadilisha sheria. Serikali kwa kawaida huongoza mchakato huo, ambao unaweza kujumuisha Wabunge (k.m. nchini Uingereza na Ujerumani). Lakini katika mfumo wa kiraisi, serikali inachagua baraza la mawaziri kutawala kutoka kwa washirika wake kisiasa ikiwa wamechaguliwa au la (k.m. nchini Marekani au Brazili), na jukumu la bunge linapunguza liwe kukubali au kukataa.[154]

Serikali hariri

Makala kuu: Serikali
 
Mikutano ya G20 inahusisha wawakilishi wa serikali ya kila nchi

Mtendaji katika mfumo wa kisheria hutumika kama kituo cha serikali cha mamlaka ya kisiasa. Katika mfumo wa kibunge, kama vile nchini Uingereza, Italia, Ujerumani na Ujapani, mtendaji hujulikana kama serikali, na huwa na wanachama wa bunge. Mtendaji huchaguliwa na Waziri Mkuu au Chansela, ambaye ofisi yake ina nguvu za chini ya imani ya bunge. Kwa sababu uchaguzi wenye watu wengi huteua vyama vya kisiasa kutawala, kiongozi a chama anaweza kubadilika katika kipindi kabla ya uchaguzi mwingine. Mkuu wa Taifa ni kando na mtendaji, na kimfano hupitisha sheria na huwa kama mwakilishi wa nchi. Baadhi ya mifano ni Rais wa Ujerumani (anayeapishwa na Bunge); Malkia wa Uingereza (wadhifa wa kurithi), na Rais wa Austria (anachaguliwa kwa kura ya wengi). Mfano mwingine muhimu ni mfumo wa kirais, unaopatikana nchini Ufaransa, Marekani na Urusi. Katika mifumo ya kirais, mtrndaji huwa kama mkuu wa taifa na mkuu wa serikali, na ana nguvu za kuchagua baraza la mawaziri pekee yake. Chini ya mfumo wa kirais, tawi la mtendaji ni kando na bunge ambapo haiwajibiki mbele ya bunge.[155][156]

Ingawa jukumu la mtendaji ni tofauti toka nchi moja hado nyingine, kawaida itapendekeza wingi wa sheria, na kupendekeza ajenda ya serikali. Katika mifumo ya kirais, mtendaji mara nyingi ana nguvu za kukataa sheria. Mara nyingi mtendaji katika mifumo yote ana wajibu wa sera za mahusiano ya nje, jeshi na polisi na urasimu. Mawaziri au maafisa wengine wanasimamia ofisi za nchi, kama vile wizara ya nje au wizara ya ndani. Uchaguzi wa mtendaji tofauti kwa hivyo ina uwezo wa kupindua mtazamo wa nchi nzima wa serikali.

Jeshi na polisi hariri

Makala kuu: Jeshi na Polisi
 
Maafisa wa Marekani wa Forodha na Ulinzi wa Mipaka

Ingawa mashirika ya kijeshi yamekuwepo kwa muda mrefu kama serikali yenyewe, dhana la kikosi cha polisi kilicho tayari ni dhana ya kisasa. Mfumo wa Uingereza ya Zama za Kati ya mahakama ya jinai ya kusafiri, au assize, ilitumia kesi za maonyesho na unyongaji hadharani kufanya jamii ziwe na hofu na hivyo kudumisha udhibiti.[157] Polisi wa kwanza wa kisasa pengine walikuwa wale wa Paris wa karne ya 17, katika mahakama ya Louis XIV,[158] ingawa Polisi wa Mkoa wa Paris ndio wanadai kuwa wao ndio waliokuwa wa kwanza kuvaa sare.[159]

Weber yu maarufu kwa kudokeza kwamba taifa ni lile ambalo linadhibiti kihalali utumizi wa kipekee wa vurugu.[160][161] Majeshi na askari wanalinda usalama kufuatana na amri ya serikali au mahakama. Maneno taifa lililopangarayika yanaashiria taifa ambalo haliwezi kutekeleza au kulazimisha sera; askari wao na majeshi hawana uwezo wa kulinda usalama na amani na jamii inaelekea vurugu pekee, wakati serikali inapokosekana.[162]

Urasimu hariri

Makala kuu: Urasimu
 
Makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York yana watumishi wa kiserikali wanaotoa huduma kwa mataifa wanachama 192 ya shirika hilo.

Asili ya neno "Urasimu" kwa Kiingereza (bureaucracy) ni neno la Kifaransa la "ofisi" (bureau) na neno la Kigiriki cha Zamani cha "nguvu" (kratos).[163] Kama tu wanajeshi na polisi, watumishi wa mfumo wa kisheria wa serikali na miili inayounda urasimu wake hufuata maagizo ya Mtendaji. Mojawapo ya marejeo kwa dhana yalifanywa Baron de Grimm, mwandishi wa Kijerumani aliyeishi nchini Ufaransa. Mnamo mwaka wa 1765 aliandika,

Roho halisi ya sheria nchini Ufaransa ni urasimu amabo marehemu Monsieur de Gournay alikuwa akilalamika sana kuhusu; hapa ofisi, makarani, makatibu, wasimamizi na wanaonuia kufanya kazi fulani hawaapishwi kufaidi maslahi ya umma, kwa hakika maslahi ya ummayanaonekana kuanzishwa ili ofisi hizo ziwepo.[164]

Wasiwasi kuhusu "utawala wa kiofisi" bado ni kawaida, na utendaji wa watumishi wa umma kawaida hutofautishwa na wa kampuni za kibinafsi zinazoendeshwa na lengo la faida.[165] Kwa kweli kampuni za kibinafsi, hasa zile kubwa, pia zina urasimu.[166] Mtazamo mbaya wa "urasimu" kando, huduma za umma kama vile elimu, afya na shughuli za polisi au uchukuzi wa umma ni kazi muhimu nchi hivyo basi kufanya urasimu wa umma chanzo cha nguvu za serikali.[166] Akiandika mapema katika karne ya 20, Max Weber aliamini kuwa sifa muhimu ya nchi iliyoendelea ilikuwa imekuwa msaada wake wa kirasimu.[167] Weber aliandika kuwa sifa za kawaida za urasimu wa kisasa ni kuwa maafisa wanafafanua lengo lake, wigo wa kazi umefungwa na kanuni, usimamizi unajumuisha wataalamu wa wataalamu wa kitaaluma, amabo ambao husimamia kuanzia juu kuenda chini, wakiwasiliana kupitia kuandika na kufunga uwezo wa wafanyikazi wa umma kufanya watakavyo kwa kutumia kanuni.[168]

Taaluma ya sheria hariri

Makala kuu: Taaluma ya sheria
 
Katika mifumo ya sheria ya kiraia kama ile ya Ufaransa, Ujerumani, Italia, Uhispania na Ugiriki, kuna aina maalum ya Karani wa sheria ya kiraia, afisaa wa umma mwenye ufunzi wa kisheria, anayelipwa fidia na wanaofanya biasharaa.[169] Hii ni picha ya karne ya 16 ya karani wa sheria ya kiraia kama huyo ya mchoraji wa Kiflemi Quentin Massys.

Hitimisho la utawala wa sheria ni kuwepo kwa taaluma ya kisheria yenye uhuru wa kutosha wa kuweza kuomba mamlaka ya mahakama huru; haki ya usaidizi kusaidiwa na wakili mahakamani uanatokana na hitimisho hili—nchini Uingereza kazi ya wakili inatofautishwa na ile ya mshauri wa kisheria.[170] Kama mahakama ya Ulaya ya Haki za Binadamu yanavyosema, sheria inafaa kupatikana na kila mtu na waty wanfaa kutabiri jinsi sheria itakavyowaathiri.[171] Ili kudumisha utaaluma, zoezi la sheria kawaida linachungwa na serikali au mwili huru kama vile chama cha mawikili, baraza la mawakili au jamii ya sheria. Mawakili wa kisasa wanapata utambulisho maalum wa kisheria kupitia taratibu maalum za kisheria (k.m. mafanikio katika mitihani), yanahitajika na sheria ili kuwa na cheti maalum (elimi ya kisheria inayompa mwanafunzi Shahada ya Sheria, Shahada ya Sgeria ya Kiraia, au Shahada ya Juris Doctor[172]), na zinawekwa ofisini kwa kutumia fomu za kisheria za kuapishwa (kukubaliwa katika baraza la mawakili). Nchi nyingi za Kiisalmu zina sheria sawa kuhusu elimu ya kisheria na taaluma ya kisheria, lakini zingine bado zinaruhusu mawakili wenye mafunzo katika sheria ya Kiislamu ya jadi katika taaaluma ua sheria katika mahakama ya hadhi ya kibinasfi.[173] Nchini Uchina na katika nchi zingine za ulimwengu unaoendelea hakuna watu wa kutosha wenye mafunzo ya kisheria kufanya kazi katika mifumo ya mahakama iliyopo katika nchi hizo, na, kufuatana na hilo, viwango rasmi si vikali sana.[174]

Baada ya kupata kukubalika, wakili mara nyingi atafanya kazi katika kampuni ya sheria, katika vyumba kama wakili wa kipekee, katika wadhifa wa kiserikali au katika shirika la kibinafsi kama mshauri wa ndani. Isitoshe wakili anaweza kuwa [[|utafiti wa kisheria|mtafiti wa kisheria]] anayepeana uatafiti wa kisheria unapoitishwa kupitia maktaba, huduma ya kibiashara au kazi isiyokuwa na muajiri mmoja. Watu wengi wenye mafunzo katika sheria walitumia utafiti wao katika taaluma nyingine tofauti kabisa. Adhimu kwa zoezi la sheria katika mapokeo ya sheria ya kawaida ni utafiti wa kisheria kujua hali ya wakati wa sasa wa sheria. Hili linahushisha kuchunguza ripoti za kesi, majarida ya kisheria na sheria. Zoezi la sheria pia inahusu kuandika hati kama vile kuiitia kwa mahakama, [[brifu [sheria)|brifu]], mikataba, au amana. Majadiliano na ujuzu wa kusuluhisha migogoro (ikijumuisha mbinu za ADR) pia ni muhimi kwa zoezi la sheria, ikitegemea na aina ya taaluma.[175]

Mashirika ya kijamii hariri

 
Maandamano mjini Washington D.C. wakati wa Harakati ya Haki za Kiraia ya Marekani mnamo mwaka wa 1963

Dhana ya Kiripablikani wakati kulipokuwa na madaraja mbalimbali ya kijamii ya "mashirika ya kijamii" ilianzia wakati wa Hobbes na Locke.[176] Locke aliona mashirika ya kijamii kama watu wenye "sheria sawa na mahakama kurejelea , yenye mamlaka ya kuamua utata baina yao."[177] Mwanafalsafa wa Kijerumani Georg Wilhelm Friedrich Hegel alitofautisha "taifa" na "mashirika ya kijamii" (burgerliche Gesellschaft) katika kitabu chake Vipengele vya Falsafa ya Sawa.[178] Hegel aliamini kuwa mashirika ya kijamii na taifa zilikuwa kinyume kabisa, katika mpangilio wa nadharia yake ya historia. Taifa la kisasa lenye pande hizi mbili–mashirika ya kijamii lilizaliwa tena katika nadharia za Alexis de Tocqueville na Karl Marx.[179][180] Siku hizi katika nadharia ya wakati wa baada ya kisasa za mashirika la kijamii lazima iwe chanzo cha sheria, kwa kuwa msingi ambapo watu wanaunda maoni na kushwishi yale wanayoamini sheria inafaa kuwa. Kama wakili wa Kiaustralia na mwandishi Geoffrey Robertson QC alivyoandika kuhusu sheria ya kimataifa,

... mojawapo ya vyanzo vyake vya kisasa inapatikana katika majibu ya kawaida ya wanaume na wanawake, na mashirika yasiyo ya kiserikali, amabyo wengi huunga, kwa ukiukaji wa haki za kibinadamu amabyo wengi huona kwenye runinga wakiwa sebuleni nyumbani mwao.[181]

Uhuru wa kujieleza, uhuru wa kujumuika na sheria zingine nyingi za kibinafsi zinawaruhusu watu kukusanyika, kujadili, kukosoa na kufanya serikali zao kuwajibika, ambapo msingi wa demokrasia ya majadiliano inaibuka. Watu wanapozidi kujihusisha mamlaka ya kisheria na na kuwa na uwezo wa kubadilisha jinsi mamlaka ya kisiasa yanapotumika maishani mwao; ndivyo sheria inapozidi kuwa halali kwa watu. Taasisi ambazo ni za kawaida sana za mashirika ya kijamii ni masoko ya kibiashra, kampuni zenye malengo ya kupata faida, familia, vyama vya kibiashara, hospitali, vyuo vikuu, shule, mashirika ya msaada, vilabu vya kujadili, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, vitongoji, makanisa, na vyama vya kidini.[182]


Tazama pia hariri

  [[Portal:{{{1}}}|{{{1}}} portal]]

Tanbihi hariri

  1. Hamilton, Marci. God vs. the Gavel, page 296 (Cambridge University Press 2005): “The symbol of the judicial system, seen in courtrooms throughout the United States, is blindfolded Lady Justice.”
  2. Fabri, Marco. The challenge of change for judicial systems, page 137 (IOS Press 2000): “the judicial system is intended to be apolitical, its symbol being that of a blindfolded Lady Justice holding balanced scales.”
  3. Luban, Law's Blindfold, 23
  4. from Old English lagu "Words of Mel"; legal comes from Latin legalis, from lex "law", "statute" (Law, Online Etymology Dictionary; Legal, Merriam-Webster's Online Dictionary)
  5. Robertson, Crimes against humanity, 90; see "analytical jurisprudence" for extensive debate on what law is; in The Concept of Law Hart argued law is a "system of rules" (Campbell, The Contribution of Legal Studies, 184); Austin said law was "the command of a sovereign, backed by the threat of a sanction" (Bix, John Austin); Dworkin describes law as an "interpretive concept" to achieve justice (Dworkin, Law's Empire, 410); and Raz argues law is an "authority" to mediate people's interests (Raz, The Authority of Law, 3–36).
  6. "it is more proper that law should govern than any one of the citizens: upon the same principle, if it is advantageous to place the supreme power in some particular persons, they should be appointed to be only guardians, and the servants of the laws." (Aristotle, Politics 3.16).
  7. The original French is: "La loi, dans un grand souci d'égalité, interdit aux riches comme aux pauvres de coucher sous les ponts, de mendier dans les rues et de voler du pain" (France, The Red Lily, Chapter VII).
  8. Although many scholars argue that "the boundaries between public and private law are becoming blurred", and that this distinction has become mere "folklore" (Bergkamp, Liability and Environment, 1–2).
  9. E.g. in England these seven subjects, with EU law substituted for international law, make up a "qualifying law degree". For criticism, see Peter Birks' poignant comments attached to a previous version of the Notice to Law Schools.
  10. History of the UN, United Nations. Winston Churchill (The Hinge of Fate, 719) comments on the League of Nations' failure: "It was wrong to say that the League failed. It was rather the member states who had failed the League."
  11. The prevailing manner of enforcing international law is still essentially "self help"; that is the reaction by states to alleged breaches of international obligations by other states (Robertson, Crimes against Humanity, 90; Schermers-Blokker, International Institutional Law, 900–901).
  12. Petersmann, The GATT/WTO Dispute Settlement System, 32
  13. Redfem, International Commercial Arbitration, 68–69
  14. Schermers–Blokker, International Institutional Law, 943
  15. See the C-26/62 Van Gend en Loos v Nederlanse Administratie Der Belastingen, and Flaminio Costa v E.N.E.L. decisions of the European Court.
  16. Entick v Carrington (1765) 19 Howell's State Trials 1030; [1765] 95 ER 807
  17. Entick v Carrington. 19 Howell’s State Trials 1029 (1765). Constitution Society. Iliwekwa mnamo 2008-11-13.
  18. Locke, The Second Treatise, Chapter 9, section 124
  19. Tamanaha, On the Rule of Law, 47
  20. Auby, Administrative Law in France, 75
  21. Cesare Beccaria's seminal treatise of 1763–1764 is titled On Crimes and Punishments (Dei delitti e delle pene).
  22. 22.0 22.1 Brody, Acker and Logan, Criminal Law, 2; Wilson, Criminal Law, 2
  23. Brody, Acker and Logan, Criminal Law, 2
  24. See e.g. Brody, Acker and Logan, Criminal Law, 205 about Robinson v California, 370 U.S. 660 (1962).
  25. See e.g. Feinman, Law 111, 260–261 about Powell v Texas, 392 U.S. 514 (1968).
  26. Dörmann, Doswald-Beck and Kolb, Elements of War Crimes, 491
  27. Kaiser, Leistungsstörungen, 333
  28. About R v Dudley and Stephens [1884] 14 QBD 273 DC Archived 28 Februari 2005 at the Wayback Machine., see Simpson, Cannibalism and the Common Law, 212–217, 229–237
  29. Pelser, Criminal Legislation, 198
  30. The States Parties to the Rome Statute, International Criminal Court
  31. Wenberg, Pacta Sunt Servanda, 775
  32. About Carlill v Carbolic Smoke Ball Company Archived 5 Desemba 2004 at the Wayback Machine. [1893] 1 QB 256, and the element of consideration, see Beale and Tallon, Contract Law, 142–143
  33. Austotel v Franklins (1989) 16 NSWLR 582
  34. e.g. In Germany, § 311 Abs. II BGB
  35. § 105 Abs. II BGB
  36. Smith, The Structure of Unjust Enrichment Law, 1037
  37. Bolton v Stone [1951] AC 850
  38. 38.0 38.1 Donoghue v Stevenson ([1932] A.C. 532, 1932 S.C. (H.L.) 31, [1932] All ER Rep 1). See the original text of the case in UK Law Online Archived 16 Februari 2007 at the Wayback Machine..
  39. Donoghue v Stevenson [1932] AC 532, 580
  40. 40.0 40.1 Sturges v Bridgman (1879) 11 Ch D 852
  41. e.g. concerning a British politician and the Iraq War, George Galloway v Telegraph Group Ltd [2004] EWHC 2786
  42. Taff Vale Railway Co v Amalgamated Society of Railway Servants [1901] AC 426
  43. In the UK, Trade Union and Labour Relations (Consolidation) Act 1992; c.f. in the U.S., National Labor Relations Act
  44. Harris, The Bubble Act, 610-627
  45. eg Hunter v Canary Wharf Ltd [1997] 2 All ER 426
  46. Armory v Delamirie (1722) 93 ER 664, 1 Strange 505
  47. Matthews, The Man of Property, 251–274
  48. Savigny, Das Recht des Besitzes, 25 Archived 18 Aprili 2008 at the Wayback Machine.
  49. Locke, Second Treatise on Civil Government, Chap. IX. Of the Ends of Political Society and Government. Chapter 9, section 123.
  50. McGhee, Snell's Equity, 7
  51. c.f. Bristol and West Building Society v Mothew [1998] Ch 1
  52. Keech v Sandford (1726) Sel Cas Ch 61
  53. Nestle v National Westminster Bank plc [1993] 1 WLR 1260
  54. A Guide to the Treaty of Lisbon, The Law Society
  55. Berle, Modern Corporation and Private Property
  56. WIPO, Intellectual Property, 3
  57. Modern scholars argue that the significance of this distinction has progressively declined; the numerous legal transplants, typical of modern law, result in the sharing by modern legal systems of many features traditionally considered typical of either common law or civil law (Mattei, Comparative Law and Economics, 71)
  58. Civil law jurisdictions recognise custom as "the other source of law"; hence, scholars tend to divide the civil law into the broad categories of "written law" (ius scriptum) or legislation, and "unwritten law" (ius non scriptum) or custom. Yet they tend to dismiss custom as being of slight importance compared to legislation (Georgiadis, General Principles of Civil Law, 19; Washofsky, Taking Precedent Seriously, 7).
  59. Gordley-von Mehren, Comparative Study of Private Law, 18
  60. Gordley-von Mehren, Comparative Study of Private Law, 21
  61. Stein, Roman Law in European History, 32
  62. Stein, Roman Law in European History, 35
  63. Stein, Roman Law in European History, 43
  64. Badr, Islamic Law, 187–198 [196–8]
  65. 65.0 65.1 Makdisi, The Islamic Origins, 1635–1739
  66. Hatzis, The Short-Lived Influence of the Napoleonic Civil Code in Greece, 253–263
  67. Demirgüç-Kunt -Levine, Financial Structures and Economic Growth, 204
  68. The World Factbook — Field Listing – Legal system Archived 26 Desemba 2018 at the Wayback Machine., CIA
  69. Magna Carta Archived 10 Septemba 2014 at the Wayback Machine., Fordham University
  70. Gordley-von Mehren, Comparative Study of Private Law, 4
  71. Gordley-von Mehren, Comparative Study of Private Law, 3
  72. Pollock (ed) Table Talk of John Selden (1927) 43; "Equity is a roguish thing. For law we have a measure... equity is according to the conscience of him that is Chancellor, and as that is longer or narrower, so is equity. 'Tis all one as if they should make the stadard for the measure a Chancellor's foot."
  73. Gee v Pritchard (1818) 2 Swans. 402, 414
  74. Blackstone, Commentaries on the Laws of England, Book the First – Chapter the First Archived 29 Machi 2013 at the Wayback Machine.
  75. Gordley-von Mehren, Comparative Study of Private Law, 17
  76. Glenn, Legal Traditions of the World, 159
  77. Anderson, Law Reform in the Middle East, 43
  78. Giannoulatos, Islam, 274–275
  79. Sherif, Constitutions of Arab Countries, 157–158
  80. Saudi Arabia, Jurist
  81. Akhlagi, Iranian Commercial Law, 127
  82. Hallaq, The Origins and Evolution of Islamic Law, 1
  83. Théodoridés. "law". Encyclopedia of the Archaeology of Ancient Egypt.
  84. VerSteeg, Law in ancient Egypt
  85. Richardson, Hammurabi's Laws, 11
  86. Kelly, A Short History of Western Legal Theory, 5–6
  87. Ober, The Nature of Athenian Democracy, 121
  88. Kelly, A Short History of Western Legal Theory, 39
  89. Stein, Roman Law in European History, 1
  90. Kama mfumo wa kisheria, Sheria ya Kirumi imeathiri moja kwa moja sheria za duniani kote. Pia ni sehemu ya msingi ya mkusanyiko wa sheria wa nchi nyingi za barani Ulaya, na imekuwa muhimu katika kuunda kwa dhana ya utamaduni sawa Ulaya (Stein, Sheria ya Kirumi katika Historia ya Ulaya, 2, 104–107).
  91. Sealey-Hooley, Commercial Law, 14
  92. Mattei, Comparative Law and Economics, 71
  93. Badr, Islamic Law, 187–198
  94. Justice Gamal Moursi Badr argues that Islamic law may "be called a lawyer's law if common law is a judge's law"(Badr, Islamic Law, 187–198, El-Gamal, Islamic Finance, 16).
  95. The "royal English contract protected by the action of debt is identified with the Islamic Aqd, the English assize of novel disseisin is identified with the Islamic Istihqaq, and the English jury is identified with the Islamic Lafif". Other parallels include "the scholastic method, the license to teach" (Ijazah), the "law schools known as Inns of Court in England and Madrasas in Islam", and the agency (Hawala) and trust law (Waqf) (Gaudiosi, The Influence of the Islamic Law , 1231–1261; Makdisi, The Islamic Origins, 1635–1739).
  96. For discussion of the composition and dating of these sources, see Olivelle, Manu's Code of Law, 18-25.
  97. Glenn, Legal Traditions of the World, 276
  98. Glenn, Legal Traditions of the World, 273
  99. Glenn, Legal Traditions of the World, 287
  100. Glenn, Legal Traditions of the World, 304
  101. Glenn, Legal Traditions of the World, 305
  102. Glenn, Legal Traditions of the World, 307
  103. Glenn, Legal Traditions of the World, 309
  104. Farah, Five Years of China WTO Membership, 263–304
  105. Bix, John Austin
  106. Roeber, What the Law Requires, 887
  107. Stone, Human Law and Human Justice, 14, 51
  108. Fritz Berolzheimer, The World's Legal Philosophies, 115–116
  109. Kant, Immanuel, Groundwork of the Metaphysics of Morals, 42 (par. 434)
  110. Green, Legal Positivism
  111. Nietzsche, Zur Genealogie der Moral, Second Essay, 11
  112. Kazantzakis, Friedrich Nietzsche and the Philosophy of Law, 97–98
  113. Linarelli, Nietzsche in Law's Cathedral, 23–26
  114. Marmor, The Pure Theory of Law
  115. Bielefeldt, Carl Schmitt's Critique of Liberalism, 25–26
  116. Finn, Constitutions in Crisis, 170–171
  117. Bayles, Hart's Legal Philosophy, 21
  118. Dworkin, Law's Empire, 410
  119. Raz, The Authority of Law, 3–36
  120. Raz, The Authority of Law, 37 etc.
  121. According to Malloy (Law and Economics, 114), Smith established "a classical liberal philosophy that made individuals the key referential sign while acknowledging that we live not alone but in community with others".
  122. Jakoby, Economic Ideas and the Labour Market, 53
  123. The Becker-Posner Blog. Iliwekwa mnamo 2007-02-03.
  124. Coase, The Nature of the Firm, 386–405
  125. Coase, The Problem of Social Cost, 1–44
  126. Coase, The Problem of Social Cost, IV, 7
  127. Coase, The Problem of Social Cost, V, 9
  128. Coase, The Problem of Social Cost, VIII, 23
  129. 129.0 129.1 Jary, Collins Dictionary of Sociology, 636
  130. Rottleuthner, La Sociologie du Droit en Allemagne, 109
  131. Rottleuthner, Rechtstheoritische Probleme der Sociologie des Rechts, 521
  132. Rheinstein, Max Weber on Law and Economy in Society, 336
  133. Johnson, The Blackwell Dictionary of Sociology, 156
  134. Gurvitch, Sociology of Law, 142
  135. Papachristou, Sociology of Law, 81–82
  136. Hamilton and Spiro, The Dynamics of Law, 3
  137. Jakobs, Pursuing Equal Opportunities, 5–6
  138. Karkatsoulis, The State in Transition, 275 etc.
  139. Montesquieu, The Spirit of Laws, Book XI: Of the Laws Which Establish Political Liberty, with Regard to the Constitution, Chapters 6–7
  140. Thomas Hobbes, Leviathan, XVII
  141. Curtin–Wessel, Good Governance, 73
  142. Fukuyama, State-Building, 132
  143. A Brief Overview of the Supreme Court, Supreme Court of the United States
  144. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-10-16. Iliwekwa mnamo 2010-01-15.
  145. House of Lords Judgements, House of Lords
  146. Entscheidungen des Bundesverfassungsgerichts Archived 21 Novemba 2006 at the Wayback Machine., Bundesverfassungsgericht
  147. Jurisprudence, publications, documentation Archived 9 Februari 2007 at the Wayback Machine., Cour de cassation
  148. Goldhaber, European Court of Human Rights, 1–2
  149. Roe v Wade (1973) 410 U.S. 113 Retrieved 2007-01-26
  150. Dicey, Law of the Constitution, 37–82
  151. E.g., the court president is a political appointee (Jensen–Heller, Introduction, 11–12). About the notion of "judicial independence" in China, see Findlay, Judiciary in the PRC, 282–284
  152. 152.0 152.1 Sherif, Constitutions of Arab Countries, 158
  153. Rasekh, Islamism and Republicanism, 115–116
  154. About "cabinet accountability" in both presidential and parliamentary systems, see Shugart–Haggard, Presidential Systems, 67 etc.
  155. Haggard, Presidents, Parliaments and Policy, 71
  156. Olson, The New Parliaments of Central and Eastern Europe, 7
  157. See, eg Tuberville v Savage (1669), 1 Mod. Rep. 3, 86 Eng. Rep. 684, where a knight said in a threatening tone to a layman, "If it were not assize time, I would not take such language from you."
  158. History of Police Forces, History.com Encyclopedia
  159. Des Sergents de Ville et Gardiens de la Paix à la Police de Proximité, La Préfecture de Police
  160. Weber, Politics as a Vocation
  161. Weber, The Theory of Social and Economic Organisation, 154
  162. In these cases sovereignty is eroded, and often warlords acquire excessive powers (Fukuyama, State-Building, 166–167).
  163. Bureaucracy, Online Etymology Dictionary
  164. Albrow, Bureaucracy, 16
  165. Mises, Bureaucracy, II, Bureaucratic Management
  166. 166.0 166.1 Kettl, Public Bureaucracies, 367
  167. Weber, Economy and Society, I, 393
  168. Kettl, Public Bureaucracies, 371
  169. Hazard–Dondi, Legal Ethics, 22
  170. Hazard–Dondi, Legal Ethics, 1
  171. The Sunday Times v The United Kingdom [1979] ECHR 1 at 49 Case no. 6538/74
  172. Higher academic degrees may also be pursued. Examples include a Master of Laws, a Master of Legal Studies or a Doctor of Laws.
  173. Ahamd, Lawyers: Islamic Law
  174. Hazard–Dondi, Legal Ethics, 22–23
  175. Fine, The Globalisation of Legal Education, 364
  176. Warren, Civil Society, 3–4
  177. Locke, Second Treatise, Chap. VII, Of Political or Civil_Society. Chapter 7, section 87
  178. Hegel, Elements of the Philosophy of Right, 3, II, 182; Karkatsoulis, The State in Transition, 277–278
  179. (Pelczynski, The State and Civil Society, 1–13; Warren, Civil Society, 5–9)
  180. Zaleski, Pawel (2008). "Tocqueville on Civilian Society. A Romantic Vision of the Dichotomic Structure of Social Reality". Archiv für Begriffsgeschichte (Felix Meiner Verlag) 50. 
  181. Robertson, Crimes Against Humanity, 98–99
  182. There is no clear legal definition of the civil society, and of the institutions it includes. Most of the institutions and bodies who try to give a list of institutions (such as the European Economic and Social Committee) exclude the political parties. For further information, see Jakobs, Pursuing Equal Opportunities, 5–6; Kaldor–Anheier–Glasius, Global Civil Society, passim Archived 17 Agosti 2007 at the Wayback Machine. (PDF); Karkatsoulis, The State in Transition, 282–283.

https://www.path-2-happiness.com/sw

Marejeo hariri

Printed sources
Online sources

Viungo vya nje hariri

Jua habari zaidi kuhusu Law kwa kutafuta kupitia mradi wa Wikipedia Sister
  Uchambuzi wa kamusi kutoka Wikamusi
  Vitabu kutoka Wikitabu
  Dondoo kutoka Wikidondoa
  Matini za vyanzo kutoka Wikichanzo
  Picha na media kutoka Commons
  Habari kutoka Wikihabari
  Vyanzo vya elimu kutoka Wikichuo