Jongoo Miguu-michache

(Elekezwa kutoka Pauropoda)
Jongoo miguu-michache
Spishi isiyotambuliwa ya Pauropoda
Spishi isiyotambuliwa ya Pauropoda
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Faila: Arthropoda
Nusufaila: Myriapoda
Ngeli: Pauropoda
Oda: Pauropodina
Ngazi za chini

Familia:

Majongoo miguu-michache ni aina za arithropodi wadogo katika ngeli Pauropoda ya nusufaila Myriopoda. Wana mnasaba na majongoo ya kawaida lakini wana urefu mfupi (mm 0.5-2) na miguu michache kuliko hawa (jozi 9-11 katika wanyama wazima). Vipapasio vyao vina vitawi. Hawana macho wala moyo. Huonekana katika udongo na inawezekana kama hula kuvu na dutu ya viumbehai.

Picha hariri

  Makala hii kuhusu "Jongoo Miguu-michache" inatumia neno (au maneno) ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio la kutafsiri neno (au maneno) la asili Pauropoda kutoka lugha ya Kilatini. Neno (au maneno) la jaribio ni jongoo miguu-michache.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.