Rijili ya Jabari (en:Rigel) ni nyota jitu katika kundinyota la Jabari (en:Orion).

Mahali pa Rijili Jabari (=Rigel) katika Jabari - Orion
Ulinganifu wa ukubwa baina ya Rijili Jabari na Jua letu (kushoto)

Jina hariri

Jina la Kiswahili Rijili ya Jabari linatokana na ar. رجل الجبار rijil-al-jabar. Maana ya jina ni "mguu wa jitu" maana mataifa ya kale waliona kundinyota lote kama picha ya jitu katika anga. Jina la kimagharibi "Rigel"[1] linatokana pia na neno lilelile la Kiarabu kwa "mguu" yaani رجل inayoandikwa kwa herufi za Kilatini ama "rijil" au "rigil". [2].

Jina la kitaalamu kufuatana na mfumo wa Bayer ni Beta Orionis kwa maana ya kwamba ilitazamiwa kuwa nyota ya pili kwa uangavu kati ya nyota za Jabari (Orion).

Tabia hariri

Rijili Jabari inaonekana kama nyota angavu sana kwenye anga la usiku. Mwangaza unaoonekana ni 0.13 mag kwa hiyo ni nyota angavu ya saba angani. Rangi yake ni nyeupe hadi buluu-nyeupe. Katika darubini kubwa inaonekana kama nyota maradufu yaani mfumo wa nyota tatu, labda pia tano.

Umbali na dunia ni miaka nuru 778.

Tanbihi hariri

  1. ni pia jina lililokubaliwa na Umoja wa Kimataifa wa Astronomia, ling. The Constellations, tovuti ya International Astronomical Union, iliangaliwa Julai 2017
  2. Herufi ya ج kwa kawaida husomwa kama "j" jinsi ilivyo pia kwenye Rasi ya Uarabuni lakini pale Misri matamshi ya "g" ni kawaida. Vokali fupi za i na e hazitofautishwi katika mwandiko wa Kiarabu