Sakristia

Sakristia (kutoka Kilatini "sacristia"; kwa Kiingereza "sacristy") ni chumba maalumu kwa ajili ya kutunza mavazi ya liturujia (kama vile alba na kasula) na vifaa vingine vya ibada za Kikristo (kama vile mkate, divai, mishumaa n.k.).[1]

Sakristia ikiwa na mavazi yameandaliwa.

Kwa kawaida sakristia iko jirani na ukumbi wa kanisa, ili padri na watumishi waingie moja kwa moja baada ya kuvaa kiibada.

TanbihiEdit

  1. Vestry. Oxford University Press. Jalada kutoka ya awali juu ya 2016-11-26. Iliwekwa mnamo 2017-10-14.

Viungo vya njeEdit

Wikimedia Commons ina media kuhusu: