Shakwe-mporaji
Shakwe-mporaji pomarina
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Charadriiformes (Ndege kama vitwitwi)
Familia: Stercorariidae (Ndege walio na mnasaba na shakwe-waporaji)
Jenasi: Stercorarius
Spishi: S. longicaudus (Vieillot, 1819)

S. parasiticus (Linnaeus, 1758)
S. pomarinus (Linnaeus, 1758)
S. skua Brünnich, 1764
S. antarcticus Brooke, 1978
S. chilensis (Bonaparte, 1857)
S. maccormicki (Vieillot, 1819)

Shakwe-waporaji ni ndege wa jenasi Stercorarius, jenasi pekee katika familia Stercorariidae. Pengine huitwa skua pia. Hawa ni ndege wakubwa kadiri ambao wana mnasaba na shakwe. Wana rangi ya kahawa au kijivu; spishi ndogo zina madoa meupe bawani na mileli miwili ya kati ya mikia yao ni mirefu. Wana mdomo mwenye nguvu na ncha kwa umbo la kulabu. Wanaweza kuogelea na kuna ngozi kati ya vidole vya miguu yao.

Ndege hawa wanaweza kupuruka sana na hufukuzia shakwe na ndege wengine wa bahari ili kupora mateka yao (kleptoparasitism). Nyakati nyingine hukamata samaki au hula mizoga na matumbo. Spishi kubwa zinaweza kuua na kula ndege wengine hata mpaka ukubwa wa Shakwe Mgongo-mweusi Mkubwa. Wakati wa majira ya kuzaa hula panya wa tundra (lemming) na mayai na makinda ya ndege wengine. Hutaga mayai yao chini kwa maeneo ya Akitiki.

Spishi za Afrika hariri

Spishi za mabara mengine hariri

Picha hariri