Sheila Kawamara Mishambi

Muandishi wa habari wa Uganda

Sheila Kawamara-Mishambi ni mwandishi wa habari wa Uganda na mkurugenzi mtendaji wa Mpango wa Msaada wa Kanda ya Afrika Mashariki kwa Maendeleo ya Wanawake EASSI na Mbunge wa zamani katika Bunge la Afrika Mashariki EALA.[1]

Sheila Kawamara
Amezaliwa Sheila Kawamara
Iganga- Uganda
Jina lingine kawamara
Kazi yake Mwandishi wa Habari na mkurugenzi mtendaji

Maisha ya awali na elimu hariri

Kawamara alizaliwa Iganga, wazazi wake wakiwa Sergio Kawamara na Helena Kajumba Kawamara ambao kwa sasa ni marehemu. Familia ilibadili makazi yake na kuishi Tooro wilaya ya Kabarole kabla ya kuelekea Kampala ambapo alianza kusoma katika shule ya msingi ya Luzira. Pia alihudhuria shule ya Shimoni.[2]

Kawamara alisoma shule ya upili ya Trinity College Nabbingo huko Kampala. Hapa ndipo alipokaidi ushauri wa kusomea sheria kama chaguo la kwanza kutoka kwa walimu wake pindi atakapojiunga na chuo kikuu na kuchagua kusomea ualimu.[3] Ana shahada kutoka Chuo Kikuu cha Makerere, taasisi ya ustawi wa jamii.

Marejeo hariri

  1. "Mishambi, Sheila K. —East African Legislative Assembly". www.eala.org. Iliwekwa mnamo 27 June 2020.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Nantaba, Agnes (2017-04-04). "Sheila Kawamara: Born to fight for rights". The Independent Uganda (kwa en-US). Iliwekwa mnamo 2020-07-14. 
  3. www.newvision.co.ug https://www.newvision.co.ug/news/1443610/trinity-junior-school-project-sh260m-boost. Iliwekwa mnamo 2020-07-14.  Missing or empty |title= (help)
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sheila Kawamara Mishambi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.