Stefan Bajcetic
Stefan Bajcetic Maquieira (alizaliwa 22 Oktoba 2004) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Hispania ambaye anacheza kama beki wa kati au kiungo wa kati katika klabu ya Liverpool.
Maisha yake ya awali hariri
Stefan Bajcetic Maquieira[1] alizaliwa tarehe 22 Oktoba 2004[2] huko Vigo Galicia, Uhispania.Ni mtoto wa mchezaji wa mpira wa miguu wa zamani wa Serbia Srđan Bajčetić na mama mgalisia.[3][4]
Maisha ya klabu hariri
Bajcetic alitoka katika akademi ya vijana ya Celta Vigo, na alisajiliwa na klabu ya Liverpool katika Premia ligi ya Uingereza mnamo Desemba 2020..[5][6][7][8]
Maendeleo ya mchezaji huyo Bajcetic ya uwanjani yalipelekea kuongezewa mkataba mpya mnamo Agosti 2022.[9] Alipata nafasi ya kuingia kwa mara ya kwanza tarehe 27 agosti akitokea benchi pindi Liverpool ilipokuwa ikicheza na klabu ya AFC Bournemouth na Liverpool kupata ushindi wa magoli 9 kwa 0 wakiwa nyumbani Anfield.[10] Pia Bajcetic alipata nafasi ya kuingia kwa mara ya kwanza katika michuano mikubwa dunia ya UEFA walipokuwa wakicheza dhidi ya klabu ya Ajax mnamo tarehe 13 september ambapo aliingia kutoa nje katika dakika za 90 , kuchukua nafasi ya mkongwe Thiago Alcântara. [11]Kwa kufanya hivyo, akawa mchezaji mwenye umri mdogo zaidi wa Liverpool kushiriki katika Ligi ya Mabingwa UEFA, na kufikia rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Billy Koumetio.[12]
Marejeo hariri
- ↑ 2022/23 Premier League squad lists. Premier League (16 September 2022).
- ↑ Stefan Bajcetic: Overview. Premier League.
- ↑ "Un meteoro vigués en Liverpool". (es)
- ↑ Stefan u dresu Srbije moja velika želja! Ne verujemo u baksuzno "ić" na Enfildu: Otac Liverpulove nade za 24sedam izneo planove za budućnost (sr).
- ↑ Celta y Liverpool acuerdan la marcha del canterano Stefan Bajcetic (es) (23 December 2020).
- ↑ O'Neill, Caoimhe (30 July 2022). Who is Stefan Bajcetic and why are Liverpool fans so excited?.
- ↑ Stefan Bajcetic: Liverpool is the best place for me to develop. Liverpool F.C..
- ↑ Bacariza, Marcos L. (23 July 2022). Stefan Bajcetic: "Valió la pena irme del Celta al Liverpool" (es). Iliwekwa mnamo 18 February 2023.
- ↑ Stefan Bajcetic signs new contract after impressive Liverpool pre-season (10 August 2022).
- ↑ Liverpool 9–0 Bournemouth: Reds record biggest ever Premier League win (27 August 2022).
- ↑ "Liverpool's Joël Matip rises to see off Ajax and ease the Anfield anxiety", 13 September 2022. Retrieved on 14 September 2022.
- ↑ Stefan Bajcetic becomes Liverpool's youngest-ever Champions League player (14 September 2022).
Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Stefan Bajcetic kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |