Vivumishi vya kumiliki

Mifano
  • Nyumba yangu imebomoka
  • Mtoto wetu amepotea
  • Mtoto wenu amepotea
  • Mtoto wao amepotea

*Maneno kama -ake, -ako, -angu, -ao na -etu huitwa pia vivumishi vimilikish.

Vivumishi vya kumiliki ni maneno yanayotoa taarifa ya kujulisha umiliki wa nomino. Maneno hayo hujulisha kuwa nomino hiyo iliyotajwa ni mali ya nani.

Mchanganuo hariri

Mashina ya vivumishi vya kumiliki yanajikita katika nafsi:

Nafsi Umoja Wingi
I -angu -etu
II -ako -enu
III -ake -ao
Mifano

Nafsi ya kwanza:

  • Nyumba yangu imebomoka - umoja
  • Shamba langu limelimwa - umoja
  • Mtoto wetu amepotea - wingi wake

Nafsi ya pili:

  • Nyumba yako imebomoka - umoja
  • Shamba lako limelimwa - umoja
  • Mtoto wenu amepotea - wingi wake

Nafsi ya tatu:

  • Nyumba yake imebomoka - umoja
  • Shamba lake limelimwa - umoja
  • Mtoto wao amepotea - wingi wake

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vivumishi vya kumiliki kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.