Wikipedia:Makala ya wiki

Maelezo
Ukitaka kupeleka makala hapa (itaonekana baadaye kwenye ukurasa wa Mwanzo kwa kubadilishana na nyingine)

  1. A) Chagua makala unaotaka kuonyesha kwenye ukurasa wa kwanza
  2. B) tunga hitimisho fupi ya makala hii (si zaidi ya alama 1100) na kuihifadhi kwa jina la Wikipedia:Makala ya wiki/XXXXXXX - badala ya XXXXXXX andika jina la makala
  3. Andika jina la makala uliyotunga hapa badala ya jina la nyingine. Usiongeze idadi kwa jumla!
  4. katika makala hii kopi Kigezo:Makala ya wiki
|jina= (jina la makala) Badala ya mabano andika jina la makala.
|picha= (jina la picha) Badala ya mabano andika jina la faili ya picha.
|nakala ya picha = (matini itakayoonekana chini ya picha) Badala ya mabano andika maelezo ya picha.
|makala = (sehemu ya makala uliyochagua - izizidi alama 1100 - 1150) Badala ya mabano andika sehemu ya makala uliyochagua - izizidi alama 1100. Tofauti na kawaida weka maneno ya kwanza yenye jina la makala kwa mabano mraba mfano [[Wolfgang Amadeus Mozart]] maanake hii inasidia kufungua makala yenyewe.

Mwisho wa maelezo - hariri chini yake


Kimondo cha chuma kilichopatikaka huko Tuva, Urusi

Vimondo (pia: meteori au meteoridi) ni magimba madogo ya angani yanayozunguka jua. Yanaweza kuangukia duniani yakionekana kama moto angani. Ukubwa wa kimondo ni kuanzia punje ya mchanga hadi kufikia kipenyo cha mita kadhaa. Hivyo kimondo ni kidogo kuliko asteoridi na kikubwa kushinda vumbi la angani. Obiti ya kimondo inaweza kuingiliana na obiti ya dunia au sayari nyingine. Kimondo kikilikaribia gimba la angani kubwa zaidi kinavutwa nalo. Kikikaribia mno dunia yetu kinaingia katika angahewa na kuanguka chini kwa kasi kubwa sana. Njiani kinapashwa moto kutokana na shindikizo la hewa dhidi yake. Kiasi cha joto kinatosha kuchoma kabisa kimondo kidogo hewani. Hii inaonekana kwa macho matupu kama mstari wa moto angani. Kama kimondo ni kikubwa zaidi ni sehemu zake za nje tu zinazochomwa na kiini kinagonga uso wa dunia. Kati ya vimondo kumi vikubwa kabisa duniani ambavyo mabaki yake yanaonekana, kimojawapo ni Kimondo cha Mbozi nchini Tanzania. ►Soma zaidi