Ben Pol
Bernard Michael Paul Mnyang’anga (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Ben Pol; amezaliwa 8 Septemba 1989) ni msanii wa muziki wa kizazi kipya na mwigizaji kutoka nchini Tanzania. Hasa anaimba muziki wa R&B.
Ben Pol | |
---|---|
Jina la kuzaliwa | Bernard Michael Paul Mnyang’anga |
Pia anajulikana kama | Ben Pol |
Amezaliwa | 8 Septemba 1989 Dar es salaam |
Kazi yake | Mwimbaji Mwigizaji |
Ala | Sauti |
Miaka ya kazi | 2009-hadi sasa |
Ameshirikiana na | Darassa, Saida Karoli, Belle 9 |
Ben Pol alianza kujulikana mnamo mwaka 2010 baada ya kutoa kibao cha "Nikikupata" ambacho kiliweza kumtambulisha katika ulimwengu wa Bongo Flava. Baadaye akaja kutamba zaidi na vibao kama vile Samboira, Moyo Mashine, Jikubali, Namba One Fan, TATU, Sophia n.k.
Kwa asili Ben ni mtu wa Dodoma[1], tena anajisifu kama mtu kutoka kanda ya kati.
Upande wa filamu, amepata kucheza katika filamu ya Sunshine na baadhi tu ya filamu zilizokuwa chini ya MFDI Tanzania na kuongozwa na Karabani.[2]
Tuzo
haririAmeshinda tuzo za mziki Tanzania (KTMA) Kwa miaka mitatu mfululizo kudhibitisha ubora wake katika muziki wa R&B.
- 2012
- 2013
- 2014
Ameshinda tuzo za www.mdundo.com
- 2016
Tuzo za hipipo Uganda
- 'Muzuki' wimbo bora wa Afrika Mashariki
Tazama pia
haririMarejeo
hariri- ↑ www.bongoswaggz.comIlihifadhiwa 19 Mei 2014 kwenye Wayback Machine. katika Bongo Swaggz
- ↑ Sunshine "Ben Pol akicheza kama m-bwia unga".
Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ben Pol kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |