Chicago ni mji mkubwa wa jimbo la Illinois na pia mji mkubwa wa tatu nchini Marekani, bada tu ya New York na Los Angeles. Iko kando ya Ziwa Michigan. Idadi ya wakazi ni 2,900,000 (2000); pamoja na rundiko la mji ni watu milioni tisa.

Mji wa Chicago






Jiji la Chicago

Bendera
Jiji la Chicago is located in Marekani
Jiji la Chicago
Jiji la Chicago

Mahali pa mji wa Chicago katika Marekani

Majiranukta: 41°50′26″N 87°40′46″W / 41.84056°N 87.67944°W / 41.84056; -87.67944
Nchi Marekani
Jimbo Illinois
Wilaya Cook
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 8,711,000
Tovuti:  www.cityofchicago.org
Nyumba kubwa za jiji la Chicago kando la ziwa Michigan

Ni mji muhimu wa biashara na viwanda. Kwa kuwa meli za Atlantiki zinafika Chicago kupitia njia ya maji ya Saint Lawrence na pia ni chanzo cha reli muhimu huitwa mara nyingi "geti la magharibi" la Marekani. Kabla ya kujengwa kwa reli mfereji muhimu uliunganisha mji na mto Mississippi.

Chanzo cha Chicago kilikuwa kituo cha biashara kwenye mdomo wa mto Chicago. Mji uliundwa 12 Agosti 1833 ukawa manispaa 1837. Wakazi waliongezeka haraka. Walikuwa 30,000 mwaka 1850, 100,000 mwaka 1860 na hadi 1880 waliongezeka kuwa 500,000. Milioni ilifikwa 1890.

Kwa miaka mingi (kati ya 1974 hadi 1998) jengo la Sears Tower lilikuwa kubwa kuliko yote duniani likiwa na kimo cha mita 442.

Historia ya Chicago hariri

Mji wa Chicago ni mji mkubwa sana katika Marekani, lakini haikuwa hivyo wakati wote. Mji wa Chicago ulianza kama ngome ndogo sana karibu na ziwa Michigan. Ngome ilijenga katika mwaka elfu moja mia nane kumi na sita kwa serikali ya Marekani. Wao walijenga hapa kwa sababu ni mhali muhimu sana. Ni muhimu kwa biashara na vita na asili ya Marekani, pia na Uingereza na Kifaransa. Ni muhimu sana kwa sababu ni katika mahali nzuri sana. Mji wa Chicago ni katika pwani la ziwa Michigan, hili ni nzuri kwa biashara na chakula kwa sababu kulikuwa na samaki sana katika ziwa. Ni nzuri kwa vita kwa sababu ni rahisi kwa meli ya jeshi ili kujengwa na kuenda mahali tofauti sana. Kwa mfano, meli ya jeshi katika iliweza kushambulia mhali katika nchi ya Canada kama maili 500 mbali.

Katika mwaka 1829, watu katika kijiji ya Chicago walijenga mfereji kutoka zima Michigan mpaka mto Mississippi. Kwa sababu ya hili watu katika kijiji ya Chicago waliweza kufanya biashara katika kila jimbo kati ya jimbo la Illinois na jimbo la Louisiana, na kwa mahali kama nchi ya Mexico au Cuba. Katika mwaka elfu moja mia nane arobaini na nane reli kutoka mashariki na Marekani na mji wa Chicago ilijengwa, reli pia alikwenda mgodi mkubwa katika kusini ya Illinois. Hili unasababishwa idadi ya watu kukua harakaharaka.

Katika tarehe nane, mwezi wa tisa, mwaka 1871 kulikuwa na moto wa Chicago, moto mkubwa sana ambayo iliteketeza mji mzima. Hadithi inasema kwamba ngombe katika mji alipiga taa juu ya nyasi nah ii ndiyo iliyoanza moto. Ilichukua miaka minne kujenga mji la Chicago tena. Majivu kutoka moto ya Chicago iliweka katika ziwa Michigan, na kwa sababu ilikuwa majivu sana, watu waliweza kujenga majengo mpya katika ardhi mpya. Baada ya moto ya Chicago, watu walianza kujenga majengo na vifaa kama chuma kwa sababu chuma haiwezi kuchoma. Kwa sababu watu walianza kujenga na chuma, waliweza kujenga majengo mrefu sana. Watu wengi wanasema kwamba mji wa Chicago ni mji wa kwanza kujenga skyscrapers.  

Jina tofauti kwa Chicago ni “The windy city”. Watu wengi wanafikiri inaitwa hii kwa sababu mji wa Chicago inakuwa na upepo sana kwa sababu ni katika ziwa Michigan, lakini watu ambaye anaishi katika Chicago wanasema ni kwa sababu ofisi ya serikali wanaweza kuongea kwa muda mrefu sana.

Sasa, idadi ya watu wa mji wa Chicago ni karibu na milioni tatu. Watu katika Chicago Metropolitan Agency for Planning (CMAP) wanafikiri kwamab katika mwaka elfu mbili hamsini, idadi ya watu wa mji wa Chicago itakuwa karibu na milioni kumi.  

Ni mji mkubwa katika Marekani kwa biashara, elimu, utalii, na huduma ya afya. Watu wakubwa katika biashara kama John Crerar, John Whitfield Bunn, Richard Teller Crane, Marshall Field, John Farwell, na Julius Rosenwald wanafanya au walifanya biashara katika mji wa Chicago. Kwa elimu, mji wa Chicago ina chuo kiku sana kama The University of Chicago, Loyola University, na DePaul University. Kuna makaburi na majengo sana katika mji wa Chicago hiyo ni maarufu sana kwa utalii. Baadhi ya haya ni kama Millennium Park, Willis Tower, na Navy Pier. Sehemu ya Navy Pier imejengwa katika majivu kutoka moto Chicago. Kila mwaka mji wa Chiacago hupata karibu na millioni hamsini watalii katika vivutio tofauti.      

Watu wengi ambaye wanaishi katika mji wa Chicago wanafikiri kwamba hali ya hewa katika mji wa Chicago ni mbaya sana. Katika majira ya kiangaiz ni joto kidogo lakini ni unyevu sana. Kila mwezi inakuwa na upepo sana na mvua au theleuji pia. Katika majira ya baridi, hali ya hewa inaweza kuanguka chini ya digrii 0 Fahrenheit. Ni kawaida katika mji wa Chicago kupata karibu na miguu kumi au kumi na tano kila mwaka. Katika majira ya joto ni kawaida kupata ngurumo au kimbunga pia.  

Mji wa Chicago ni nyumba kwa watu sana maarufu. Watu kama: Frank Lloyd Wright, Rais Obama, Derrick Rose, Walt Disney na wengine wengi sana.

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: