Mfereji
Mfereji ni njia ya maji iliyotengenezwa na watu tofauti na njia asilia za maji kama mito au maziwa.
Kuna aina mbili za mifereji:
- mfereji wa kupeleka maji yanapotakiwa kwa mfano kwa umwagiliaji wa mashamba
- mfereji wa usafiri kwa boti au meli
Mifereji ya kwanza inayojulikana ilitengenezwa zamani za Mesopotamia ya Kale, Misri ya Kale au Uhindi ya Kale kwa umwagiliaji.
Mnamo mwaka 2300 KK mfalme Pepi I aliamuru mfereji kuchimbwa kama njia ya usafiri wa kuepukana na maporomoko ya mto Naili karibu na Aswan.
Mfalme Necho II wa Misri alianzisha njia ya maji ya kwanza kati ya Mediteranea na Bahari ya Shamu kwa kuchimba mfereji kati ya mto Naili na Bahari ya Shamu. Mfereji huu ulikuwa mtangulizi wa Mfereji wa Suez.
Kati ya mifereji muhimu ya kimataifa ni Mfereji wa Panama pamoja na Mfereji wa Suez.
Kwa jumla mifereji ya maji ni sehemu muhimu za miundombinu wa kila nchi ama kama njia za kubeba mizigo kwa meli au kama njia ya kupeleka maji panapohitajika. .
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mfereji kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
|