Dawasco (kwa kirefu: Dar es Salaam Water Sewerage Cooperation) ni shirika la maji ambalo hutoa huduma ya maji katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani.

Uzalishaji wake hutokea mto Ruvu na kufanyiwa uchujaji na utakatishaji wa maji katika maeneo ya Pwani, halafu maji hayo kusambazwa maeneo yote ya Pwani na Dar es Salaam.