Hala Basha-Gorani (Kiarabu: هالة غوراني) (amezaliwa 1 Machi 1970) ni Mwamerika wa kutoka nchini Syria ambaye ni mwanahabari wa CNN International katika makao yake makuu mjini Atlanta, Georgia. Hapo awali alikuwa akitangaza kutoka afisi ya CNN jijini London, lakini sasa yuko kwa CNN International International Desk. Yeye pia alikuwa akitangaza kwa kipindi cha CNN (iliyokuwa ikionyeshwa katika siku ya Jumamosi/Jumapili) inayoitwa Inside the Middle East. Mnamo Februari 2009, ilitangazwa ya kwamba kipindi cha Inside the Middle East imesimamishwa. Hala alikuwa akitangaza kwenye kipindi cha Your World Today pamoja na Jim Clancy hadi Februari 2009 alipoanzisha kipindi chake mwenyewe (International Desk).

Hala Gorani


Hala Gorani
Amezaliwa Hala Basha Gorani
1 Machi 1970
Seattle, Marekani
Kazi yake Mwanahabari
Ndoa Fadi Ghandour (Mei 2010)
Tovuti CNN´s Hala Gorani

Wasifu hariri

Gorani alizaliwa mjini Seattle, Washington, Marekani. Wazazi wake wana asili ya kutoka Syria, mjini Aleppo; lakini alilelewa mjini Paris, Ufaransa. Yeye pia aliishi nchini Algeria. Jina la Hala ni la Kiarabu iliyo na maana ya Mwangaza. Yeye alifuzu kwa shahada ya Sayansi katika uchumi kutoka Chuo Kikuu cha George Mason karibu na mji wa Washington, DC na amemaliza kutoka Institut d'études politiques (inayojulikana kwa Kiingereza kama Sciences Po) mjini Paris mwaka wa 1995.

Kazi hariri

Ameanza kazi kama mwandishi wa habari kwa La Voix du Nord na Agence France-Presse kabla ya kujiunga na France 3 mwaka 1994. Baada ya kuacha kazi kwa Bloomberg Television jijini London, alijiunga na CNN mwaka 1998.

Yeye alijitambulisha kama mtaalamu wa matukio ya Mashariki ya Kati, akiripotia matukio kama vita vya Hezbollah-Israel katika majira ya joto ya 2006, kutoka Lebanon kama mwanahabari mkuu wa CNN. Taarifa hizi za Mashariki ya Kati ilipelekea CNN kushinda tuzo ya Edward R. Murrow kwa "Ubora katika Uanahabari ".

Gorani pia anaripoti kutoka Saudi Arabia, Iraq, Lebanon, Syria na Misri.

Mwaka wa 2002 na Aprili 2007, yeye aliripotia kuhusu uchaguzi wa rais wa Ufaransa mnamo mwaka wa 2007.

Gorani hapendi kujadiliana kuhusu maoni yake ya kisiasa na ya kidini, kwa ajili ya kutotaka kupendelea upande mmoja. Hata hivyo, taarifa yake ya Hija mnamo mwaka 2006 ilionyesha kuwa yeye ni Muislamu kwa sababu ni Waislamu tu ndio wanaoruhusiwa kuingia mjini Makkah.

Maisha ya Kibinafsi. hariri

Yeye anaongea Kiingereza, Kifaransa na Kiarabu. Anaishi mjini Atlanta.

Mwandishi wa Kifaransa anayeitwa Yann Moix alitoa wakfu wa riwaya yake ya kwanza "Jubilations hist Le ciel" kwa Gorani mwaka 1996.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri