Jahazi (Kiarabu جهاز chombo) ni mashua yenye tanga ambayo hutumika kubeba watu na shehena (mizigo).

Kundi la jahazi za Kiingereza ikielekea Uhindi mnamo mwaka 1802
Jahazi ya Kihindi Tarangini wakati wa mashindano huko Newport, Marekani mnamo 2007

Leo hutumika katika kazi za uvuvi kwa wavuvi wadogowadogo na matumizi ya usafiri, pia kama chombo cha burudani au mashindano ya kukimbizana.

Kabla ya matumizi ya injini za mvuke na injini za diseli kwenye meli kulikuwa na jahazi kubwa zilizotekeleza usafiri wa baharini. Jahazi kubwa za mwisho ziliacha kutumiwa kibiashara kwenye miaka ya 1950.

.