Joe Slovo

Mwanasiasa wa Afrika kusini

Joe Slovo (alizaliwa 23 Mei 1926 -6 Januari 1995) alikuwa mwanasiasa wa Afrika Kusini, na mpinzani wa mfumo wa ubaguzi wa rangi. Mwana -Marxist-Leninist, alikuwa kiongozi wa muda mrefu na mwananadharia katika Chama cha Kikomunisti cha Afrika Kusini (SACP), mwanachama mkuu wa African National Congress (ANC), na kamanda wa tawi la kijeshi la ANC Umkhonto we Sizwe (MK) .

Raia wa Afrika Kusini kutoka familia ya Kiyahudi-Kilithuania, Slovo alikuwa mjumbe wa Kongamano la watu wa makabila mbalimbali la Juni 1955 ambalo lilitayarisha Mkataba wa Uhuru . Alifungwa kwa miezi sita mwaka wa 1960, na akaibuka kama kiongozi wa Umkhonto we Sizwe mwaka uliofuata. Aliishi uhamishoni kutokea mwaka 1963 hadi 1990, akiendesha operesheni dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi kutoka Uingereza, Angola, Msumbiji na Zambia . Mwaka 1990 alirejea Afrika Kusini, na kushiriki katika mazungumzo yaliyomaliza ubaguzi wa rangi. Alijulikana kwa kupendekeza "vifungu vya machweo" vinavyohusu miaka 5 kufuatia uchaguzi wa kidemokrasia, ikijumuisha dhamana na makubaliano kwa pande zote, [1] na msimamo wake mkali wa kuto ubaguzi wa rangi . Baada ya uchaguzi wa mwaka 1994, alikua Waziri wa Makazi katika serikali ya Nelson Mandela . Alifariki kwa saratani mwaka wa 1995. [2]


Marejeo hariri

  1. Negotiations: What room for compromise?. www.sacp.org.za. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-05-12. Iliwekwa mnamo 25 January 2018.
  2. Joe Slovo, Anti-Apartheid Stalinist, Dies at 68, NY Times, 1995-01-07.
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Joe Slovo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.