Mto Kafue ni kati ya matawimto makubwa ya mto Zambezi; una chanzo chake kusini mwa mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Zambia. Urefu wa mwendo wake ni takriban kilomita 960.

Mto wa Kafue
Feri ya mto Kafue ndani ya hifadhi ya Kafue
Chanzo Kaskazini mwa Zambia karibu na mpaka wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Mdomo mto Zambezi mpakani na Zimbabwe
Nchi Zambia
Urefu 960 km
Kimo cha chanzo 1,350 m
Mkondo 320 m³/s wastani
Eneo la beseni km² 155,000
Miji mikubwa kando lake Kafue, Mazabuka

Inajiunga na Zambezi karibu na mji wa Chirundu (Zimbabwe).

Ni kati ya mito mikubwa ya Zambia na maji yake husaidia sana kilimo pamoja na kutengeneza umeme.

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kafue (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.