Katanga

Katanga (au Shaba, 1971-1997) ilikuwa jimbo la kusini-mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katanga (au Shaba, 1971-1997) ilikuwa jimbo la kusini-mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mahali pa Katanga katika Kongo.

Mji mkuu ulikuwa Lubumbashi (iliyoitwa Elizabethville hadi 1966). Eneo lake lilikuwa km² 496.871 na wakazi 4,125,000.

Kiswahili kilitumiwa kama lugha rasmi.

Jimbo ni maarufu kwa utajiri wake wa madini mbalimbali. Hasa mashariki mwa jimbo ni sehemu ya Kanda la Shaba linaloenea hadi Zambia. Kati ya madini yake ni kobalti, shaba, stani, radiamu, urani na almasi.

Baada ya uhuru wa Kongo mwaka 1960 jimbo lilijitenga na kuwa nchi ya pekee chini ya urais wa Moise Tshombe. Jeshi la UM lilimaliza kipindi hiki kwa nguvu ya kijeshi na kurudisha Katanga kuwa sehemu ya Kongo tena hadi Januari 1963. Katika kipindi hiki kifupi waziri mkuu wa Kongo Patrice Lumumba aliuawa katika Katanga.

Kiutawala Katanga imegawiwa katika sehemu nne kufuatana na mipango ya katiba mpya ya Kongo: Mkoa wa Tanganyika, wa Lomami Juu, wa Lualaba na wa Katanga Juu.

Makala hii kuhusu maeneo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Katanga kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.