Kikoi Vazi

mstatili wa kitamaduni wa kitambaa cha kusuka kutoka Afrika, haswa kando ya pwani ya mashariki hadi kusini kama Pembe ya Afrika.

Kikoi ni kitambaa cha utamaduni cha kusuka chenye umbo la mstatili kutoka Afrika[1]. Inachukuliwa kuwa sehemu ya utamaduni wa Waswahili, kikoi huvaliwa zaidi na Wamasai na Wakikuyu wa Kenya na pia wanaume kutoka Tanzania na Zanzibar. Kwa kawaida hutazamwa aina ya mtandio (sarong)

Mtoto aliyelala amebebwa kwenye kikoi
Mtoto aliyelala amebebwa kwenye kikoi

Maelezo hariri

Kikoi kimetengenezwa kwa pamba na michoro hufumwa badala ya kuwekwa rangi kwenye kitambaa[1]. Kama ilivyo kwa sarong zote, ni kipande kimoja cha kitambaa ambacho huzungushwa kiunoni, na kuviringishwa nje mara kadhaa. Nje ya matumizi yaliyokusudiwa kama sarong, zinaweza kutumika kama kubebea mtoto mgongoni, taulo au  kitambaa cha kufungia kichwani.

Historia hariri

Kikoi kilitokana na mabadilishano ya kitamaduni kati ya Waafrika Mashariki na washirika wao wa kibiashara kutoka mataifa kama Oman karne zilizopita[2].Mnamo 1987, mwanamitindo Iman Abdul Majjid alianzisha kikois kwenye soko la Amerika na kusambazwa na Echo Design Group[3]. Vazi hilo linasalia kuwa ukumbusho maarufu kwa watalii wanaotembelea Kenya[4].

  1. 1.0 1.1 "African Textile Collection"
  2. "Traditional Kenyan cloth becomes focus of trademark controversy"
  3. "Versatility in a Wrap Handmade in Kenya"
  4. http://content.time.com/time/travel/cityguide/article/0,31489,1974866_1974863_1974852,00.html