Lahaja sanifu (au lugha sanifu) ni lahaja ambayo imeteuliwa kutoka lahaja nyingine kutumika kwa upana zaidi kuliko lahaja za kawaida. Lahaja sanifu hutumika hasa kwa mawasiliano baina ya wasemaji wa lahaja tofauti za lugha moja; tena, hutumika katika shughuli zilizo rasmi. Ili kuwa sanifu, lahaja teule hufanyiwa marekebisho madogomadogo upande wa matamshi, sarufi na semantiki. Marekebisho hayo yanawezekana kutokea bila watu kujua.

Marejeo hariri

  • TUKI 1990, "Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
  • Massamba, David 2004, "Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
  • Buliba, Aswani, Kimani Njogu & Alice Mwihaki 2006, "Isimujamii kwa Wanafunzi wa Kiswahili", Nairobi: The Jomo Kenyatta Foundation

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lahaja sanifu kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.