Majadiliano:Nadir Haroub Ali

(Elekezwa kutoka Majadiliano:Nadir haroub Ali)
Latest comment: miaka 8 iliyopita by Kipala in topic Masahihiho ya lazima

Masahihiho ya lazima hariri

Silausi salaam, unahitaji kusafisha kasoro kadhaa, hasa tahajia na kutunga sentensi sanifu. (Naomba wenzangu tumwachie kazi hii tuone kama anaweza mwenyewe!)

  • lemma: "Nadir haroub Ali" iwe "Nadir Haroub Ali" - tumia menyu ya "more" + "hamisha" - kwenye dirisha la "Kuelekeza jina jipya:" uandike Nadir Haroub Ali, baadaye thebitisha
  • Maneno ya kwanza yaani Lemma=jina la mwenyewe kwenye makala yawe kwa maandishi koze. Nimewahi kukumbusha kuhusu hiyo, ni utaratibu hapa.
  • Hakuna jamii kwa makala ambayo ni kosa sana (ambalo mimi nimelifanya pia wakati wa kuchoka, hata hivyo kosa zito!).
  • Sentensi ya kwanza imemaliza baada ya "Yanga Sc". Hapa unapaswa kuweka nukta na kuanza sentensi ya pili (herufi kubwa kwa neno ya kwanza).
  • hakuna sababu kuandika "Beki", "Nahodha" na "Taifa" kwa herufi kubwa si neno la kwanza katika sentensi wala jina. Ziwe kwa herufi ndogo.
  • Hajazaliwa "Februali" bali "Februari" (hata tukijua sote kuna vita ya r/l kwenye mkoa wa Mbeya, wikipedia hii inasaidia kushinda!)
  • Kiswahili cha "timu hio" ni "timu hiyo"
  • Siyo katikati ya maneno " mwaka 2016 Machi" ni sentensi moja inayokwisha na nyingine inayoanza?? Basi: nukta iwepo
  • Canada kwa Kiswahili ni "Kanada", Vancover kwa lugha yote ni "Vancouver"
  • "Kuhusu Kucheza" iwe "Kuhusu kucheza"
  • Halafu inafaa kujaribu mabano mraba [[ ]] pale ambako nchi au mahali hutajwa, maana labda kuna tayari makala ya wikipedia. Ukibofya "Onyesha hakikisho la mabadiliko" utaona kama neno litakuwa buluu (=makala ipo, mabano yabaki) au nyekundu (hakuna makala bado, si lazima kuweka mabano). Jaribu hii kwa kila mahali kuanzia mahali pa kuzaliwa hadi "Vancouver".

Wasalaam --Kipala (majadiliano) 19:53, 22 Aprili 2016 (UTC)Reply

Rudi kwenye ukurasa wa " Nadir Haroub Ali ".