Toguna (au kibanda cha majadiliano) ni aina ya jengo la umma lililojengwa na Wadogon katika nchi ya Afrika Magharibi, Mali. Toguna kwa kawaida ziko katikati ya kijiji.

Toguna zimejengwa kwa paa la chini sana, kwa madhumuni ya kulazimisha wageni kukaa badala ya kusimama. Hii husaidia kuzuia vurugu wakati majadiliano yanapopamba moto. Zinatumiwa na wazee wa kijiji kujadili matatizo ya jamii, lakini pia zinaweza kutumika kama mahali pa sheria za kimila[1].

Toguna hutumiwa kama sehemu ya jumla ya mkusanyiko katikati ya kijiji, ikitoa kivuli na utulivu kutokana na joto la mchana, ambapo wazee wa kijiji hukaa saa zenye joto zaidi za siku wakizungumza wao kwa wao.

Marejeo hariri

  1. ^
  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Toguna kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.