Umma ni jumla ya watu wote katika kikundi, jamii au nchi.

Watu jamii ya Kihindi wakikusanyika kwa ajili ya Ibada

Kisosholojia, umma ni watu walio na nia sawa katika jambo fulani kama vile, wasomaji wa gazeti, watazamaji wa televisheni au kandanda ama watumiaji wa mtandao.

Katika sayansi ya siasa, umma ni wananchi wakilinganishwa na serikali ambayo hudhaniwa kuwa mtu. Serikali humiliki mali (mali ya umma) kwa niaba ya wananchi wake. Vilevile, huduma zozote zinazotolewa na serikali husemekana kuwa za umma kwa sababu umma (wananchi) ndio huigharamia serikali kwa wafanyakazi, kodi, ushuru, n.k. Kwa mfano, shule za umma.[1]

Tanbihi hariri

  1. "What is PUBLIC?", The Law Dictionary, ilipatikana 19-03-2018
  Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Umma kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.