Uzito wa kitu (jinsi chembe zilivyowekwa kwenye maada) ni kipimo cha nguvu iliyomo kwenye kitu hiko kwa kani ya mvutano. Uzito haupaswi kuchanganywa na dhana inayohusiana na masi. Kwa vitu vidogo duniani, nguvu ya uzito inaelekezwa kuelekea katikati ya sayari. Kwa vitu vingi, kama vile Mwezi unaozunguka pande zote za Dunia, nguvu inaelekezwa kuelekea katikati.

Kifaa cha kupimia uzito.

Kwa lugha ya kawaida, uzito unaweza kueleweka kirahisi pale unapopimwa karibu na dunia au kwenye uso wa dunia. Uzito kwa kawaida hupimwa kwa kutumia vizio vya masi kama vile kilogramu, gramu n.k., lakini kizio chake ni Newton (kifupi "N").

Kwa miaka mingi ya historia ya binadamu uzito umekuwa ukipimwa katika uso wa dunia. Uzito una uwiano sawa na masi. Kitu chochote chenye masi sawa kina uzito sawa. Imekuwa kawaida kuvitumia vitu hivyo viwili kila siku kwa pamoja. Kwa kawaida inawachanganya watu wengi kuhusiana na vitu hivyo viwili, masi na uzito.

Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uzito kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.