Voi

Mji nchini Kenya

Voi ni mji mkubwa wa Kaunti ya Taita-Taveta, kusini mwa Kenya. Awali ilikuwa kati ya wilaya sita za Mkoa wa Pwani.

Muonekano wa Mji wa Voi

Voi inapatikana Magharibi mwa jangwa la Taru, Kusini na Magharibi mwa Mbuga ya Kitaifa ya Tsavo Magharibi iliyo maarufu sana duniani kote.

Wakazi walikuwa 45,483 wakati wa sensa ya mwaka 2009[1].

Uchumi hariri

 
Njia panda karibu na Mji wa Voi

Voi ni soko la bidhaa za kilimo na nyama kutoka milima ya Taita na maeneo mengine jirani. Mji wa Voi una maduka ya jumla, maduka ya rejereja, soko na hoteli kadhaa. Hoteli zinazo hudumia watalii zipo viungani mwa mji. Mashamba ya makonge yapo Magharibi mwa mji. Familia kubwa ya maskota inapatikana kwenya mashamba ya makonge.

Voi ina uchumi wa saa ishirini na nne.

Historia hariri

Kulingana na historia ya wenyeji, jina la mji linatokana na mfanyibiashara muuza watumwa aliyejulikana kama Chifu Kivoi ambaye alifanya makao kwenye kingo za mto Voi takribani karne nne zilizopita. Baadae makazi hayo yalikua kituo cha biashara kwa wenyeji wataita na makabila mengine ikiwemo waarabu.

Mji ulianza kukua zaidi mwisho wa karne ya 19 wakati ujenzi wa reli ya Uganda. Watu walipata kazi katika shirika la reli na shamba la makonge. Ingawaje mji ulikuwa wa kilomita mraba 16.27 (maili mraba 6.28), ni mwaka wa 1932 ambapo ulipata hadhi ya kuwa mji. Kwa sasa mji wa Voi umepitiliza hadhi hiyo.

Usafiri hariri

Treni/Garimoshi hariri

Mji wa Voi ndio ulio na makutano ya kwanza ya reli kutuka Mombasa. Makutano haya ndio yanayo elekea Tanzania kupitia Taveta. Hivyo basi ni kituo muhimu.

Teksi hariri

Teksi zinaweza kupatikana katika kituo cha mji. Ada za nauli ni mazungumzo, si umewekwa.

Matatu hariri

Matatu zinatoa huduma za usafiri mjini na viungani mwake. Matatu pia zinasafirisha watu na bidhaa kuelekea Wundanyi, Taveta, Mombasa na maeneo mengi mengine.

Mabasi hariri

Coast bus na Mash ni baadhi ya kampuni za mabasi yanayo hudumu kwa usiku na mchana kwenda Mombasa na Nairobi.

Hewa hariri

Uwanja mdogo wa ndege Ikanga Air Strip upo karibu na mji.

  • Aina nyingine za usafiri ni pamoja na tuk tuks na pikipiki ambazo hufanya kazi  saa ishirini na nne na nauli ni nafuu sana.

Manispaa hariri

Manispaa ya Voi, ni pamoja na vijiji vya Ikanga na Mkwachunyi. Manispaa ya Voi inaongozwa na Halmashauri ya Manispaa, mamlaka za mitaa, na si chini ya Taita-Taveta County Council. Halmashauri ya Manispaa inaongozwa na meya.

Uchaguzi Kata hariri

Manispaa ya Voi imegawanywa katika kata sita, kila kata humchagua diwani mmoja

  • Kighononyi
  • Kirutai
  • Voi Kati Ya Kata
  • Voi Kaskazini-Mashariki Kata
  • Voi South Ward
  • Voi West Ward

Halmashauri ya Manispaa ya Voi hariri

Halmashauri ya Manispaa ya Voi inaongozwa na madiwani sita waliochaguliwa na kila kata na wanne wanaoteuliwa na kufanya jumla yao kuwa kumi.

Utalii na Burudani hariri

Voi ni eneo la utalii kwa kuwa inapakana na mbuga ya kitaifa ya Tsavo Mashariki iliyo maarufu duniani kote. Upande wa burudani kuna vilabu vingi.

Katika ubunifu hariri

Makala kama Xbox 360 na Halo 3 yanafanyika mjini Voi. Halo 3 unafanyika mwishoni mwa mwaka 2552, eti Voi ni taswira ya zamani ya kuwa na viwanda vingi sana, tofauti na hali halisi ya Voi.

Marejeo hariri

  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

Viungo vya nje hariri