Wangasa ni kabila dogo la watu wa Tanzania kaskazini wanaoishi upande wa mashariki wa mlima Kilimanjaro, katika mkoa wa Kilimanjaro.

Mwaka 2000 walihesabiwa kuwa 4,285, ambao kati yao 200-300 tu waliweza kutumia lugha yao, Kingasa, jamii ya Kimasai. Kwa sasa lugha mama ya wengi wao ni Kichaga na inawezekana hakuna anayejua tena Kingasa.

Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wangasa kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.