Wikimedia Foundation

Wikimedia Foundation ni shirika lisilo la kiserikali lililopo Marekani linaloendesha mradi wa Wikipedia pamoja na miradi mingine.

Nembo la Wikimedia Foundation
Wikimedia Foundation, San Francisco

Shabaha yake ni usambazaji wa elimu huria inayopatikana bure kwa watu wote kwa njia ya mtandao. Lilianzishwa na Jimmy Wales mwaka 2001. Shirika linaendeleza maendeleo ya programu huria za wikiwiki zinazomruhusu msomaji si kusoma tu bali kuandika na kuhariri vilevile.

Kwa ujumla karibia miradi yote ya Wikimedia Foundation si ya kibiashara na maudhui yote yaliyomo katika miradi hiyo hutungwa na wachangiaji wengi wanaojitolea bila malipo kutoka karibia pande zote za Dunia.

Mapato ya shirika hutokana na michango ya watu binafsi. Makampuni makubwa kama Amazon[1] na Google[2] yamewahi kutoka zawadi za dolar milioni, na mfadhili Georg Soros alituma pia zawadi ya dolar milioni 2[3] .

Mnamo mwaka 2018/2019 mapato ya taasisi yalifikia dolar milioni 120 ilhali matumizi yake yalikuwa milioni 91.[4]

Miradi mingine ya Wikimedia Foundation ukiacha ule wa Wikipedia ni pamoja na Wikamusi (Wiktionary), Wikiquote, Wikisource, Wikinews, Wikibooks, Wikiversity, Wikimedia Commons na Meta-Wiki.

Shirika hili haliangalii yaliyomo kama makala ya Wikipedia ambayo hutungwa na jumuiya za watumiaji katika lugha zinazofikia karibu 200.

Marejeo hariri

  1. Darum spendet Amazon eine Million Dollar für Wikipedia. In:derStandard.de, 26. September 2018, abgerufen am 27. September 2018.
  2. Google.org donates $2 million to Wikipedia’s parent org, Techcrunch, 22. Januar 2019
  3. George Soros, founder of Open Society Foundations, invests in the future of free and open knowledge Kaitlin Thaney, Pressemitteilung der Wikimedia-Foundation vom 15. Oktober 2018, in englischer Sprache, abgerufen am 5. März 2019
  4. Wikimedia Foundation, Inc. Financial Statements 2018 and 2019 (PDF; 350KB). Abgerufen am 11. Juli 2020.

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya elimu bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wikimedia Foundation kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.