Yusuph Godfrey Mlela (amezaliwa tarehe 11 Oktoba, 1986) ni mwigizaji wa filamu, mtunzi wa filamu na mwanamitindo kutoka nchini Tanzania. Mlela ni miongoni mwa waigizaji waliokuwa wachanga na kuja juu haraka sana. Filamu yake kwanza ilikuwa "Diversion of Love" (2006), Family Curse (2014), I Know You (2014), Shaymaa (2013), Nesi Selena (2013), Samira, Chumo na Poor Minds (2013).

Yusuph Mlema
Amezaliwa Yusuph Godfrey Mlela
11 Oktoba 1986 (1986-10-11) (umri 37)
Tabora, Tanzania
Jina lingine Angelo
Kazi yake Mwigizaji
Mwanamitindo
Miaka ya kazi 2006

Wasifu hariri

Kazi na maisha hariri

Mlela alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Kumbukumbu ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, halafu akajiunga na sekondari ya Kawawa iliyoko Mafinga mkoa wa Iringa, akiwa huko alisoma hadi kidato cha nne. Baadaye akaja kujiendeleza na masuala ya Kompyuta. Kikundi chake cha kwanza kujiunga kuhusu sanaa kinaitwa Tanganyika, kabla ya kwenda kujishuhulisha na masuala ya mitindo.[1]

Baadhi ya filamu zake hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

  1. Yusuph Mlela katika Blogu ya Wahapahapa.
  Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yusuph Mlela kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.