Admerali
Admerali (pia: admeri, admirali) ni cheo cha kiongozi mkuu wa kijeshi wa wanamaji. Cheo hicho kinalingana na jenerali katika matawi mengine ya jeshi.
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/c/c7/US_Navy_O10_insignia.svg/220px-US_Navy_O10_insignia.svg.png)
Neno linatokana na Kiarabu أمير البحر amir-al-bahr yaani "mwenye mamlaka baharini". Iliingia katika lugha za Ulaya kama "admiral".
Cheo hicho si kawaida katika jeshi la majini la Tanzania wala Kenya, lakini hutumiwa kutafsiri vyeo vya kigeni[1].
Marejeo
hariri- ↑ Linganisha "Admeri", katika Kamusi Kuu ya Kiswahili, Longhorn - Bakita 2016, ISBN 9789987020984