Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa) ni bara lenye eneo la km² 10,600,000 tu, lakini wakazi ni milioni 747 [2].

Ulaya kutoka angani.
Ulaya duniani.
Lugha za Ulaya.
Kanda za Ulaya.
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Wengi wenye asili ya Ulaya wakati wa ukoloni walitawanyika duniani, hasa Amerika, wakiathiri kote upande wa lugha, utamaduni na dini.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapoland hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Orodha ya nchi na maeneo

Jina la nchi au eneo,
bendera
Eneo
(km²)
Wakazi
(mnamo Julai 2002 takriban)
Wakazi kwa km² Mji Mkuu

Ulaya ya Mashariki:

 
Belarus
207,600 10,335,382 49.8 Minsk
 
Bulgaria
110,910 7,621,337 68.7 Sofia
 
Ucheki
78,866 10,256,760 130.1 Praha
 
Hungaria
93,030 10,075,034 108.3 Budapest
 
Moldova
33,843 4,434,547 131.0 Kishineu
 
Poland
312,685 38,625,478 123.5 Warshawa
 
Romania
238,391 21,698,181 91.0 Bukarest
 
Urusi (2)
3,960,000 106,037,143 26.8 Moscow
 
Slovakia
48,845 5,422,366 111.0 Bratislava
 
Ukraine
603,700 48,396,470 80.2 Kiev

Ulaya ya Kaskazini:

 
Denmark
43,094 5,368,854 124.6 Kopenhagen
 
Estonia
45,226 1,415,681 31.3 Tallinn
 
Visiwa vya Faroe (Denmark)
1,399 46,011 32.9 Tórshavn
 
Finland
337,030 5,183,545 15.4 Helsinki
 
Guernsey (3)
78 64,587 828.0 St Peter Port
 
Iceland
103,000 279,384 2.7 Reykjavík
 
Eire (Ireland )
70,280 3,883,159 55.3 Dublin
 
Kisiwa cha Man (3)
572 73,873 129.1 Douglas
 
Jersey (3)
116 89,775 773.9 Saint Helier
 
Latvia
64,589 2,366,515 36.6 Riga
 
Lituanya
65,200 3,601,138 55.2 Vilnius
 
Norwei
324,220 4,525,116 14.0 Oslo
 
Visiwa vya Svalbard and Jan
Mayen
(Norway)
62,049 2,868 0.046 Longyearbyen
 
Uswidi
449,964 8,876,744 19.7 Stockholm
 
Uingereza (Ufalme wa Maungano)
244,820 59,778,002 244.2 London

Ulaya ya Kusini:

 
Albania
28,748 3,544,841 123.3 Tirana
 
Andorra
468 68,403 146.2 Andorra la Vella
 
Bosnia na Herzegovina
51,129 3,964,388 77.5 Sarayevo
 
Kroatia
56,542 4,390,751 77.7 Zagreb
 
Gibraltar (Uingereza)
5.9 27,714 4,697.3 Gibraltar
 
Ugiriki
131,940 10,645,343 80.7 Athens
 
Italia
301,230 57,715,625 191.6 Roma
 
Masedonia Kaskazini
25,333 2,054,800 81.1 Skopje
 
Malta
316 397,499 1,257.9 Valletta
 
Montenegro
316 397,499 1,257.9 Podgorica
 
Ureno (6)
91,568 10,084,245 110.1 Lisbon
 
San Marino
61 27,730 454.6 San Marino
 
Serbia
102,173 10,280,000 100.6 Belgrad
 
Slovenia
20,273 1,932,917 95.3 Lyublyana
 
Hispania (7)
498,506 40,077,100 80.4 Madrid
 
Mji wa Vatikani
0.44 900 2,045.5 Mji wa Vatikani

Ulaya ya Magharibi:

 
Austria
83,858 8,169,929 97.4 Vienna
 
Ubelgiji
30,510 10,274,595 336.8 Brussels
 
Ufaransa (8)
547,030 59,765,983 109.3 Paris
 
Ujerumani (Udachi)
357,021 83,251,851 233.2 Berlin
 
Liechtenstein
160 32,842 205.3 Vaduz
 
Luxemburg
2,586 448,569 173.5 Luxemburg
 
Monako
1.95 31,987 16,403.6 Monako
 
Uholanzi (9)
41,526 16,318,199 393.0 Amsterdam, Den Haag
 
Uswisi
41,290 7,301,994 176.8 Bern

Asia ya Magharibi:

 
Armenia (10)
29,800 Yerevan
 
Azerbaijan (11)
39,730 4,198,491 105.7 Baku
 
Kupro (12)
5,995 780,133 130.1 Nikosia (Lefkosa)
 
Georgia (13)}
49,240 2,447,176 49.7 Tbilisi
 
Uturuki (14)
24,378 11,044,932 453.1 Ankara

Asia ya Kati:

 
Kazakhstan (15)
370,373 1,285,174 3.4 Astana
Total 10,431,299 709,022,061 68.0

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo

  1. Hivyo asili ya neno "Ulaya" ni sawa na "wilaya"; Krapf 1882 Swahili-English dictionary anaeleza: ""ULAYA (WALAYA au WILAYA ya) ... mother-country in contradistinction to colonies, foreign possessions or parts"; Sacleux 1939 Dictionnaire Swahili-Francais anataja kama etimolojia ya Ulaya "Ar. Hind. ولاية wilaya, pays etranger" (=nchi ya kigeni); Madan 1903 "Wilaya, n. (1) native land, home, but commonly used of foreigners, and so (2) Europe. Ulaya Uzungu, Europe. U, Hindi, India. Ulaya wa Wareno, Portugal
  2. Total population (both sexes combined) by region, subregion and country, World Population Prospects: The 2019 Revision" (xslx). population.un.org (custom data acquired via website). United Nations Department of Economic and Social Affairs, Population Division. Iliangaliwa Januari 2022