Mshigi

(Elekezwa kutoka Amandava)
Mshigi
Mshigi kinyago-chekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Passeroidea (Ndege kama shomoro)
Familia: Estrildidae (Ndege walio na mnasaba na mishigi)
Ngazi za chini

Jenasi 8:

Mishigi, shigi au sigi ni ndege wadogo wa jenasi mbalimbali katika familia Estrildidae ambao wanatokea Afrika, Asia na Australia. Takriban spishi zote za Afrika ni ndege weusi au kahawia na weupe wenye pengine sehemu za rangi kali kama nyekundu, machungwa na njano. Spishi nyingi za Asia na Australia zina rangi kali kwa kipande kikubwa cha mwili. Ndege hawa hula mbegu hasa na wadudu pia, hususa makinda. Tago lao ni tufe la manyasi lenye mwingilio kwa kando. Jike huyataga mayai 4-7.

Spishi za Afrika hariri

Spishi za mabara mengine hariri

Picha hariri