Baraba (kutoka Kiaramu bar abba בר אבא, yaani "mwana wa baba") alikuwa mwanamume wa Israeli katika karne ya 1 BK.

"Utupe Baraba!", mchoro wa 1910.

Ni maarufu hasa kwa sababu katika Injili, inaposimuliwa hukumu ya Ponsyo Pilato dhidi ya Yesu mjini Yerusalemu, inaelezwa kwamba Wayahudi waliokuwepo walimuomba Pilato kwamba kwa ajili ya Pasaka awaachie huru Baraba, si Yesu, ambaye hatimaye alisulubiwa (Mk 15:6-15; Lk 23:13-25; Yoh 18:38-19:16).[1]

Habari ya Math 27:25, kwamba hao walijitakia damu ya Yesu iwe juu yao (yaani walichukua jukumu la kifo chake badala ya Pilato aliyekuwa hataki kukiagiza), ilichangia baadaye chuki na dhuluma za baadhi ya Wakristo dhidi ya Wayahudi.[2][3]

Baraba alikuwa gerezani kama mpigania uhuru (Mk 15:7; Lk 23:19; Yoh 18:40).[4]

Tanbihi hariri

  1. Evans, Craig A. (2012-02-06). Matthew. Cambridge University Press. pp. 452–. ISBN 9780521812146. Retrieved 27 May 2015. 
  2. Pope Benedict XVI (2011). Jesus of Nazareth. Retrieved 2011-04-18. 
  3. Pope Benedict XVI Points Fingers on Who Killed Jesus (March 2, 2011). Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-03-07. Iliwekwa mnamo 2012-09-28. “While the charge of collective Jewish guilt has been an important catalyst of anti-Semitic persecution throughout history, the Catholic Church has consistently repudiated this teaching since the Second Vatican Council.”
  4. Contemporaries combining insurrection and murder in this way were sicarii, members of a militant Jewish movement that sought to overthrow the Roman occupiers of their land by force (Eisenman 177-84, et passim).

Marejeo hariri

  • Brown, Raymond E. (1994) The Death of the Messiah, Vol. 1. New York: Doubleday
  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Baraba kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.