Biomasi ni dhana muhimu katika ekolojia na ni namna ya kuangalia upande wa kimwili wa uhai duniani ni pia dhana muhimu katika maswali ya uzalishaji wa nishati hasa nishati mbadala.

Switchgrass ni aina ya nyasi inayotumiwa kwa kuzalisha biofueli huko Marekani
Maganda ya mpunga.

Jumla ya miili ya viumbehai hariri

Kimsingi biomasi ni jumla ya miili ya viumbehai vyote duniani.

Kiasi kikubwa ni mimea lakini miili ya wanyama au planktoni huhesabiwa pia. Vilevile wanyama na mimea iliyokufa, kukauka, kuoza na kadhalika ni sehemu ya biomasi. Sehemu zao hutumiwa na viumbehai vingine kama lishe la kujenga biomasi mpya.

Msingi wa biomasi ni mchakato wa usanisinuru katika mimea ambako nishati ya jua inawezesha mmea kujenga mwili wake kwa kuunganisha kemikali asilia kutoka mazingira yake.

Fueli za kisukuu kama mafuta ya petroli au makaa mawe ziliundwa pia kutokana na biomasi lakini huhesabiwa mle kwa sababu zimepitia mabadiliko na kufikia hali isiyotumiwa tena kama lishe ya viumbehai.

Kwa maana ya karibu biomasi hutajwa pia kama masi kwa eneo fulani kwa mfano biomasi ya nchi au ndani ya ziwa fulani.

Matumizi ya biomasi hariri

Biomasi inatumiwa na kila aina ya uhai kama mimea, wanyama au binadamu. Ilhali mimea inajenga mara nyini miili yao kutoka kwa minerali za ardhini ikiwezekana wanatumia pia molekuli za biomasi yaani mimea ilioyokufa na kuoza hata miili ya wanyama ambayo ni lishe bora kwao.

Biomasi inatunza nani yake pia kiasi kikubwa cha gesi ya dioksidi kabonia ambayo menginevyo ni gesi inayowezakuchangia kwa kupanda kwa halijoto duniani na ikishikwa ndani ya biomasi kasi ya kupanda kwa halijoti inachelweshwa. Kwa matumizi ya kibinadamu biomasi ni muhimu kama chanzo cha chakula hasa yaani katika kilimo.


Biomasi kama chanzo cha nishati mbadala hariri

Biomasi inatunza nishati ndani yake inayoweza kutumiwa kama fueli. Mfano unaojulikana zaidi katika maisha ya kila siku ni nishati katika ubao unaotumiwa kama kuni. Nishati iliyomo katika biomasi kiasili ni nishati ya jua inayoungwa katika mimea n.k. kwa njia ya usanisinuru na kuhifadhiwa mle katika muungo atomia kati ya molekuli zake.

Kiuchumi "biomasi" hutaja mara nyingi sehemu hizi za biomasi yote inayofaa kwa matumizi ya fueli. Kimsingi kila aina ya biomasi inaweza kufaa lakini hali halisi matumizi hutegemea teknolojia inayopatikana.

Kuna njia mbalimbali kutumia nishati iliyopo katika biomasi

  • kuchoma (kwa mfano kuni, majani makavu) na kutumia joto ama moja kwa moja (kama kupika) au kwa kuendesha rafadha kwa kutengeneza umeme.
  • kuibadilisha bioamasi kikemia, kwa mfano kuondoa gesi iliyomo ndani yake na biogesi hii inaweza kutumiwa kama umbo tofauti ya biofueli kwa kuendesha magari au rafadha za umeme
  • kutumia michakato ya kibiolojia kuvunja biomasi kama kuichachusha na kupata pia gesi au alikoholi.

Viungo vya Nje hariri

Marejeo hariri