Duteri (pia duteriumu[1], ing. Deuterium ni isotopi ya hidrojeni. Duteri ina protoni moja na nyutroni moja. Kiini cha hydrojeni ya kawaida haina nyutroni bali protoni moja tu. Alama ya Duteri ni 2H bali D hutumiwa pia.

Kuna isotopi nyingine ya hidrojeni inayoitwa triti yenye nyutroni mbili.

Atomu mbili za duteri pamoja na atomu moja ya oksijeni zinaweza kuwa molekuli ya "maji mazito". ni kama maji (H2O) lakini nzito zaidi kwa sababu ya nyutroni ya ziada.

Maji mazito hutumiwa katika aina kadhaa za tanuri nyuklia.

Tanbihi hariri

  1. Duteri ni pendekezo la KAST, duteriumu la KSBFK