George Tyson (jina la kuzaliwa George Otieno Okumu; 1973 - 30 Mei 2014) alikuwa muongozaji wa filamu kutoka Kenya.

Alijulikana kwa kuongoza filamu kama Girlfriend na Dilemma. Girlfriend ilikuwa filamu yake iliyompa sifa kiasi kikubwa nchini Tanzania. Filamu ilitayarishwa na Sultan Tamba na kusambazwa na GMC Wasanii Promoters.

Alifanya kazi hasa nchini Tanzania hadi alipofariki katika ajali ya gari akiwa anarudi kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam. Wakati wa kifo chake alikuwa na umri wa miaka 41.

Alifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwae "Sonia" (2002) na muigizaji wa filamu wa Tanzania Yvonne Cherrie Monalisa.

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu George Tyson kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.