Hifadhi ya Taifa ya Garamba

Hifadhi ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Hifadhi ya Taifa ya Garamba, Ina eneo la kilomita za mraba 2,000 za mbuga ya taifa iliyopo kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo .

Mtazamo wa anga wa hifadhi ya Garamba
Mtazamo wa anga wa hifadhi ya Garamba

Ni miongoni mwa mbuga kongwe zaidi barani Afrika, na iliteuliwa kuwa kwenye orodha ya Hifadhii ya Urithi wa Dunia na UNESCO mwaka 1980 kwa sababu ya mandhari na makazi muhimu ya vifaru weupe wa kaskazini, tembo, viboko na twiga . [1] Garamba imekuwa ikisimamiwa na shirika la African Parks kwa ushirikiano na Institut Congolais pour la Conservation de la Nature (ICCN), tangu 2005.

Historia hariri

Hifadhi ya taifa ilianzishwa mwaka wa 1938. [2] [3]

Hifadhi hiyo iliteuliwa kuwa hifadhi ya Urithi wa Dunia na UNESCO mnamo 1980, na ilijumuishwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia wa hifadhi zilizopo kwenye hatari katika shirika hilo kutoka 1984-1992. [4] [5]

Mimea na wanyama hariri

Mbuga hii yenye mandhari ya savanna inasaidia msongamano mdogo wa miguka . [6] [7] Baadhi ya nyasi za Garamba zinaweza kukua hadi futi 10 . [8]

Garamba ni makazi ya aina mbalimbali za mamalia, ikiwa ni pamoja na aina mbalimbali za swala, [9] pamoja na nyati, tembo, fisi, nguruwe wakubwa wa msituni, twiga, kiboko na simba . [10] [7] [11]

Hifadhi hii ina idadi ya twiga wa kipekee waliosalia katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, spishi ndogo za Kordofan, ambazo zina chini ya spishi 60; na mojawapo ya idadi kubwa zaidi ya tembo iliyosalia nchini. [6] [12]

Marejeo hariri

  1. Garamba National Park. UNESCO World Heritage Centre. United Nations Educational, Scientific, and Cultural Organization. Iliwekwa mnamo 13 Jun 2021.
  2. "Elephants Dying in Epic Frenzy as Ivory Fuels Wars and Profits", The New York Times, 2012. 
  3. Avant, Deborah D. (25 July 2005). The Market for Force: The Consequences of Privatizing Security. Cambridge University Press. pp. 205–206. ISBN 9780521615358. Retrieved 4 October 2017. 
  4. World Heritage Committee: Eighth Ordinary Session. UNESCO (1984). Iliwekwa mnamo 4 October 2017.
  5. World Heritage Committee: Twentieth Session. UNESCO. Iliwekwa mnamo 4 October 2017.
  6. 6.0 6.1 Canby (2016). Shootout in Garamba. The New Yorker. Condé Nast. Iliwekwa mnamo 3 October 2017.
  7. 7.0 7.1 Nicolon (9 May 2017). DRC's Garamba National Park: The last giraffes of the Congo. Mongabay. Iliwekwa mnamo 2 October 2017.
  8. Actman (2017). Go on Patrol with Elephant Guardians in New 360 Film. National Geographic. Iliwekwa mnamo 3 October 2017.
  9. East, Rod (1990). Antelopes: Global Survey and Regional Action Plans, Part 3. International Union for Conservation of Nature. p. 131. ISBN 9782831700168. Retrieved 6 October 2017. 
  10. Canby (2016). Shootout in Garamba. The New Yorker. Condé Nast. Iliwekwa mnamo 3 October 2017.
  11. "Two wildlife rangers killed by poachers in Democratic Republic of the Congo", The Guardian, London: Guardian Media Group, 25 April 2017. 
  12. Nicolon (9 May 2017). DRC's Garamba National Park: The last giraffes of the Congo. Mongabay. Iliwekwa mnamo 2 October 2017.
  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hifadhi ya Taifa ya Garamba kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.