Hussein Ali Mwinyi
Hussein Ali Mwinyi (amezaliwa 23 Desemba 1966) ni tabibu na mwanasiasa nchini Tanzania aliyechaguliwa kuwa rais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Honourable Dr Hussein Mwinyi | |
![]() Mwinyi katika 2014 | |
Aliingia ofisini 3 Novemba 2020 | |
Makamu wa Rais | Othman Masoud Sharif (kwanza) Hemed Suleiman Abdalla (pili) |
mtangulizi | Ali Mohamed Shein |
Muda wa Utawala 20 Januari 2014 – 3 Novemba 2020 | |
mtangulizi | Shamsi Vuai Nahodha |
aliyemfuata | Elias John Kwandikwa |
Muda wa Utawala 13 Februari 2008 – 7 Mai 2012 | |
mtangulizi | Juma Kapuya |
aliyemfuata | Shamsi Vuai Nahodha |
Muda wa Utawala 7 Mai 2012 – 20 Januari 2014 | |
mtangulizi | Hadji Mponda |
aliyemfuata | Seif Rashidi |
Muda wa Utawala 6 Januari 2006 – 13 Februari 2008 | |
Makamu wa Rais | Ali Mohamed Shein |
aliyemfuata | Muhammed Seif Khatib |
Muda wa Utawala 2000 – 2005 | |
Rais | Benjamin Mkapa |
Muda wa Utawala Desemba 2005 – 2020 | |
Muda wa Utawala Oktoba 2000 – 2005 | |
aliyemfuata | Adam Malima |
tarehe ya kuzaliwa | 23 Desemba 1966 Unguja, Zanzibar, Tanzania |
chama | CCM |
ndoa | Mama Mariam Mwinyi |
mahusiano | Abdullah Mwinyi (ndugu) |
makazi | Zanzibar State House |
mhitimu wa | Marmara University (MD) Hammersmith Hospital (PhD) |
Fani yake | Tabibu |
Mazoezi ya matibabu | Muhimbili Hospital (1993–95) HKMU (1998–2000) |

Baada ya kipindi cha kazi ya tiba aliingia katika siasa kwa kuchaguliwa mbunge wa Mkuranga (Mkoa wa Pwani) mwaka 2000[1] akaendelea kugombea na kuchaguliwa bungeni katika jimbo la Kwahani (Zanzibar) tangu mwaka 2005.[2] Anatokea katika chama cha CCM. Mwaka 2000 akateuliwa kuwa waziri katika serikali ya Tanzania alipokuwa naibu waziri ya afya mwaka 2000-2005, halafu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais kwa mambo ya Muungano 2006 - 2008, Waziri wa Ulinzi mwaka 2008- 2012 na tena 2014 hadi 2020. Mwaka 2012 hadi 2014 alikuwa Waziri wa Afya.
Hussein Ali Mwinyi ni mwana wa rais wa zamani Ali Hassan Mwinyi. Baada ya kusoma shule za sekondari za Azania na Tambaza, mwaka 1985 alijiunga na Chuo Kikuu cha Tiba cha Marmara huko Istanbul, Uturuki alipohitimu masomo ya tiba mwaka 1991. Aliongeza masomo kwenye chuo cha kifalme cha tiba katika hospitali ya Hammersmith huko London, Uingereza alipopata shahada za uzamili na uzamivu (PhD) mnamo 1997.
Miaka 1993-1995 alifanya kazi ya tabibu kwenye Hospitali ya Muhimbili akaendelea kuwa tabibu na mwalimu kwenye Chuo Kikuu cha Kumbukumbu cha Hubert Kairuki kwenye miaka 1998 - 2000.
Mwaka 2020 Mwinyi aliteuliwa na CCM kuwa mgombea wake kwa urais wa Zanzibar akatangazwa mshindi na kuapishwa.
Tazama pia
haririMarejeo
hariri- ↑ Member of Parliament CV, Hussein Ali Mwinyi, tovuti la bunge la Tanzania mwaka 2015, iliangaliwa kipitia archive. org mnamo Novemba 2020
- ↑ "Mengi kuhusu Hussein Ali Mwinyi". 1 Februari 2007. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-10-19. Iliwekwa mnamo 11 Novemba 2011.
Makala hiyo kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |