Hussein Ali Mwinyi

Rais wa Zanzibar

Hussein Ali Mwinyi (amezaliwa 23 Desemba 1966) ni tabibu na mwanasiasa nchini Tanzania aliyechaguliwa kuwa rais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Honourable Dr Hussein Mwinyi

Mwinyi katika 2014

Aliingia ofisini 
3 Novemba 2020
Makamu wa Rais Othman Masoud Sharif (kwanza)
Hemed Suleiman Abdalla (pili)
mtangulizi Ali Mohamed Shein

Muda wa Utawala
20 Januari 2014 – 3 Novemba 2020
mtangulizi Shamsi Vuai Nahodha
aliyemfuata Elias John Kwandikwa
Muda wa Utawala
13 Februari 2008 – 7 Mai 2012
mtangulizi Juma Kapuya
aliyemfuata Shamsi Vuai Nahodha

Muda wa Utawala
7 Mai 2012 – 20 Januari 2014
mtangulizi Hadji Mponda
aliyemfuata Seif Rashidi

Muda wa Utawala
6 Januari 2006 – 13 Februari 2008
Makamu wa Rais Ali Mohamed Shein
aliyemfuata Muhammed Seif Khatib

Muda wa Utawala
2000 – 2005
Rais Benjamin Mkapa

Muda wa Utawala
Desemba 2005 – 2020

Muda wa Utawala
Oktoba 2000 – 2005
aliyemfuata Adam Malima

tarehe ya kuzaliwa 23 Desemba 1966 (1966-12-23) (umri 58)
Unguja, Zanzibar, Tanzania
chama CCM
ndoa Mama Mariam Mwinyi
mahusiano Abdullah Mwinyi (ndugu)
makazi Zanzibar State House
mhitimu wa Marmara University (MD)
Hammersmith Hospital (PhD)
Fani yake Tabibu
Mazoezi ya matibabu Muhimbili Hospital (1993–95)
HKMU (1998–2000)
Picha ya Mwinyi (2014).

Baada ya kipindi cha kazi ya tiba aliingia katika siasa kwa kuchaguliwa mbunge wa Mkuranga (Mkoa wa Pwani) mwaka 2000[1] akaendelea kugombea na kuchaguliwa bungeni katika jimbo la Kwahani (Zanzibar) tangu mwaka 2005.[2] Anatokea katika chama cha CCM. Mwaka 2000 akateuliwa kuwa waziri katika serikali ya Tanzania alipokuwa naibu waziri ya afya mwaka 2000-2005, halafu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais kwa mambo ya Muungano 2006 - 2008, Waziri wa Ulinzi mwaka 2008- 2012 na tena 2014 hadi 2020. Mwaka 2012 hadi 2014 alikuwa Waziri wa Afya.

Hussein Ali Mwinyi ni mwana wa rais wa zamani Ali Hassan Mwinyi. Baada ya kusoma shule za sekondari za Azania na Tambaza, mwaka 1985 alijiunga na Chuo Kikuu cha Tiba cha Marmara huko Istanbul, Uturuki alipohitimu masomo ya tiba mwaka 1991. Aliongeza masomo kwenye chuo cha kifalme cha tiba katika hospitali ya Hammersmith huko London, Uingereza alipopata shahada za uzamili na uzamivu (PhD) mnamo 1997.

Miaka 1993-1995 alifanya kazi ya tabibu kwenye Hospitali ya Muhimbili akaendelea kuwa tabibu na mwalimu kwenye Chuo Kikuu cha Kumbukumbu cha Hubert Kairuki kwenye miaka 1998 - 2000.

Mwaka 2020 Mwinyi aliteuliwa na CCM kuwa mgombea wake kwa urais wa Zanzibar akatangazwa mshindi na kuapishwa.

Tazama pia

hariri

Marejeo

hariri
  1. Member of Parliament CV, Hussein Ali Mwinyi, tovuti la bunge la Tanzania mwaka 2015, iliangaliwa kipitia archive. org mnamo Novemba 2020
  2. "Mengi kuhusu Hussein Ali Mwinyi". 1 Februari 2007. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-10-19. Iliwekwa mnamo 11 Novemba 2011.