Ali Hassan Mwinyi

Rais wa pili wa Tanzania

Ali Hassan Mwinyi (8 Mei 1925 - 29 Februari 2024) alikuwa Rais wa pili wa Tanzania kuanzia mwaka 1985 hadi 1995. Aliyemtangulia ni Mwalimu Julius Nyerere, na aliyemfuata ni Benjamin Mkapa. Pia alikuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia mwaka 1990 hadi 1996.

Ali Hassan Mwinyi


Muda wa Utawala
5 November 1985 – 23 November 1995
Waziri Mkuu Joseph Sinde Warioba
mtangulizi Julius Nyerere
aliyemfuata Benjamin Mkapa

tarehe ya kuzaliwa 8 Mei 1925 (1925-05-08) (umri 98)
Tanganyika
utaifa Mtanzania
chama CCM
ndoa Siti Mwinyi
dini Uislamu
Historia ya Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
This article is part of a series
Uendo
Historia ya Zanzibar
Afrika Mashariki 1800-1845
Ukoloni
Afrika ya Mashariki ya Kijerumani
Mkataba wa Zanzibar-Helgoland
Mkwawa
Vita vya Maji Maji
Vita vikuu vya kwanza Afrika Mashariki
Tanganyika
Mapambano ya uhuru Tanganyika
Uhuru
Uhuru wa Tanganyika
Mapinduzi ya Zanzibar
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Julius Nyerere
Ujamaa
Tamko la Arusha
Vita vya Kagera
Ali Hassan Mwinyi
Benjamin Mkapa
Jakaya Kikwete
John Magufuli
Samia Suluhu Hassan

Tanzania Portal

Kabla ya hapo alikuwa Rais wa tatu wa Zanzibar baada ya kujiuzulu kwa mtangulizi wake Aboud Jumbe Mwinyi kwenye Januari 1984. Urais wa Zanzibar ulimfanya kuwa makamu wa rais wa Tanzania; hivyo aliteuliwa kugombea urais wa kitaifa wakati Julius Nyerere alipoamua kutogombea tena kwenye mwaka 1985. Mwinyi alichaguliwa akaacha cheo chake cha Zanzibar akawa rais wa Tanzania. Visiwani alifuatwa na Idris Abdul Wakil.

Kabla hajachaguliwa kuwa Rais, Mwinyi alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Makamu Rais.

Maisha hariri

Mwinyi alizaliwa Kivure kwenye Mkoa wa Pwani wa Tanzania bara lakini wazazi wake walihamia Unguja alipokuwa mdogo. Kuanzia mwaka 1933 alipokea elimu ya msingi na sekondari kwenye shule za Mangapwani na Dole Secondary School alikohitimu mwaka 1942. Baada ya masomo ya ualimu aliendelea kwenye Chuo Kikuu cha Durham nchini Uingereza [1]. .

Alianza kufundisha shuleni akaendelea kuwa mkuu wa chuo cha ualimu Unguja hadi kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya elimu ya Zanzibar baada ya mapinduzi kwenye mwaka 1963. Mnamo 1970 alipewa uwaziri wa nchi katika ofisi ya rais akaendelea na vyeo mbalimbali katika serikali ya Zanzibar, pamoja na waziri wa afya, wa mambo ya ndani na wa utalii. Alihudumia pia miaka mitano kama balozi wa Tanzania nchini Misri. Kwenye Januari 1984 aliteuliwa kuwa rais wa Zanzibar baada ya mtangulizi wake Aboud Jumbe Mwinyi alilazimishwa kujiuzulu[2]. Katika nafasi kama rais wa Zanzibar alikuwa pia makamu wa rais wa maungano; katika uchaguzi wa 1985 aliteuliwa na CCM kuwa mgombea kwa nafasi ya raisi wa taifa akachaguliwa bila mpinzani katika mfumo wa chama kimoja.

Wakati wa urais wa kitaifa wa Mwinyi, sera za Ujamaa zilianza kugeuzwa. Badala yake sera za soko huria zilianzishwa, masharti ya kuingiza bidhaa kutoka nchi za nje yalipunguzwa na uanzishaji wa biashara ya watu binafsi ulihamasishwa. Mwaka wa 1991, Mwinyi alianzisha Tume ya Nyalali iliyopendekeza kuanzisha mfumo wa vyama vingi nchini. Wakati wa awamu yake kwenye mwaka 1995 ulitokea uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi vya kisiasa nchini Tanzania.

Sera za soko huria za Mwinyi zimeendelezwa chini ya Rais Benjamin Mkapa. Mwinyi mwenyewe, baada ya kustaafu, hakujiingiza katika mambo ya siasa tena. Anaendelea kuishi huko Dar es Salaam.

 
Gazeti la Mfanyakazi la wakati huo—liliripoti habari ya ushindi wa Ali Hassan Mwinyi kwa kupata kura kwa kishindo.

Heshima na Tuzo hariri

Nishani hariri

Nishani Nchi Mwaka Ref
  Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere   Tanzania 2011

Shahada za Heshima hariri

Chuo Kikuu Nchi Shahada ya Uzamivu Mwaka Ref
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania   Tanzania Daktari wa Barua 2012 [3]
Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki   Kenya Daktari wa Usimamizi wa Biashara 2013

Tazama Pia hariri

Marejeo hariri

  1. Chancellor Hon. Dr. Ali Hassan Mwinyi, tovuti ya Kampala International University in Tanzania (KIUT), iliangaliwa Julai 2020
  2. Tanzanian Vice President Aboud Jumbe resigned Sunday from all his posts, tovuti ya UPI Archives Jan. 29, 1984, iliangaliwa Julai 2020
  3. Why OUT awarded Mzee Ruksa a honorary degree. IPP Media (24 March 2012). Iliwekwa mnamo 7 February 2013.
Alitanguliwa na
Mwinyi Aboud Jumbe
Makamu wa Rais wa Tanzania
1984-1985
Akafuatiwa na
Joseph Sinde Warioba
Alitanguliwa na
Julius Nyerere
Rais wa Tanzania
1985-1995
Akafuatiwa na
Benjamin Mkapa