Kajiado
Kajiado ni mji wa Kenya katika Bonde la Ufa la Afrika Mashariki. Mji wa Kajiado ni makao makuu ya Kaunti ya Kajiado.

Wakazi
haririIdadi ya watu wanaoishi Kajiado ni 18,281 (sensa ya 2009) [1] Ilihifadhiwa 1 Machi 2020 kwenye Wayback Machine.. Idadi kubwa ya watu wanaoishi Kajiado ni Wamasai.
Jina
haririJina la Kajiado linatokana na neno "Orkejuado" ambalo linamaanisha "mto mrefu" katika lugha ya Kimasai. Mto huu upo magharibi mwa mji huu.
Jina halisi wa mji huu ni "Olopurupurana", ambalo lina maana ya "kilima cha mviringo".
Usafiri
haririMji huu upo kusini kwa jiji la Nairobi katika barabara kuu Nairobi - Arusha.
Mji wa Kajiado una kituo katika reli ya Magadi Soda Railway ambaye inatokea Konza mpaka Magadi.
Viungo vya nje
hariri- http://www.kajiado-district-dev-trust.org.uk/kajiado.htm Ilihifadhiwa 28 Septemba 2007 kwenye Wayback Machine.
- http://www.kajiadochildrenshome.com
Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kajiado kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |