Kakao (pia: kakau[1]; kwa Kiingereza: cocoa) ni zao la mkakao linalotolewa katika mbegu iliyomo ndani ya tunda linaloitwa mkokwa.

Mbegu za kakao ndani ya mkokwa
Unga wa kakao ni msingi wa kutengeneza kinywaji na pia chokoleti

Jina hilo hutumiwa kwa ajili ya mbegu za mkakao, kwa unga unaotengenezwa kutoka mbegu hizo na pia kwa kinywaji kinachotengenezwa kwa unga wa mbegu pamoja na maji au maziwa na sukari.

Matumizi ya kakao yalianza huko Amerika ya Kati, hasa Meksiko, ambako walipenda kinywaji lakini walitumia pia mbegu kama pesa.

Mbegu ya kakao huvunjwa, hukaangwa na kusagwa; kuna mafuta mengi ndani ya mbegu, na kwa matumizi ya kinywaji ni lazima kutenganisha mafuta na unga kavu; hivyo sehemu kubwa ya mafuta ya kakao hutolewa; kwa chokoleti yanahitajika tena[2].

Mkakao hulimwa sana nchini Ghana, lakini pia Tanzania katika maeneo kama vile Kyela. Hata hivyo kwa zao hilo kumekuwa na soko gumu la kibiashara.

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kakao kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.