Kalenda ya Kiajemi

Kalenda ya Kiajemi ni kalenda rasmi katika nchi za Iran na Afghanistan. Ni kalenda ya jua yenye siku 365 na siku 366 katika mwaka mrefu. Mwaka hugawiwa kwa miezi 12.

Mkataba wa Irani uliochapishwa mwaka 1910,ukiwa unafuata kalenda ya Hijra.

Mwaka unaanza kwenye 1 Farwardin ambayo ni sawa na 21 Machi, isipokuwa katika mwaka mrefu wa Kalenda ya Gregori ni 20 Machi.

Hesabu ya miaka unafuata hijra ya Mtume Muhamad, kwa hiyo hesabu inaanza katika mwaka 622 ya kalenda ya Gregori. Mwaka 2014 wa kimataifa unalingana na miaka 1392/1393 wa kalenda ya Kiajemi.

Kalenda hiyo inatumiwa pamoja na kalenda ya Kiislamu inayoanza hesabu yake pia kwenye Hijra lakini kwa sababu ni kalenda ya mwezi miaka yake ni mifupi, hivyo mwaka 1393 wa Kiajemi unalingana na mwaka 1435 wa Kiislamu. Ilhali hesabu zote mbili zina msingi wa Kiislamu kwa kurejea hijra zinatofautishwa pia kwa kutumia majina "hijri shamsi" (hijri ya jua) na "hijri qamari" (hijri ya mwezi).

Miezi hariri

Jina Siku Jina la Kiajemi
Farvardin فروردین 31
Ordibehesht اردیبهشت 31
Khordâd خرداد 31
Tir تیر 31
Mordad مرداد 31
Shahrivar شهریور 31
Mehr مهر 30
Aban آبان 30
Azar آذر 30
Dey دی 30
Bahman بهمن 30
Esfand اسفند 29

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kalenda ya Kiajemi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.