Kihonda ni kata ya Wilaya ya Morogoro Mjini katika Mkoa wa Morogoro, Tanzania yenye Postikodi namba 67114.

Kata ya Kihonda
Majiranukta: 6°49′12″S 37°38′36″E / 6.82000°S 37.64333°E / -6.82000; 37.64333
Nchi Tanzania
Mkoa Morogoro
Wilaya Morogoro Mjini
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 35,579

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 35,579 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 44,424 waishio humo.[2] Hivyo ni kata kubwa zaidi katika Wilaya hiyo yote.

Inapatikana kwenye barabara inayoelekea Dodoma.

Kata ya Kihonda ina shule nyingi sana.

Kata ina tatizo la maji, ambalo limekuwa kero kwa wakazi, hasa kwa wale wa Kihonda Kwa Chambo.

Kata ilikuwa ikisumbuliwa na uhalifu, kama vile ujambazi na wizi. Hapo wanakata wakaitisha kikao ili kuzuia uhalifu huo wakapata njia ya kwamba usiku kuwe na walinzi waitwao sungusungu. Ingawa walikamatwa wezi, ulinzi uliendelea mpaka wezi walipotokomea.

Marejeo hariri

  Kata za Wilaya ya Morogoro Mjini - Mkoa wa Morogoro - Tanzania  

Bigwa | Boma | Chamwino | Kauzeni | Kichangani | Kihonda | Kihonda Maghorofani | Kilakala | Kingo | Kingolwira | Kiwanja cha Ndege | Luhungo | Lukobe | Mafiga | Mafisa | Magadu | Mazimbu | Mbuyuni | Mindu | Mji Mkuu | Mji Mpya | Mkundi | Mlimani | Mwembesongo | Mzinga | Sabasaba | Sultan Area | Tungi | Uwanja wa Taifa


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Morogoro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kihonda kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa na viongozi wa sasa maana wanabadilika haraka mno.