Morogoro ni jina la mto, mji, wilaya na mkoa wa Tanzania.

Mkoa wa Morogoro
Mahali paMkoa wa Morogoro
Mahali paMkoa wa Morogoro
Mahali pa Mkoa wa Morogoro katika Tanzania
Majiranukta: 8°0′S 37°0′E / 8.000°S 37.000°E / -8.000; 37.000
Nchi Tanzania
Wilaya 8
Mji mkuu Morogoro
Serikali
 - Mkuu wa Mkoa
Eneo
 - Jumla 73,039 km²
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 3,197,104
Tovuti:  http://www.morogoro.go.tz/
Mnara wa saa, Morogoro

Mkoa wa Morogoro ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye Postikodi namba 67000.

Umepakana na mikoa ya Tanga, Pwani, Lindi, Ruvuma, Iringa, Dodoma na Arusha.

Eneo lake ni km² 72 939, ambapo kuna wakazi 3,197,104 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1] (kutoka 2,218,492 wa mwaka 2012). Hivyo Morogoro ni kati ya mikoa mikubwa na yenye wakazi wengi zaidi ya Tanzania.

Jiografia hariri

Eneo la Mkoa wa Morogoro liko katikati ya mikoa ya pwani ya Bahari Hindi na Nyanda za Juu za Kusini Tanzania.

Kuna tambarare za chini kama vile Ifakara / Kilombero, pia milima ya juu kama Uluguru yenye mlima wa Kimhandu wenye mita 2646 juu ya UB.

Mito mikubwa ni Wami na Ruvu inayoanza kwenye milima ya Uluguru. Ruvu ndio mto wa kutoa maji kwa wakazi wa Dar es Salaam.

Karibu nusu ya eneo la Mkoa wa Morogoro ni hifadhi za taifa za Mikumi na sehemu ya eneo la Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na la ile ya Udzungwa.

Utawala hariri

Mkoa una wilaya tisa ambazo ndizo (katika mabano idadi ya wakazi mwaka 2022): Gairo (268,205), Kilosa (617,032), Malinyi (225,126), Mlimba (292,536), Morogoro Vijijini (387,736), Morogoro Mjini (471,409), Mvomero (421,741), Ulanga (232,895).

Wakazi walio wengi hukalia wilaya za kaskazini. Zaidi ya robo huishi katika miji ya mkoa.

Ramani Wilaya au manisipaa Wakazi (2002) Tarafa Kata Kijiji Eneo km²
 
Wilaya za Mkoa wa Morogoro
Wilaya ya Kilombero 321,611 5 19 81 14,918
Wilaya ya Kilosa 489,513 9 37 164 14,245
Wilaya ya Morogoro Vijijini 263,920 6 25 132 11,925
Wilaya ya Morogoro Mjini 227,921 1 19 - 531
Wilaya ya Mvomero 260,525 4 17 101 7,325
Wilaya ya Ulanga 193,280 5 24 65 24,560
Jumla 1,759,809 30 141 543 73,039
Makisio ya idadi ya watu kwa mwaka 2008 ni watu 2,021,714
kutokana na kiwango cha ongezeko la watu la asilimia 2.6 kwa mwaka.
Marejeo: Mkoa wa Morogoro

Wakazi hariri

Kabila kubwa ni la Waluguru waliotoa jina kwa mji wa Morogoro pamoja na milima ya Uluguru.

Makabila mengine makubwa zaidi ni Wangulu, Wakagulu, Wasagala, Wapogolo, Wandamba, Wabena, Wambungu, Wakutu na Wavidunda.

Upande wa dini, karibu nusu ni Waislamu na nusu ni Wakristo.

Mawasiliano hariri

Barabara Kuu za lami za Dar es Salaam - Morogoro - Mbeya - Zambia/Malawi na Dar es Salaam - Morogoro - Dodoma hupita eneo la mkoa pamoja na reli ya kati Dar es Salaam - Morogoro - Dodoma - Kigoma / Mwanza. Reli ya TAZARA hupita wilaya ya Kilombero.

Uchumi hariri

 
Matunda aina ya maembe yakiwa mtini huko Morogoro

Ardhi ya Morogoro ina takribani rutuba ya kufaa kwa mazao mengi. Lakini kilimo kinategemea hali ya mvua.

Karibu nusu ya eneo la mashamba yote hulimwa mahindi.

Mazao ya sokoni hulimwa milimani.

Mkoa wa Morogoro ni eneo lililojaliwa na Mungu kwa uzalishaji wa sukari kwa wingi. Hasa Wilaya ya Kilombero ina mashamba makubwa ya miwa.

Majimbo ya bunge hariri

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Morogoro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Morogoro kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa na viongozi wa sasa maana wanabadilika haraka mno.
  1. https://assengaonline.com/2022/11/05/matokeo-ya-sensa-2022-tanzania/