Kinyakyusa (au Kinyekyosa; pia huitwa Kingonde) ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wanyakyusa wanaokaa hasa Rungwe. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kinyakyusa imehesabiwa kuwa watu 805,000. Pia kuna wasemaji 300,000 nchini Malawi.

Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kinyakyusa iko katika kundi la M30.Na asili ya jina hilo la wanyakyusa ni kutokana na jina la mke wa mtawala wa kimila au chifu aliyeitwa kyusa, pia awali waliitwa wasokile hiyo ni kutokana na salamu yao asali aliyosema sooki sooki nna!

Mfumo wa sauti (fonolojia) hariri

Lugha ya Kinyakyusa ina irabu 7 na konsonanti 26. Pia, tofauti kati ya irabu fupi na irabu ndefu huleta tofauti za maana.

Mfano wa sentensi ya lugha hiyo hariri

Ubumi bwa Yesu bwali bwa pamwanya fiyo, yo nongwa bo Yehova ansyusisye ukubuka kumwanya abandu bapeliwe ulusako lwa kwikala nubumi bwa bwila na bwila.

Tafsiri ya Kiswahili: Uhai wa Yesu ulikuwa na thamani sana hivi kwamba baada ya Mungu kumfufua Yesu kwenda mbinguni, Mungu aliwapa wanadamu wote wanaomwamini Yesu fursa ya kuishi milele.

Marejeo hariri

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Felberg, Knut. 1996. Nyakyusa-English-Swahili & English-Nyakyusa dictionary. Dar es Salaam: Mkuki na Nyota Publishers. Kurasa xxii, 222. ISBN 9976-973-32-2
  • Kishindo, J. P. 1998. IkyaNgonde: a preliminary analysis. Journal of humanities (Zomba), 13, uk.59-86.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kinyakyusa kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.